< Yeremia 13 >

1 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ununue mkanda wa kitani, ujivike kiunoni mwako, lakini usiuache uguse maji.”
خداوند به من فرمود: «برو و یک کمربند کتانی بخر و به کمرت ببند، ولی آن را نشوی.»
2 Kwa hiyo nikanunua mkanda, kama Bwana alivyoniagiza, nikajivika kiunoni.
پس کمربندی خریدم و به کمرم بستم.
3 Ndipo neno la Bwana likanijia kwa mara ya pili:
سپس خداوند به من گفت:
4 “Chukua mkanda ulionunua ambao umeuvaa kiunoni mwako, uende sasa Frati uufiche ndani ya ufa mdogo kwenye mwamba.”
«به کنار رود فرات برو و آن کمربند را در شکاف صخره‌ای پنهان کن.»
5 Ndipo nikaenda na kuuficha ule mkanda huko Frati, kama Bwana alivyoniamuru.
رفتم و همان‌طور که خداوند فرموده بود، پنهانش کردم.
6 Baada ya siku nyingi Bwana akaniambia, “Nenda sasa Frati ukauchukue ule mkanda niliokuambia uufiche huko.”
پس از گذشت زمانی طولانی، خداوند فرمود که بروم و کمربند را از کنار رود فرات بیاورم.
7 Hivyo nikaenda Frati na kuuchimbua ule mkanda kutoka pale nilipokuwa nimeuficha, lakini sasa ulikuwa umeharibika na haufai tena kabisa.
من هم رفتم و آن را از جایی که پنهان کرده بودم، بیرون آوردم؛ ولی دیدم که پوسیده است و دیگر به هیچ دردی نمی‌خورد!
8 Ndipo neno la Bwana likanijia:
آنگاه خداوند فرمود: «به همین گونه من غرور مملکت یهودا و شهر اورشلیم را می‌پوسانم و از بین می‌برم.
9 “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Vivyo hivyo ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikuu cha Yerusalemu.
10 Watu hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wafuatao ukaidi wa mioyo yao na kufuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu, watakuwa kama mkanda huu ambao haufai kabisa!
این قوم بدکار که خواهان اطاعت از من نیستند و به دنبال خواهشهای ناپاک خود می‌روند و بت می‌پرستند، همچون این کمربند، پوسیده شده، به هیچ دردی نخواهند خورد.
11 Kwa maana kama vile mkanda ufungwavyo kiunoni mwa mtu, ndivyo nilivyojifunga nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda,’ asema Bwana, ‘ili wawe watu wangu kwa ajili ya utukufu wangu, sifa na heshima yangu. Lakini hawajasikiliza.’
همان‌گونه که کمربند را محکم به دور کمر می‌بندند، من نیز اسرائیل و یهودا را محکم به خود بستم تا قوم من باشند و مایهٔ سربلندی و عزت نام من گردند؛ ولی آنها از من اطاعت نکردند.»
12 “Waambie: ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo.’ Kama wao wakikuambia, ‘Kwani hatujui kwamba kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo?’
سپس خداوند فرمود: «به ایشان بگو:”همهٔ مشکهای شما از شراب پر خواهند شد.“ولی ایشان در جواب به تو خواهند گفت:”خود می‌دانیم که مشکهایمان همه از شراب لبریز خواهند شد.“
13 Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: nitawajaza ulevi wote waishio katika nchi hii, pamoja na wafalme waketio juu ya kiti cha enzi cha Daudi, makuhani, manabii na wale wote waishio Yerusalemu.
پس تو به ایشان بگو که خداوند می‌فرماید:”مردم این سرزمین را مانند کسانی که مست شده‌اند، گیج خواهم ساخت، از پادشاهی که از خاندان داوود است تا کاهنان و انبیا و همهٔ ساکنان اورشلیم را؛
14 Nitawagonganisha kila mmoja na mwenzake, baba na wana wao, asema Bwana. Sitawarehemu wala kuwahurumia ili niache kuwaangamiza.’”
و ایشان را به جان هم خواهم انداخت، حتی پدران و پسران را، تا یکدیگر را نابود کنند؛ و هیچ چیز مرا از هلاک کردن آنها باز نخواهد داشت نه دلسوزی، نه ترحم و نه شفقت.“»
15 Sikieni na mzingatie, msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amenena.
خداوند امر فرموده است، پس فروتن شوید و گوش کنید!
16 Mpeni utukufu Bwana Mungu wenu, kabla hajaleta giza, kabla miguu yenu haijajikwaa juu ya vilima vitakavyotiwa giza. Mlitarajia nuru, lakini ataifanya kuwa giza nene na kuibadili kuwa huzuni kubwa.
یهوه خدای خود را احترام نمایید، پیش از آنکه دیر شود، قبل از آنکه ظلمتی را پدید آورد که نتوانید راه خود را بر روی کوهها بیابید؛ پیش از آنکه نوری را که انتظار می‌کشیدید به تاریکی مرگبار و سهمگین تبدیل نماید.
17 Lakini kama hamtasikiliza, nitalia sirini kwa ajili ya kiburi chenu; macho yangu yatalia kwa uchungu, yakitiririka machozi, kwa sababu kundi la kondoo la Bwana litachukuliwa mateka.
اگر گوش نکنید، به سبب غرور شما در خفا خواهم گریست و اشک خواهم ریخت، چون قوم خداوند به اسارت برده می‌شوند.
18 Mwambie mfalme na mamaye, “Shukeni kutoka kwenye viti vyenu vya enzi, kwa kuwa taji zenu za utukufu zitaanguka kutoka vichwani mwenu.”
خداوند فرمود: «به پادشاه و مادرش بگو که از تخت سلطنت پایین بیایند و به خاک بنشینند، چون تاجهای پرشکوهشان از سر آنها برداشته شده است.
19 Miji iliyoko Negebu itafungwa, wala hapatakuwa na mtu wa kuifungua. Watu wa Yuda wote watapelekwa uhamishoni, wakichukuliwa kabisa waende mbali.
دروازه‌های شهرهای جنوب یهودا همه بسته است و کسی نیست که آنها را بگشاید؛ اهالی یهودا همه به اسارت رفته‌اند.
20 Inua macho yako uone wale wanaokuja kutoka kaskazini. Liko wapi lile kundi ulilokabidhiwa, kondoo wale uliojivunia?
«ای اورشلیم نگاه کن! دشمن از سوی شمال به سوی تو می‌آید! کجاست آن گلهٔ زیبایی که به دست تو سپردم تا از آن نگهداری کنی؟
21 Utasema nini Bwana atakapowaweka juu yako wale ulioungana nao kama marafiki wako maalum? Je, hutapatwa na utungu kama mwanamke aliye katika utungu wa kuzaa?
هنگامی که یارانت تو را شکست داده، بر تو حکومت کنند، چه حالی به تو دست خواهد داد؟ همچون زنی که می‌زاید، از درد به خود خواهی پیچید.
22 Nawe kama ukijiuliza, “Kwa nini haya yamenitokea?” Ni kwa sababu ya dhambi zako nyingi ndipo marinda yako yameraruliwa na mwili wako umetendewa vibaya.
اگر از خودت بپرسی که چرا این بلاها بر سرت می‌آید، بدان که به سبب ازدیاد گناهانت به این روز افتاده‌ای؛ برای همین است که دشمن به تو تجاوز نموده و غارت و پایمالت کرده است.
23 Je, Mkushi aweza kubadili ngozi yake au chui kubadili madoadoa yake? Vivyo hivyo nawe huwezi kufanya mema wewe uliyezoea kutenda mabaya.
«آیا یک حبشی می‌تواند رنگ سیاه پوستش را عوض کند؟ یا پلنگ می‌تواند خالهایش را پاک کند؟ تو هم که تا این حد به کارهای بد عادت کرده‌ای، آیا می‌توانی کار خوب بکنی؟
24 “Nitawatawanya kama makapi yapeperushwayo na upepo wa jangwani.
پس چون مرا فراموش کرده و خدایان دروغین را پیروی نموده‌ای، من هم تو را پراکنده می‌کنم، همان‌طور که باد صحرا کاه را پراکنده می‌سازد؛ این است آن سرنوشتی که برایت تعیین کرده‌ام.
25 Hii ndiyo kura yako, fungu nililokuamuria,” asema Bwana, “kwa sababu umenisahau mimi na kuamini miungu ya uongo.
26 Nitayafunua marinda yako mpaka juu ya uso wako ili aibu yako ionekane:
تو را برهنه ساخته رسوا خواهم کرد.
27 uzinzi wako na kulia kwako kama farasi kulikojaa tamaa, ukahaba wako usio na aibu! Nimeyaona matendo yako ya machukizo juu ya vilima na mashambani. Ole wako, ee Yerusalemu! Utaendelea kuwa najisi mpaka lini?”
کارهای زشت تو را دیده‌ام، ناپاکی، هوسرانی، زناکاری و بت‌پرستی‌هایت را بر تپه‌ها و کشتزارها! وای بر تو ای اورشلیم، تا به کی می‌خواهی ناپاک بمانی؟»

< Yeremia 13 >