< Yeremia 13 >

1 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ununue mkanda wa kitani, ujivike kiunoni mwako, lakini usiuache uguse maji.”
Voici ce que le Seigneur me dit: Va, et procure-toi une ceinture de lin, et tu la mettras sur tes reins, et tu ne la laveras pas dans l’eau.
2 Kwa hiyo nikanunua mkanda, kama Bwana alivyoniagiza, nikajivika kiunoni.
Et je me procurai cette ceinture, selon la parole du Seigneur, et je la mis autour de mes reins.
3 Ndipo neno la Bwana likanijia kwa mara ya pili:
Et la parole du Seigneur me fut adressée une seconde fois, disant:
4 “Chukua mkanda ulionunua ambao umeuvaa kiunoni mwako, uende sasa Frati uufiche ndani ya ufa mdogo kwenye mwamba.”
Prends la ceinture que tu t’es procurée, qui est autour de tes reins; et te levant, va vers l’Euphrate, et cache-la dans le trou d’un rocher.
5 Ndipo nikaenda na kuuficha ule mkanda huko Frati, kama Bwana alivyoniamuru.
Et j’allai, et je la cachai près de l’Euphrate, comme le Seigneur m’avait ordonné.
6 Baada ya siku nyingi Bwana akaniambia, “Nenda sasa Frati ukauchukue ule mkanda niliokuambia uufiche huko.”
Et il arriva, après plusieurs jours, que le Seigneur me dit: Lève-toi, va vers l’Euphrate, et tires-en la ceinture que je t’ai ordonné d’y cacher.
7 Hivyo nikaenda Frati na kuuchimbua ule mkanda kutoka pale nilipokuwa nimeuficha, lakini sasa ulikuwa umeharibika na haufai tena kabisa.
Et j’allai vers l’Euphrate, et je creusai, et je tirai la ceinture du lieu où je l’avais cachée; et voilà que la ceinture était pourrie, de telle sorte qu’elle n’était propre à aucun usage.
8 Ndipo neno la Bwana likanijia:
Et la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
9 “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Vivyo hivyo ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikuu cha Yerusalemu.
Voici ce que dit le Seigneur: Ainsi je ferai pourrir l’orgueil de Juda et l’orgueil excessif de Jérusalem;
10 Watu hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wafuatao ukaidi wa mioyo yao na kufuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu, watakuwa kama mkanda huu ambao haufai kabisa!
Ce peuple très méchant, qui ne veut pas entendre mes paroles et qui marche dans la dépravation de son cœur, qui a couru après des dieux étrangers, afin de les servir et de les adorer; et il sera comme cette ceinture, qui n’est propre à aucun usage.
11 Kwa maana kama vile mkanda ufungwavyo kiunoni mwa mtu, ndivyo nilivyojifunga nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda,’ asema Bwana, ‘ili wawe watu wangu kwa ajili ya utukufu wangu, sifa na heshima yangu. Lakini hawajasikiliza.’
Car comme la ceinture s’attache aux reins d’un homme, ainsi je me suis uni étroitement toute la maison d’Israël et toute la maison de Juda, dit le Seigneur, afin qu’elles fussent mon peuple, et mon nom, et ma louange, et ma gloire, et elles ne m’ont pas écouté.
12 “Waambie: ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo.’ Kama wao wakikuambia, ‘Kwani hatujui kwamba kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo?’
Tu leur diras donc cette parole: Voici ce que dit le Seigneur, Dieu d’Israël: Toute petite bouteille sera remplie de vin. Et ils te diront: Est-ce que nous ignorons que toute petite bouteille sera remplie de vin?
13 Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: nitawajaza ulevi wote waishio katika nchi hii, pamoja na wafalme waketio juu ya kiti cha enzi cha Daudi, makuhani, manabii na wale wote waishio Yerusalemu.
Et tu leur diras: Voici ce que dit le Seigneur: Voilà que moi je remplirai d’ivresse tous les habitants de cette terre, et les rois de la race de David qui sont assis sur le trône, et les prêtres et les prophètes, et tous les habitants de Jérusalem;
14 Nitawagonganisha kila mmoja na mwenzake, baba na wana wao, asema Bwana. Sitawarehemu wala kuwahurumia ili niache kuwaangamiza.’”
Et je les disperserai en séparant un homme de son frère; et les pères et les fils pareillement, dit le Seigneur; je n’épargnerai pas, et je n’accorderai rien, je n’aurai pas assez de pitié pour ne pas les perdre entièrement.
15 Sikieni na mzingatie, msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amenena.
Ecoutez et prêtez l’oreille. Ne vous enorgueillissez point; parce que c’est le Seigneur qui a parlé.
16 Mpeni utukufu Bwana Mungu wenu, kabla hajaleta giza, kabla miguu yenu haijajikwaa juu ya vilima vitakavyotiwa giza. Mlitarajia nuru, lakini ataifanya kuwa giza nene na kuibadili kuwa huzuni kubwa.
Rendez gloire au Seigneur votre Dieu, avant que les ténèbres viennent, et avant que vos pieds heurtent contre des montagnes obscures; vous attendrez la lumière, et le Seigneur la changera en ombre de mort et en une profonde obscurité.
17 Lakini kama hamtasikiliza, nitalia sirini kwa ajili ya kiburi chenu; macho yangu yatalia kwa uchungu, yakitiririka machozi, kwa sababu kundi la kondoo la Bwana litachukuliwa mateka.
Si vous n’écoutez pas cela, mon âme pleurera en secret à cause de votre orgueil: mon œil pleurant pleurera et fera couler des larmes, parce que le troupeau du Seigneur a été pris.
18 Mwambie mfalme na mamaye, “Shukeni kutoka kwenye viti vyenu vya enzi, kwa kuwa taji zenu za utukufu zitaanguka kutoka vichwani mwenu.”
Dis au roi et à la souveraine: Humiliez-vous, asseyez-vous, parce que de votre tête est tombée la couronne de votre gloire.
19 Miji iliyoko Negebu itafungwa, wala hapatakuwa na mtu wa kuifungua. Watu wa Yuda wote watapelekwa uhamishoni, wakichukuliwa kabisa waende mbali.
Les villes du midi sont fermées, et il n’y a personne qui les ouvre; tout Juda a été transféré par une transmigration entière.
20 Inua macho yako uone wale wanaokuja kutoka kaskazini. Liko wapi lile kundi ulilokabidhiwa, kondoo wale uliojivunia?
Levez vos yeux, et voyez, vous qui venez de l’aquilon; où est le troupeau qui t’a été donné, ton troupeau glorieux?
21 Utasema nini Bwana atakapowaweka juu yako wale ulioungana nao kama marafiki wako maalum? Je, hutapatwa na utungu kama mwanamke aliye katika utungu wa kuzaa?
Que diras-tu lorsque Dieu te visitera? c’est toi qui as enseigné tes ennemis contre toi-même, et qui les a instruits en exposant ta tête: est-ce que les douleurs ne te saisiront pas comme une femme en travail?
22 Nawe kama ukijiuliza, “Kwa nini haya yamenitokea?” Ni kwa sababu ya dhambi zako nyingi ndipo marinda yako yameraruliwa na mwili wako umetendewa vibaya.
Que si tu dis en ton cœur: Pourquoi sont venus sur moi ces maux? C’est à cause de la multitude de tes iniquités qu’a été mise à découvert ta honte et qu’ont été souillées les plantes de tes pieds.
23 Je, Mkushi aweza kubadili ngozi yake au chui kubadili madoadoa yake? Vivyo hivyo nawe huwezi kufanya mema wewe uliyezoea kutenda mabaya.
Si un Ethiopien peut changer sa peau, ou un léopard ses couleurs variées, vous aussi, vous pourrez faire le bien, quoique vous ayez appris le mal.
24 “Nitawatawanya kama makapi yapeperushwayo na upepo wa jangwani.
Je les disperserai comme la paille qui par le vent est emportée dans le désert.
25 Hii ndiyo kura yako, fungu nililokuamuria,” asema Bwana, “kwa sababu umenisahau mimi na kuamini miungu ya uongo.
C’est là ton sort et la part que je t’ai mesurée, dit le Seigneur, parce que tu m’as oublié, et que tu t’es confiée dans le mensonge;
26 Nitayafunua marinda yako mpaka juu ya uso wako ili aibu yako ionekane:
De là vient que moi aussi j’ai exposé ta nudité, et qu’a paru ton ignominie,
27 uzinzi wako na kulia kwako kama farasi kulikojaa tamaa, ukahaba wako usio na aibu! Nimeyaona matendo yako ya machukizo juu ya vilima na mashambani. Ole wako, ee Yerusalemu! Utaendelea kuwa najisi mpaka lini?”
Tes adultères, tes hennissements et le crime de ta fornication; sur les collines, dans les campagnes, j’ai vu tes abominations. Malheur à toi, Jérusalem! tu ne te purifieras pas en marchant à ma suite; jusques à quand encore?

< Yeremia 13 >