< Yeremia 13 >

1 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ununue mkanda wa kitani, ujivike kiunoni mwako, lakini usiuache uguse maji.”
Ainsi m'a parlé Yahweh: " Va t'acheter une ceinture de lin, et pose-là sur tes reins, mais ne la mets pas dans l'eau. "
2 Kwa hiyo nikanunua mkanda, kama Bwana alivyoniagiza, nikajivika kiunoni.
Et je m'achetai la ceinture, selon la parole de Yahweh, et je la mis sur mes reins.
3 Ndipo neno la Bwana likanijia kwa mara ya pili:
La parole de Yahweh me fut adressée une seconde fois, en ces termes:
4 “Chukua mkanda ulionunua ambao umeuvaa kiunoni mwako, uende sasa Frati uufiche ndani ya ufa mdogo kwenye mwamba.”
" Prends la ceinture que tu as achetée et qui est sur tes reins; lève-toi, va vers l'Euphrate, et là tu la cacheras dans une fente de rocher. "
5 Ndipo nikaenda na kuuficha ule mkanda huko Frati, kama Bwana alivyoniamuru.
J'allai et je la cachai près de l'Euphrate, comme Yahweh me l'avait ordonné.
6 Baada ya siku nyingi Bwana akaniambia, “Nenda sasa Frati ukauchukue ule mkanda niliokuambia uufiche huko.”
Et, au bout d'un grand nombre de jours, Yahweh me dit: " Lève-toi, va vers l'Euphrate, et là reprends la ceinture que je t'ai commandé d'y cacher ".
7 Hivyo nikaenda Frati na kuuchimbua ule mkanda kutoka pale nilipokuwa nimeuficha, lakini sasa ulikuwa umeharibika na haufai tena kabisa.
J'allai vers l'Euphrate, je creusai et je repris la ceinture au lieu où je l'avais cachée; et voilà que la ceinture était perdue, elle n'était plus bonne à rien.
8 Ndipo neno la Bwana likanijia:
Et la parole de Yahweh me fut adressée, en ces termes:
9 “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Vivyo hivyo ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikuu cha Yerusalemu.
Ainsi parle Yahweh: C'est ainsi que je perdrai l'orgueil de Juda, et le grand orgueil de Jérusalem.
10 Watu hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wafuatao ukaidi wa mioyo yao na kufuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu, watakuwa kama mkanda huu ambao haufai kabisa!
Ce peuple mauvais qui refuse d'écouter mes paroles, qui suit l'opiniâtreté de son cœur et qui va après d'autres dieux pour les servir et les adorer, il sera comme cette ceinture, qui n'est plus bonne à rien.
11 Kwa maana kama vile mkanda ufungwavyo kiunoni mwa mtu, ndivyo nilivyojifunga nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda,’ asema Bwana, ‘ili wawe watu wangu kwa ajili ya utukufu wangu, sifa na heshima yangu. Lakini hawajasikiliza.’
Car, comme la ceinture est attachée aux reins de l'homme, ainsi je m'étais attaché toute la maison d'Israël et toute la maison de Juda, — oracle de Yahweh, afin qu'elles fussent pour moi un peuple, un nom, un honneur et une gloire; mais ils n'ont pas écouté!
12 “Waambie: ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo.’ Kama wao wakikuambia, ‘Kwani hatujui kwamba kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo?’
Et tu leur diras cette parole: " Ainsi parle Yahweh, Dieu d'Israël: Toute cruche doit être remplie de vin. " Ils te répondront: " Ne savons-nous pas que toute cruche doit être remplie de vin? "
13 Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: nitawajaza ulevi wote waishio katika nchi hii, pamoja na wafalme waketio juu ya kiti cha enzi cha Daudi, makuhani, manabii na wale wote waishio Yerusalemu.
Et tu leur diras: " Ainsi parle Yahweh: Je vais remplir tous les habitants de ce pays, et les rois qui sont assis sur le trône de David, les prêtres et les prophètes, et tous les habitants de Jérusalem, d'ivresse.
14 Nitawagonganisha kila mmoja na mwenzake, baba na wana wao, asema Bwana. Sitawarehemu wala kuwahurumia ili niache kuwaangamiza.’”
Et je les briserai les uns contre les autres, les pères et les fils ensemble, — oracle de Yahweh; je n'épargnerai pas, je n'aurai pas de compassion, je n'aurai pas de pitié pour ne pas les détruire.
15 Sikieni na mzingatie, msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amenena.
Ecoutez, prêtez l'oreille, ne soyez point orgueilleux, car Yahweh a parlé.
16 Mpeni utukufu Bwana Mungu wenu, kabla hajaleta giza, kabla miguu yenu haijajikwaa juu ya vilima vitakavyotiwa giza. Mlitarajia nuru, lakini ataifanya kuwa giza nene na kuibadili kuwa huzuni kubwa.
Rendez gloire à Yahweh, votre Dieu, avant que viennent les ténèbres, que vos pieds se heurtent aux montagnes de la nuit, qu'il change en ombre de mort la lumière que vous attendez, et qu'il en fasse une obscurité profonde.
17 Lakini kama hamtasikiliza, nitalia sirini kwa ajili ya kiburi chenu; macho yangu yatalia kwa uchungu, yakitiririka machozi, kwa sababu kundi la kondoo la Bwana litachukuliwa mateka.
Si vous n'écoutez pas cela, mon âme pleurera en secret, à cause de votre orgueil; mes yeux pleureront amèrement, se fondront en larmes, car le troupeau de Jacob sera emmené captif.
18 Mwambie mfalme na mamaye, “Shukeni kutoka kwenye viti vyenu vya enzi, kwa kuwa taji zenu za utukufu zitaanguka kutoka vichwani mwenu.”
Dis au roi et à la reine: Asseyez-vous à terre, car elle tombe de votre tête, votre couronne de gloire.
19 Miji iliyoko Negebu itafungwa, wala hapatakuwa na mtu wa kuifungua. Watu wa Yuda wote watapelekwa uhamishoni, wakichukuliwa kabisa waende mbali.
Les villes du midi sont fermées, et personne ne les ouvre; Juda tout entier est déporté; la déportation est complète.
20 Inua macho yako uone wale wanaokuja kutoka kaskazini. Liko wapi lile kundi ulilokabidhiwa, kondoo wale uliojivunia?
Lève les yeux et vois ceux qui viennent du septentrion: Où est le troupeau qui t'avait été donné, les brebis qui faisaient ta gloire?
21 Utasema nini Bwana atakapowaweka juu yako wale ulioungana nao kama marafiki wako maalum? Je, hutapatwa na utungu kama mwanamke aliye katika utungu wa kuzaa?
Que diras-tu quand Yahweh te donnera pour maîtres ceux que tu as instuits contre toi — tes familiers? Les douleurs ne te saisiront-elles pas, comme une femme qui enfante?
22 Nawe kama ukijiuliza, “Kwa nini haya yamenitokea?” Ni kwa sababu ya dhambi zako nyingi ndipo marinda yako yameraruliwa na mwili wako umetendewa vibaya.
Et si tu dis dans ton cœur: " Pourquoi ces malheurs m'arrivent-ils?... " C'est à cause de la multitude de tes iniquités que les pans de ta robe ont été relevés, que tes talons ont été meurtris.
23 Je, Mkushi aweza kubadili ngozi yake au chui kubadili madoadoa yake? Vivyo hivyo nawe huwezi kufanya mema wewe uliyezoea kutenda mabaya.
Un Ethiopien changera-t-il sa peau, un léopard ses taches? Et vous, pourriez-vous faire le bien, vous qui êtes appris à mal faire?
24 “Nitawatawanya kama makapi yapeperushwayo na upepo wa jangwani.
Je les disperserai comme la paille qui passe, au souffle du vent du désert.
25 Hii ndiyo kura yako, fungu nililokuamuria,” asema Bwana, “kwa sababu umenisahau mimi na kuamini miungu ya uongo.
Tel est ton sort, la part que je te mesure, — oracle de Yahweh, parce que tu m'as oublié, que tu as mis ta confiance dans le mensonge.
26 Nitayafunua marinda yako mpaka juu ya uso wako ili aibu yako ionekane:
Et moi aussi je relèverai les pans de ta robe sur ton visage, et l'on verra ta honte.
27 uzinzi wako na kulia kwako kama farasi kulikojaa tamaa, ukahaba wako usio na aibu! Nimeyaona matendo yako ya machukizo juu ya vilima na mashambani. Ole wako, ee Yerusalemu! Utaendelea kuwa najisi mpaka lini?”
Tes adultères, tes hennissements, tes criminelles prostitutions, sur les collines en pleine campagne, toutes tes abominations, je les ai vues. Malheur à toi, Jérusalem! Tu es impure jusques à quand encore?

< Yeremia 13 >