< Yeremia 13 >

1 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ununue mkanda wa kitani, ujivike kiunoni mwako, lakini usiuache uguse maji.”
Thus said the LORD unto me: 'Go, and get thee a linen girdle, and put it upon thy loins, and put it not in water.'
2 Kwa hiyo nikanunua mkanda, kama Bwana alivyoniagiza, nikajivika kiunoni.
So I got a girdle according to the word of the LORD, and put it upon my loins.
3 Ndipo neno la Bwana likanijia kwa mara ya pili:
And the word of the LORD came unto me the second time, saying:
4 “Chukua mkanda ulionunua ambao umeuvaa kiunoni mwako, uende sasa Frati uufiche ndani ya ufa mdogo kwenye mwamba.”
'Take the girdle that thou hast gotten, which is upon thy loins, and arise, go to Perath, and hide it there in a cleft of the rock.'
5 Ndipo nikaenda na kuuficha ule mkanda huko Frati, kama Bwana alivyoniamuru.
So I went, and hid it in Perath, as the LORD commanded me.
6 Baada ya siku nyingi Bwana akaniambia, “Nenda sasa Frati ukauchukue ule mkanda niliokuambia uufiche huko.”
And it came to pass after many days, that the LORD said unto me: 'Arise, go to Perath, and take the girdle from thence, which I commanded thee to hide there.'
7 Hivyo nikaenda Frati na kuuchimbua ule mkanda kutoka pale nilipokuwa nimeuficha, lakini sasa ulikuwa umeharibika na haufai tena kabisa.
Then I went to Perath, and digged, and took the girdle from the place where I had hid it; and, behold, the girdle was marred, it was profitable for nothing.
8 Ndipo neno la Bwana likanijia:
Then the word of the LORD came unto me, saying:
9 “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Vivyo hivyo ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikuu cha Yerusalemu.
Thus saith the LORD: After this manner will I mar the pride of Judah, and the great pride of Jerusalem,
10 Watu hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wafuatao ukaidi wa mioyo yao na kufuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu, watakuwa kama mkanda huu ambao haufai kabisa!
even this evil people, that refuse to hear My words, that walk in the stubbornness of their heart, and are gone after other gods to serve them, and to worship them, that it be as this girdle, which is profitable for nothing.
11 Kwa maana kama vile mkanda ufungwavyo kiunoni mwa mtu, ndivyo nilivyojifunga nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda,’ asema Bwana, ‘ili wawe watu wangu kwa ajili ya utukufu wangu, sifa na heshima yangu. Lakini hawajasikiliza.’
For as the girdle cleaveth to the loins of a man, so have I caused to cleave unto Me the whole house of Israel and the whole house of Judah, saith the LORD, that they might be unto Me for a people, and for a name, and for a praise, and for a glory; but they would not hearken.
12 “Waambie: ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo.’ Kama wao wakikuambia, ‘Kwani hatujui kwamba kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo?’
Moreover thou shalt speak unto them this word: Thus saith the LORD, the God of Israel: 'Every bottle is filled with wine'; and when they shall say unto thee: 'Do we not know that every bottle is filled with wine?'
13 Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: nitawajaza ulevi wote waishio katika nchi hii, pamoja na wafalme waketio juu ya kiti cha enzi cha Daudi, makuhani, manabii na wale wote waishio Yerusalemu.
Then shalt thou say unto them: Thus saith the LORD: Behold, I will fill all the inhabitants of this land, even the kings that sit upon David's throne, and the priests, and the prophets, and all the inhabitants of Jerusalem, with drunkenness.
14 Nitawagonganisha kila mmoja na mwenzake, baba na wana wao, asema Bwana. Sitawarehemu wala kuwahurumia ili niache kuwaangamiza.’”
And I will dash them one against another, even the fathers and the sons together, saith the LORD; I will not pity, nor spare, nor have compassion, that I should not destroy them.
15 Sikieni na mzingatie, msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amenena.
Hear ye, and give ear, be not proud; for the LORD hath spoken.
16 Mpeni utukufu Bwana Mungu wenu, kabla hajaleta giza, kabla miguu yenu haijajikwaa juu ya vilima vitakavyotiwa giza. Mlitarajia nuru, lakini ataifanya kuwa giza nene na kuibadili kuwa huzuni kubwa.
Give glory to the LORD your God, before it grow dark, and before your feet stumble upon the mountains of twilight, and, while ye look for light, He turn it into the shadow of death, and make it gross darkness.
17 Lakini kama hamtasikiliza, nitalia sirini kwa ajili ya kiburi chenu; macho yangu yatalia kwa uchungu, yakitiririka machozi, kwa sababu kundi la kondoo la Bwana litachukuliwa mateka.
But if ye will not hear it, my soul shall weep in secret for your pride; and mine eyes shall weep sore, and run down with tears, because the LORD'S flock is carried away captive.
18 Mwambie mfalme na mamaye, “Shukeni kutoka kwenye viti vyenu vya enzi, kwa kuwa taji zenu za utukufu zitaanguka kutoka vichwani mwenu.”
Say thou unto the king and to the queen-mother: 'Sit ye down low; for your headtires are come down, even your beautiful crown.'
19 Miji iliyoko Negebu itafungwa, wala hapatakuwa na mtu wa kuifungua. Watu wa Yuda wote watapelekwa uhamishoni, wakichukuliwa kabisa waende mbali.
The cities of the South are shut up, and there is none to open them; Judah is carried away captive all of it; it is wholly carried away captive.
20 Inua macho yako uone wale wanaokuja kutoka kaskazini. Liko wapi lile kundi ulilokabidhiwa, kondoo wale uliojivunia?
Lift up your eyes, and behold them that come from the north; where is the flock that was given thee, thy beautiful flock?
21 Utasema nini Bwana atakapowaweka juu yako wale ulioungana nao kama marafiki wako maalum? Je, hutapatwa na utungu kama mwanamke aliye katika utungu wa kuzaa?
What wilt thou say, when He shall set the friends over thee as head, whom thou thyself hast trained against thee? Shall not pangs take hold of thee, as of a woman in travail?
22 Nawe kama ukijiuliza, “Kwa nini haya yamenitokea?” Ni kwa sababu ya dhambi zako nyingi ndipo marinda yako yameraruliwa na mwili wako umetendewa vibaya.
And if thou say in thy heart: 'Wherefore are these things befallen me?' — for the greatness of thine iniquity are thy skirts uncovered, and thy heels suffer violence.
23 Je, Mkushi aweza kubadili ngozi yake au chui kubadili madoadoa yake? Vivyo hivyo nawe huwezi kufanya mema wewe uliyezoea kutenda mabaya.
Can the Ethiopian change his skin, or the leopard his spots? Then may ye also do good, that are accustomed to do evil.
24 “Nitawatawanya kama makapi yapeperushwayo na upepo wa jangwani.
Therefore will I scatter them, as the stubble that passeth away by the wind of the wilderness.
25 Hii ndiyo kura yako, fungu nililokuamuria,” asema Bwana, “kwa sababu umenisahau mimi na kuamini miungu ya uongo.
This is thy lot, the portion measured unto thee from Me, saith the LORD; because thou hast forgotten Me, and trusted in falsehood.
26 Nitayafunua marinda yako mpaka juu ya uso wako ili aibu yako ionekane:
Therefore will I also uncover thy skirts upon thy face, and thy shame shall appear.
27 uzinzi wako na kulia kwako kama farasi kulikojaa tamaa, ukahaba wako usio na aibu! Nimeyaona matendo yako ya machukizo juu ya vilima na mashambani. Ole wako, ee Yerusalemu! Utaendelea kuwa najisi mpaka lini?”
Thine adulteries, and thy neighings, the lewdness of thy harlotry, on the hills in the field have I seen thy detestable acts. Woe unto thee, O Jerusalem! thou wilt not be made clean! When shall it ever be?

< Yeremia 13 >