< Yeremia 12 >
1 Wewe daima u mwenye haki, Ee Bwana, niletapo mashtaka mbele yako. Hata hivyo nitazungumza nawe kuhusu hukumu yako: Kwa nini njia ya waovu inafanikiwa? Kwa nini wasio waaminifu wote wanaishi kwa raha?
Davamı önüne getirsem, Haklı çıkarsın, ya RAB. Ama adalet konusunda Seninle tartışmak istiyorum. Neden kötülerin işi iyi gidiyor? Neden hainler tasasızca yaşıyor?
2 Umewapanda, nao wameota, wanakua na kuzaa matunda. Daima u midomoni mwao, lakini mbali na mioyo yao.
Onları sen diktin, kök saldılar, Büyüyüp ürün verdiler. Adın ağızlarından düşmüyor, Yürekleriyse senden uzak.
3 Hata hivyo unanijua mimi, Ee Bwana; unaniona na kuyachunguza mawazo yangu kukuhusu wewe. Wakokote kama kondoo wanaokwenda kuchinjwa! Watenge kwa ajili ya siku ya kuchinjwa!
Beni tanırsın, ya RAB, Beni görür, yüreğimin seninle olduğunu bilirsin. Kasaplık koyun gibi ayır onları, Kesim gününe hazırla!
4 Je, nchi itakaa katika hali ya kuomboleza mpaka lini, na majani katika kila shamba kunyauka? Kwa sababu wale waishio ndani yake ni waovu, wanyama na ndege wameangamia. Zaidi ya hayo, watu wanasema, “Bwana hataona yatakayotupata sisi.”
İçinde yaşayanların kötülüğü yüzünden, Ülke ne zamana dek yas tutacak, Otlar ne zamana dek sararıp solacak? Hayvanlarla kuşlar yok oldu. Çünkü bu halk, “O başımıza neler geleceğini görmüyor” dedi.
5 “Ikiwa umeshindana mbio na watu kwa mguu na wakakushinda, unawezaje kushindana na farasi? Ikiwa unajikwaa kwenye nchi ambayo ni salama, utawezaje kwenye vichaka kando ya Yordani?
“Ey Yeremya, İnsanlarla yarışa girip yoruldunsa, Atlarla nasıl yarışacaksın? Güvenli bir ülkede sendelersen, Şeria çalılıklarıyla nasıl başa çıkacaksın?
6 Ndugu zako, watu wa jamaa yako mwenyewe: hata wao wamekusaliti; wameinua kilio kikubwa dhidi yako. Usiwaamini, ingawa wanazungumza mema juu yako.
Kardeşlerin, öz ailen bile sana ihanet etti, Arkandan seslerini yükselttiler. Yüzüne karşı olumlu konuşsalar bile onlara güvenme.
7 “Nitaiacha nyumba yangu, nitupe urithi wangu; nitamtia yeye nimpendaye mikononi mwa adui zake.
Evimi terk ettim, Mirasımı reddettim, Sevgilimi düşmanlarının eline verdim.
8 Urithi wangu umekuwa kwangu kama simba wa msituni. Huningurumia mimi, kwa hiyo ninamchukia.
Mirasım karşımda Ormandaki aslan gibi oldu; Kükreyip üzerime saldırdı. Bu yüzden ondan nefret ediyorum.
9 Je, urithi wangu haukuwa kama ndege wa mawindo wa madoadoa ambaye ndege wengine wawindao humzunguka na kumshambulia? Nenda ukawakusanye pamoja wanyama wote wa mwituni; walete ili wale.
Mirasım sırtlan ya da yırtıcı kuş mu oldu karşımda? Çevresindeki yırtıcı kuşlar saldırıyor ona. Gidin, bütün yabanıl hayvanları toplayıp getirin, Yiyip bitirsinler onu.
10 Wachungaji wengi wataliharibu shamba langu la mizabibu na kulikanyaga shamba langu; watalifanya shamba langu zuri kuwa jangwa la ukiwa.
Pek çok çoban bağımı bozdu, Tarlamı çiğnedi, Güzelim tarlamı ıssız çöle döndürdü.
11 Litafanywa kuwa jangwa, lililokauka na kuachwa ukiwa mbele zangu; nchi yote itafanywa jangwa kwa sababu hakuna hata mmoja anayejali.
Onu viraneye çevirdiler, Önümde viran olmuş ağlıyor; Bütün ülke viran olmuş, Yine de aldıran yok.
12 Juu ya miinuko yote ilivyo kama jangwani mharabu atajaa, kwa maana upanga wa Bwana utawala, kuanzia ncha moja ya nchi hadi nyingine; hakuna hata mmoja atakayekuwa salama.
Çöldeki çıplak tepelere Yıkıcılar geldi. RAB'bin kılıcı ülkeyi Bir uçtan bir uca yiyip bitiriyor. Kimse kavuşmayacak esenliğe.
13 Watapanda ngano lakini watavuna miiba; watajitaabisha lakini hawatafaidi chochote. Kwa hiyo beba aibu ya mavuno yako kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.”
Halkım buğday ekip diken biçti, Emek verip yarar görmedi. RAB'bin kızgın öfkesi yüzünden Ürününüzden utanacaksınız.”
14 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa habari ya majirani zangu wote wabaya wanaonyangʼanya urithi ambao ninawapa watu wangu Israeli, nitawangʼoa kutoka nchi zao, nami nitaingʼoa nyumba ya Yuda kutoka katikati yao.
RAB diyor ki, “Halkım İsrail'e verdiğim mülke el koyan bütün kötü komşularımı ülkelerinden söküp atacak, Yahuda halkını da atacağım.
15 Lakini baada ya kuwangʼoa, nitawahurumia tena na kumrudisha kila mmoja wao kwenye urithi wake mwenyewe na kwenye nchi yake mwenyewe.
Hepsini söküp attıktan sonra Yahuda'ya yine acıyacak, her birini kendi mülküne, kendi ülkesine geri getireceğim.
16 Ikiwa watajifunza vyema njia za watu wangu na kuapa kwa Jina langu, wakisema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo,’ hata kama wakati fulani walifundisha watu wangu kuapa kwa Baali, ndipo watakapofanywa imara katikati ya watu wangu.
Halkıma Baal'ın adıyla ant içmeyi öğrettiler. Bunun gibi, halkımın yolunda yürümeyi ve ‘RAB'bin varlığı hakkı için’ diyerek benim adımla ant içmeyi de iyice öğrenirlerse, halkımın arasında sağlam yerleri olacak.
17 Lakini kama taifa lolote halitasikiliza na kutii, nitalingʼoa kabisa na kuliangamiza,” asema Bwana.
Ama kulak asmayan her ulusu kökünden söküp atacak, yok edeceğim” diyor RAB.