< Yeremia 12 >

1 Wewe daima u mwenye haki, Ee Bwana, niletapo mashtaka mbele yako. Hata hivyo nitazungumza nawe kuhusu hukumu yako: Kwa nini njia ya waovu inafanikiwa? Kwa nini wasio waaminifu wote wanaishi kwa raha?
Vous êtes certainement juste, vous, Seigneur, si je dispute avec vous; cependant je vous dirai des choses justes: Pourquoi la voie des impies est-elle prospère, et le bonheur est-il pour tous ceux qui prévariquent, et qui agissent iniquement?
2 Umewapanda, nao wameota, wanakua na kuzaa matunda. Daima u midomoni mwao, lakini mbali na mioyo yao.
Vous les avez plantés, et ils ont poussé des racines; ils croissent, et font du fruit; vous êtes près de leur bouche, et loin de leurs reins.
3 Hata hivyo unanijua mimi, Ee Bwana; unaniona na kuyachunguza mawazo yangu kukuhusu wewe. Wakokote kama kondoo wanaokwenda kuchinjwa! Watenge kwa ajili ya siku ya kuchinjwa!
Et vous, Seigneur, vous m’avez connu, vous m’avez vu et vous avez éprouvé que mon cœur est avec vous; assemblez-les comme un troupeau destiné au sacrifice, et consacrez-les pour le jour de la tuerie.
4 Je, nchi itakaa katika hali ya kuomboleza mpaka lini, na majani katika kila shamba kunyauka? Kwa sababu wale waishio ndani yake ni waovu, wanyama na ndege wameangamia. Zaidi ya hayo, watu wanasema, “Bwana hataona yatakayotupata sisi.”
Jusques à quand la terre pleurera-t-elle, et l’herbe de toute la contrée sera-t-elle desséchée, à cause de la méchanceté de ceux qui l’habitent? le quadrupède et le volatile ont été consumés, parce que ces hommes ont dit: Dieu ne verra pas nos derniers moments.
5 “Ikiwa umeshindana mbio na watu kwa mguu na wakakushinda, unawezaje kushindana na farasi? Ikiwa unajikwaa kwenye nchi ambayo ni salama, utawezaje kwenye vichaka kando ya Yordani?
Si en courant avec les piétons, tu t’es fatigué, comment pourras-tu le disputer de vitesse aux chevaux? mais si dans une terre de paix tu étais en sûreté, que feras-tu au milieu de l’orgueil du Jourdain?
6 Ndugu zako, watu wa jamaa yako mwenyewe: hata wao wamekusaliti; wameinua kilio kikubwa dhidi yako. Usiwaamini, ingawa wanazungumza mema juu yako.
Car tes frères et la maison de ton père, eux aussi ont combattu contre toi, et ont crié derrière toi à pleine voix; ne les crois pas, lorsqu’ils te donneront de bonnes paroles.
7 “Nitaiacha nyumba yangu, nitupe urithi wangu; nitamtia yeye nimpendaye mikononi mwa adui zake.
J’ai laissé ma maison; j’ai abandonné mon héritage; j’ai livré mon âme chérie aux mains de ses ennemis.
8 Urithi wangu umekuwa kwangu kama simba wa msituni. Huningurumia mimi, kwa hiyo ninamchukia.
Mon héritage est devenu pour moi comme un lion dans la forêt; il a élevé sa voix contre moi; c’est pour cela que je l’ai haï.
9 Je, urithi wangu haukuwa kama ndege wa mawindo wa madoadoa ambaye ndege wengine wawindao humzunguka na kumshambulia? Nenda ukawakusanye pamoja wanyama wote wa mwituni; walete ili wale.
Est-ce que mon héritage n’est pas pour moi un oiseau de diverses couleurs? n’est-ce pas un oiseau entièrement coloré? venez, assemblez-vous, vous toutes, bêtes de la terre; hâtez-vous pour dévorer.
10 Wachungaji wengi wataliharibu shamba langu la mizabibu na kulikanyaga shamba langu; watalifanya shamba langu zuri kuwa jangwa la ukiwa.
Des pasteurs nombreux ont ravagé ma vigne, ils ont foulé aux pieds mon partage; ils ont fait de mon partage précieux un désert solitaire.
11 Litafanywa kuwa jangwa, lililokauka na kuachwa ukiwa mbele zangu; nchi yote itafanywa jangwa kwa sababu hakuna hata mmoja anayejali.
Ils l’ont livré à la dévastation, et il a pleuré sur moi; par la désolation a été désolée toute la terre, parce qu’il n’est personne qui réfléchisse en son cœur.
12 Juu ya miinuko yote ilivyo kama jangwani mharabu atajaa, kwa maana upanga wa Bwana utawala, kuanzia ncha moja ya nchi hadi nyingine; hakuna hata mmoja atakayekuwa salama.
Sur toutes les voies du désert sont venus des dévastateurs; parce que le glaive du Seigneur dévorera d’une extrémité de la terre à son autre extrémité; il n’y a de paix pour aucune chair.
13 Watapanda ngano lakini watavuna miiba; watajitaabisha lakini hawatafaidi chochote. Kwa hiyo beba aibu ya mavuno yako kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.”
Ils ont semé du froment, et ils ont moissonné des épines; ils ont reçu un héritage, et il ne leur servira pas; vous serez confondus par la perte de vos fruits, à cause de la colère de la fureur du Seigneur.
14 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa habari ya majirani zangu wote wabaya wanaonyangʼanya urithi ambao ninawapa watu wangu Israeli, nitawangʼoa kutoka nchi zao, nami nitaingʼoa nyumba ya Yuda kutoka katikati yao.
Voici ce que dit le Seigneur contre tous ces voisins très méchants, qui touchent à l’héritage que j’ai distribué à mon peuple d’Israël: Voilà que moi je les arracherai de leur terre, et que j’arracherai la maison de Juda du milieu d’eux.
15 Lakini baada ya kuwangʼoa, nitawahurumia tena na kumrudisha kila mmoja wao kwenye urithi wake mwenyewe na kwenye nchi yake mwenyewe.
Et lorsque je les aurai ainsi déracinés, je me tournerai et j’aurai pitié d’eux, et je les ramènerai l’un dans son héritage, et l’autre dans sa terre.
16 Ikiwa watajifunza vyema njia za watu wangu na kuapa kwa Jina langu, wakisema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo,’ hata kama wakati fulani walifundisha watu wangu kuapa kwa Baali, ndipo watakapofanywa imara katikati ya watu wangu.
Et il arrivera que si, instruits, ils apprennent les voies de mon peuple et jurent par mon nom: Le Seigneur vit! comme ils ont appris à mon peuple à jurer par Baal, ils seront établis au milieu de mon peuple.
17 Lakini kama taifa lolote halitasikiliza na kutii, nitalingʼoa kabisa na kuliangamiza,” asema Bwana.
Que s’ils n’écoutent point ma voix, je les extirperai par l’extirpation et par la ruine, dit le Seigneur.

< Yeremia 12 >