< Yeremia 12 >

1 Wewe daima u mwenye haki, Ee Bwana, niletapo mashtaka mbele yako. Hata hivyo nitazungumza nawe kuhusu hukumu yako: Kwa nini njia ya waovu inafanikiwa? Kwa nini wasio waaminifu wote wanaishi kwa raha?
Éternel! tu es juste quand je conteste avec toi; toutefois je parlerai avec toi de [tes] jugements. Pourquoi la voie des méchants est-elle prospère? [Pourquoi] ceux qui agissent très perfidement sont-ils en paix?
2 Umewapanda, nao wameota, wanakua na kuzaa matunda. Daima u midomoni mwao, lakini mbali na mioyo yao.
Tu les as plantés, même ils prennent racine; ils progressent, même ils portent du fruit. Tu es près, dans leur bouche, mais tu es loin de leurs reins.
3 Hata hivyo unanijua mimi, Ee Bwana; unaniona na kuyachunguza mawazo yangu kukuhusu wewe. Wakokote kama kondoo wanaokwenda kuchinjwa! Watenge kwa ajili ya siku ya kuchinjwa!
Mais toi, Éternel! tu me connais, tu m’as vu, et tu as éprouvé mon cœur à ton égard. Traîne-les comme des brebis à la tuerie, et mets-les à part pour le jour de la tuerie.
4 Je, nchi itakaa katika hali ya kuomboleza mpaka lini, na majani katika kila shamba kunyauka? Kwa sababu wale waishio ndani yake ni waovu, wanyama na ndege wameangamia. Zaidi ya hayo, watu wanasema, “Bwana hataona yatakayotupata sisi.”
Jusques à quand le pays mènera-t-il deuil et l’herbe de tous les champs séchera-t-elle? À cause de l’iniquité de ceux qui y habitent, le bétail et les oiseaux périssent; car ils disent: Il ne verra pas notre fin.
5 “Ikiwa umeshindana mbio na watu kwa mguu na wakakushinda, unawezaje kushindana na farasi? Ikiwa unajikwaa kwenye nchi ambayo ni salama, utawezaje kwenye vichaka kando ya Yordani?
Si tu as couru avec les piétons, et qu’ils t’aient lassé, comment rivaliseras-tu avec les chevaux? Et si, dans une terre de paix, tu te crois en sécurité, que feras-tu quand le Jourdain sera enflé?
6 Ndugu zako, watu wa jamaa yako mwenyewe: hata wao wamekusaliti; wameinua kilio kikubwa dhidi yako. Usiwaamini, ingawa wanazungumza mema juu yako.
Car tes frères aussi et la maison de ton père, eux aussi ont agi perfidement envers toi, eux aussi ont crié après toi à plein gosier. Ne les crois point, même s’ils te disent de bonnes [paroles].
7 “Nitaiacha nyumba yangu, nitupe urithi wangu; nitamtia yeye nimpendaye mikononi mwa adui zake.
J’ai abandonné ma maison, j’ai délaissé mon héritage, j’ai livré le bien-aimé de mon âme en la main de ses ennemis.
8 Urithi wangu umekuwa kwangu kama simba wa msituni. Huningurumia mimi, kwa hiyo ninamchukia.
Mon héritage m’est devenu comme un lion dans la forêt; il a fait retentir sa voix contre moi, c’est pourquoi je l’ai haï.
9 Je, urithi wangu haukuwa kama ndege wa mawindo wa madoadoa ambaye ndege wengine wawindao humzunguka na kumshambulia? Nenda ukawakusanye pamoja wanyama wote wa mwituni; walete ili wale.
Mon héritage m’est comme un oiseau de proie tacheté; les oiseaux de proie sont contre lui, tout à l’entour. Venez, assemblez toutes les bêtes des champs, faites-les venir pour dévorer.
10 Wachungaji wengi wataliharibu shamba langu la mizabibu na kulikanyaga shamba langu; watalifanya shamba langu zuri kuwa jangwa la ukiwa.
Plusieurs pasteurs ont gâté ma vigne, ils ont foulé mon lot, ils ont réduit le lot de mon désir en un désert aride;
11 Litafanywa kuwa jangwa, lililokauka na kuachwa ukiwa mbele zangu; nchi yote itafanywa jangwa kwa sababu hakuna hata mmoja anayejali.
on en a fait une désolation; tout désolé, il mène deuil devant moi; toute la terre est dévastée, car personne ne la prend à cœur.
12 Juu ya miinuko yote ilivyo kama jangwani mharabu atajaa, kwa maana upanga wa Bwana utawala, kuanzia ncha moja ya nchi hadi nyingine; hakuna hata mmoja atakayekuwa salama.
Sur toutes les hauteurs dans le désert sont venus les destructeurs; car l’épée de l’Éternel dévore depuis un bout du pays jusqu’à l’autre bout du pays: il n’y a de paix pour aucune chair.
13 Watapanda ngano lakini watavuna miiba; watajitaabisha lakini hawatafaidi chochote. Kwa hiyo beba aibu ya mavuno yako kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.”
Ils ont semé du froment, et ils moissonnent des épines; ils se sont tourmentés, [et] ils n’en ont pas eu de profit: soyez confus du rapport de vos [champs], à cause de l’ardeur de la colère de l’Éternel.
14 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa habari ya majirani zangu wote wabaya wanaonyangʼanya urithi ambao ninawapa watu wangu Israeli, nitawangʼoa kutoka nchi zao, nami nitaingʼoa nyumba ya Yuda kutoka katikati yao.
Ainsi dit l’Éternel contre tous mes mauvais voisins qui mettent la main sur l’héritage que j’ai fait hériter à mon peuple, à Israël: Voici, je les arracherai de dessus leur sol, et j’arracherai la maison de Juda du milieu d’eux.
15 Lakini baada ya kuwangʼoa, nitawahurumia tena na kumrudisha kila mmoja wao kwenye urithi wake mwenyewe na kwenye nchi yake mwenyewe.
Et il arrivera qu’après que je les aurai arrachés, je leur ferai de nouveau miséricorde et je les ferai retourner chacun à son héritage et chacun dans son pays.
16 Ikiwa watajifunza vyema njia za watu wangu na kuapa kwa Jina langu, wakisema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo,’ hata kama wakati fulani walifundisha watu wangu kuapa kwa Baali, ndipo watakapofanywa imara katikati ya watu wangu.
Et il arrivera que, s’ils apprennent diligemment les voies de mon peuple, pour jurer par mon nom: L’Éternel est vivant! comme ils ont enseigné à mon peuple à jurer par Baal, ils seront édifiés au milieu de mon peuple.
17 Lakini kama taifa lolote halitasikiliza na kutii, nitalingʼoa kabisa na kuliangamiza,” asema Bwana.
Et s’ils n’écoutent pas, j’arracherai entièrement cette nation-là et je la ferai périr, dit l’Éternel.

< Yeremia 12 >