< Yeremia 12 >
1 Wewe daima u mwenye haki, Ee Bwana, niletapo mashtaka mbele yako. Hata hivyo nitazungumza nawe kuhusu hukumu yako: Kwa nini njia ya waovu inafanikiwa? Kwa nini wasio waaminifu wote wanaishi kwa raha?
righteous you(m. s.) LORD for to contend to(wards) you surely justice: judgement to speak: speak with you why? way: journey wicked to prosper to prosper all to act treacherously treachery
2 Umewapanda, nao wameota, wanakua na kuzaa matunda. Daima u midomoni mwao, lakini mbali na mioyo yao.
to plant them also to uproot to go: continue also to make fruit near you(m. s.) in/on/with lip their and distant from kidney their
3 Hata hivyo unanijua mimi, Ee Bwana; unaniona na kuyachunguza mawazo yangu kukuhusu wewe. Wakokote kama kondoo wanaokwenda kuchinjwa! Watenge kwa ajili ya siku ya kuchinjwa!
and you(m. s.) LORD to know me to see: see me and to test heart my with you to tear them like/as flock to/for slaughtered and to consecrate: prepare them to/for day slaughter
4 Je, nchi itakaa katika hali ya kuomboleza mpaka lini, na majani katika kila shamba kunyauka? Kwa sababu wale waishio ndani yake ni waovu, wanyama na ndege wameangamia. Zaidi ya hayo, watu wanasema, “Bwana hataona yatakayotupata sisi.”
till how to mourn [the] land: country/planet and vegetation all [the] land: country to wither from distress: evil to dwell in/on/with her to snatch animal and bird for to say not to see: see [obj] end our
5 “Ikiwa umeshindana mbio na watu kwa mguu na wakakushinda, unawezaje kushindana na farasi? Ikiwa unajikwaa kwenye nchi ambayo ni salama, utawezaje kwenye vichaka kando ya Yordani?
for with on foot to run: run and be weary you and how? to contend with [the] horse and in/on/with land: country/planet peace: well-being you(m. s.) to trust and how? to make: do in/on/with pride [the] Jordan
6 Ndugu zako, watu wa jamaa yako mwenyewe: hata wao wamekusaliti; wameinua kilio kikubwa dhidi yako. Usiwaamini, ingawa wanazungumza mema juu yako.
for also brother: male-sibling your and house: household father your also they(masc.) to act treacherously in/on/with you also they(masc.) to call: call out after you full not be faithful in/on/with them for to speak: speak to(wards) you welfare
7 “Nitaiacha nyumba yangu, nitupe urithi wangu; nitamtia yeye nimpendaye mikononi mwa adui zake.
to leave: forsake [obj] house: temple my to leave [obj] inheritance my to give: give [obj] beloved soul my in/on/with palm enemy her
8 Urithi wangu umekuwa kwangu kama simba wa msituni. Huningurumia mimi, kwa hiyo ninamchukia.
to be to/for me inheritance my like/as lion in/on/with wood to give: cry out upon me in/on/with voice her upon so to hate her
9 Je, urithi wangu haukuwa kama ndege wa mawindo wa madoadoa ambaye ndege wengine wawindao humzunguka na kumshambulia? Nenda ukawakusanye pamoja wanyama wote wa mwituni; walete ili wale.
bird of prey variegated inheritance my to/for me bird of prey around upon her to go: went to gather all living thing [the] land: wildlife to come to/for food
10 Wachungaji wengi wataliharibu shamba langu la mizabibu na kulikanyaga shamba langu; watalifanya shamba langu zuri kuwa jangwa la ukiwa.
to pasture many to ruin vineyard my to trample [obj] portion my to give: make [obj] portion desire my to/for wilderness devastation
11 Litafanywa kuwa jangwa, lililokauka na kuachwa ukiwa mbele zangu; nchi yote itafanywa jangwa kwa sababu hakuna hata mmoja anayejali.
to set: make her to/for devastated to mourn upon me devastation be desolate: destroyed all [the] land: country/planet for nothing man: anyone to set: put upon heart
12 Juu ya miinuko yote ilivyo kama jangwani mharabu atajaa, kwa maana upanga wa Bwana utawala, kuanzia ncha moja ya nchi hadi nyingine; hakuna hata mmoja atakayekuwa salama.
upon all bareness in/on/with wilderness to come (in): come to ruin for sword to/for LORD to eat from end land: country/planet and till end [the] land: country/planet nothing peace to/for all flesh
13 Watapanda ngano lakini watavuna miiba; watajitaabisha lakini hawatafaidi chochote. Kwa hiyo beba aibu ya mavuno yako kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.”
to sow wheat and thorn to reap be weak: weak not to gain and be ashamed from produce your from burning anger face: anger LORD
14 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa habari ya majirani zangu wote wabaya wanaonyangʼanya urithi ambao ninawapa watu wangu Israeli, nitawangʼoa kutoka nchi zao, nami nitaingʼoa nyumba ya Yuda kutoka katikati yao.
thus to say LORD upon all neighboring my [the] bad: evil [the] to touch in/on/with inheritance which to inherit [obj] people my [obj] Israel look! I to uproot them from upon land: soil their and [obj] house: household Judah to uproot from midst their
15 Lakini baada ya kuwangʼoa, nitawahurumia tena na kumrudisha kila mmoja wao kwenye urithi wake mwenyewe na kwenye nchi yake mwenyewe.
and to be after to uproot I [obj] them to return: again and to have compassion them and to return: again them man: anyone to/for inheritance his and man: anyone to/for land: country/planet his
16 Ikiwa watajifunza vyema njia za watu wangu na kuapa kwa Jina langu, wakisema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo,’ hata kama wakati fulani walifundisha watu wangu kuapa kwa Baali, ndipo watakapofanywa imara katikati ya watu wangu.
and to be if to learn: learn to learn: teach [obj] way: conduct people my to/for to swear in/on/with name my alive LORD like/as as which to learn: learn [obj] people my to/for to swear in/on/with Baal and to build in/on/with midst people my
17 Lakini kama taifa lolote halitasikiliza na kutii, nitalingʼoa kabisa na kuliangamiza,” asema Bwana.
and if not to hear: hear and to uproot [obj] [the] nation [the] he/she/it to uproot and to perish utterance LORD