< Yeremia 12 >

1 Wewe daima u mwenye haki, Ee Bwana, niletapo mashtaka mbele yako. Hata hivyo nitazungumza nawe kuhusu hukumu yako: Kwa nini njia ya waovu inafanikiwa? Kwa nini wasio waaminifu wote wanaishi kwa raha?
O Lord, if I dispute with thee, thou art righteous: yet let mee talke with thee of thy iudgements: wherefore doeth the way of the wicked prosper? why are all they in wealth that rebelliously transgresse?
2 Umewapanda, nao wameota, wanakua na kuzaa matunda. Daima u midomoni mwao, lakini mbali na mioyo yao.
Thou hast planted them, and they haue taken roote: they grow, and bring forth fruite: thou art neere in their mouth, and farre from their reines.
3 Hata hivyo unanijua mimi, Ee Bwana; unaniona na kuyachunguza mawazo yangu kukuhusu wewe. Wakokote kama kondoo wanaokwenda kuchinjwa! Watenge kwa ajili ya siku ya kuchinjwa!
But thou, Lord, knowest me: thou hast seene me, and tried mine heart towarde thee: pull them out like sheepe for the slaughter, and prepare them for the day of slaughter.
4 Je, nchi itakaa katika hali ya kuomboleza mpaka lini, na majani katika kila shamba kunyauka? Kwa sababu wale waishio ndani yake ni waovu, wanyama na ndege wameangamia. Zaidi ya hayo, watu wanasema, “Bwana hataona yatakayotupata sisi.”
Howe long shall the lande mourne, and the herbes of euery fielde wither, for the wickednesse of them that dwell therein? the beastes are consumed and the birdes, because they sayd, He wil not see our last ende.
5 “Ikiwa umeshindana mbio na watu kwa mguu na wakakushinda, unawezaje kushindana na farasi? Ikiwa unajikwaa kwenye nchi ambayo ni salama, utawezaje kwenye vichaka kando ya Yordani?
If thou hast runne with the footemen and they haue wearied thee, then howe canst thou match thy selfe with horses? and if thou thoughtest thy selfe safe in a peaceable lande, what wilt thou do in the swelling of Iorden?
6 Ndugu zako, watu wa jamaa yako mwenyewe: hata wao wamekusaliti; wameinua kilio kikubwa dhidi yako. Usiwaamini, ingawa wanazungumza mema juu yako.
For euen thy brethren, and the house of thy father, euen they haue delt vnfaithfully with thee, and they haue cryed out altogether vpon thee: but beleeue them not, though they speake faire to thee.
7 “Nitaiacha nyumba yangu, nitupe urithi wangu; nitamtia yeye nimpendaye mikononi mwa adui zake.
I haue forsaken mine house: I haue left mine heritage: I haue giuen the dearely beloued of my soule into the hands of her enemies.
8 Urithi wangu umekuwa kwangu kama simba wa msituni. Huningurumia mimi, kwa hiyo ninamchukia.
Mine heritage is vnto mee, as a lion in the forest: it crieth out against mee, therefore haue I hated it.
9 Je, urithi wangu haukuwa kama ndege wa mawindo wa madoadoa ambaye ndege wengine wawindao humzunguka na kumshambulia? Nenda ukawakusanye pamoja wanyama wote wa mwituni; walete ili wale.
Shall mine heritage bee vnto mee, as a bird of diuers colours? are not the birdes about her, saying, Come, assemble all ye beastes of the fielde, come to eate her?
10 Wachungaji wengi wataliharibu shamba langu la mizabibu na kulikanyaga shamba langu; watalifanya shamba langu zuri kuwa jangwa la ukiwa.
Many pastors haue destroyed my vineyarde, and troden my portion vnder foote: of my pleasant portion they haue made a desolate wildernesse.
11 Litafanywa kuwa jangwa, lililokauka na kuachwa ukiwa mbele zangu; nchi yote itafanywa jangwa kwa sababu hakuna hata mmoja anayejali.
They haue layde it waste, and it, being waste, mourneth vnto me: and the whole lande lyeth waste, because no man setteth his minde on it.
12 Juu ya miinuko yote ilivyo kama jangwani mharabu atajaa, kwa maana upanga wa Bwana utawala, kuanzia ncha moja ya nchi hadi nyingine; hakuna hata mmoja atakayekuwa salama.
The destroyers are come vpon all the high places in the wildernesse: for the sworde of the Lord shall deuoure from the one end of the land, euen to the other ende of the lande: no flesh shall haue peace.
13 Watapanda ngano lakini watavuna miiba; watajitaabisha lakini hawatafaidi chochote. Kwa hiyo beba aibu ya mavuno yako kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.”
They haue sowen wheate, and reaped thornes: they were sicke, and had no profite: and they were ashamed of your fruites, because of the fierce wrath of the Lord.
14 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa habari ya majirani zangu wote wabaya wanaonyangʼanya urithi ambao ninawapa watu wangu Israeli, nitawangʼoa kutoka nchi zao, nami nitaingʼoa nyumba ya Yuda kutoka katikati yao.
Thus sayeth the Lord against all mine euill neighbours, that touch the inheritance, which I haue caused my people Israel to inherite, Beholde, I will plucke them out of their lande, and plucke out the house of Iudah from among them.
15 Lakini baada ya kuwangʼoa, nitawahurumia tena na kumrudisha kila mmoja wao kwenye urithi wake mwenyewe na kwenye nchi yake mwenyewe.
And after that I haue plucked them out, I will returne, and haue compassion on them, and will bring againe euery man to his heritage, and euery man to his land.
16 Ikiwa watajifunza vyema njia za watu wangu na kuapa kwa Jina langu, wakisema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo,’ hata kama wakati fulani walifundisha watu wangu kuapa kwa Baali, ndipo watakapofanywa imara katikati ya watu wangu.
And if they will learne the wayes of my people, to sweare by my Name, (The Lord liueth, as they taught my people to sweare by Baal) then shall they be built in the middes of my people.
17 Lakini kama taifa lolote halitasikiliza na kutii, nitalingʼoa kabisa na kuliangamiza,” asema Bwana.
But if they will not obey, then will I vtterly plucke vp, and destroy that nation, sayeth the Lord.

< Yeremia 12 >