< Yeremia 11 >
1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
Beseda, ki je prišla k Jeremiju od Gospoda, rekoč:
2 “Sikia maneno ya agano hili, nawe uwaambie watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu.
»Poslušaj besede te zaveze in govori možem iz Juda in prebivalcem [prestolnice] Jeruzalem
3 Waambie kwamba hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Amelaaniwa mtu ambaye hatayatii maneno ya agano hili,
in jim reci: ›Tako govori Gospod, Izraelov Bog: ›Preklet bodi mož, ki ne uboga besed te zaveze,
4 maneno niliyowaamuru baba zenu nilipowatoa katika nchi ya Misri, kutoka tanuru la kuyeyushia vyuma.’ Nilisema, ‘Nitiini mimi na mfanye kila kitu ninachowaamuru, nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.
ki sem jo zapovedal vašim očetom na dan, ko sem jih izpeljal iz egiptovske dežele, iz železne talilne peči, rekoč: ›Ubogajte moj glas in jih izvršujte, glede na vse, kar vam zapovedujem. Tako boste moje ljudstvo in jaz bom vaš Bog,
5 Kisha nitatimiza kiapo nilichowaapia baba zenu, kuwapa nchi itiririkayo maziwa na asali,’ nchi ambayo mnaimiliki leo.” Nikajibu, “Amen, Bwana.”
da bom lahko izpolnil prisego, ki sem jo prisegel vašim očetom, da jim dam deželo, kjer tečeta mleko in med, kakor je to ta dan.‹« Potem sem odgovoril in rekel: »Tako naj bo, oh Gospod.«
6 Bwana akaniambia, “Tangaza maneno haya yote katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu: ‘Sikilizeni maneno ya agano hili na kuyafuata.
Potem mi je Gospod rekel: »Razglasi vse te besede po Judovih mestih in ulicah Jeruzalema, rekoč: ›Poslušajte besede te zaveze in jih izpolnjujte.
7 Tangu wakati ule niliwapandisha baba zenu kutoka Misri mpaka leo, niliwaonya tena na tena, nikisema “Nitiini mimi.”
Kajti iskreno sem izpričal vašim očetom na dan, ko sem jih privedel gor iz egiptovske dežele, celó do današnjega dne, [jih] zgodaj vzdigoval in izjavljal, rekoč: ›Ubogajte moj glas.‹
8 Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Hivyo nikaleta juu yao laana zote za agano nililokuwa nimewaamuru wao kulifuata, lakini wao hawakulishika.’”
Vendar niso ubogali niti nagnili svojega ušesa, temveč so vsi hodili v zamisli svojega zlega srca. Zato bom nanje privedel vse besede te zaveze, ki sem jim jo zapovedal izpolnjevati, toda oni jih niso izpolnjevali.
9 Kisha Bwana akaniambia, “Kuna shauri baya linaloendelea miongoni mwa watu wa Yuda na wale wanaoishi Yerusalemu.
Gospod mi je rekel: »Zarota je najdena med Judovimi možmi in med prebivalci Jeruzalema.
10 Wamerudia dhambi za baba zao, waliokataa kusikiliza maneno yangu. Wameifuata miungu mingine kuitumikia. Nyumba zote mbili za Israeli na Yuda zimelivunja agano nililofanya na baba zao.
Obrnili so se nazaj h krivičnostim svojih pradedov, ki so odklanjali poslušati moje besede; in šli za drugimi bogovi, da jim služijo. Izraelova hiša in Judova hiša sta prelomili mojo zavezo, ki sem jo sklenil z njihovimi očeti.
11 Kwa hivyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitaleta juu yao maafa ambayo hawawezi kuyakimbia. Hata kama wakinililia, sitawasikiliza.
Zato tako govori Gospod: ›Glej, nanje bom privedel zlo, ki mu ne bodo mogli pobegniti. Čeprav bodo klicali k meni, jim ne bom prisluhnil.
12 Miji ya Yuda na watu wa Yerusalemu watakwenda kuililia miungu ambayo wameifukizia uvumba, lakini haitawasaidia kamwe wakati maafa yatakapowapiga.
Potem bodo Judova mesta in prebivalci Jeruzalema šli in klicali k bogovom, katerim darujejo kadilo. Toda sploh jih ne bodo rešili v času njihove stiske.
13 Mnayo miungu mingi kama miji mliyo nayo, ee Yuda, nazo madhabahu mlizozijenga za kufukizia uvumba huyo mungu wa aibu Baali ni nyingi kama barabara za Yerusalemu.’
Kajti glede na število tvojih mest so bili tvoji bogovi, oh Juda; in glede na število ulic [prestolnice] Jeruzalem ste postavili oltarje tisti sramotni stvari, celó oltarje, da zažigate kadilo Báalu.
14 “Wewe usiwaombee watu hawa wala kufanya maombezi yoyote au kunisihi kwa ajili yao, kwa sababu sitawasikiliza watakaponiita wakati wa taabu yao.
Zatorej ne moli za to ljudstvo niti ne povzdiguj vpitja ali molitve zanje, kajti jaz jih ne bom poslušal ob času, ko zaradi svoje stiske vpijejo k meni.
15 “Mpenzi wangu anafanya nini hekaluni mwangu, anapofanya mashauri yake maovu na wengi? Je, nyama iliyowekwa wakfu yaweza kuondolea mbali adhabu yako? Unapojiingiza katika ubaya wako, ndipo unashangilia.”
Kaj ima moj ljubljeni za početi v moji hiši, ko vidi, da je ona izvrševala nespodobnost s številnimi in je sveto meso odšlo od tebe? Ko počneš zlo, potem se razveseljuješ.
16 Bwana alikuita mti wa mzeituni uliostawi ulio na matunda mazuri kwa sura. Lakini kwa ngurumo ya mawimbi makuu atautia moto, nayo matawi yake yatavunjika.
Gospod je tvoje ime imenoval: ›Zelena oljka, čeden in lep sad.‹ Z zvokom velikega hrupa je na njej vžgal ogenj in njene mladike so polomljene.
17 Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliyekupanda, ametamka maafa kwa ajili yako, kwa sababu nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda mmefanya maovu na kunikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba.
Kajti Gospod nad bojevniki, ki te je zasadil, je zoper tebe proglasil zlo, zaradi zla Izraelove hiše in Judove hiše, ki so ga storili zoper sebe, da bi me dražili do jeze v darovanju kadila Báalu.
18 Kwa sababu Bwana alinifunulia hila zao mbaya, nilizifahamu, kwa kuwa wakati ule alinionyesha yale waliyokuwa wanayafanya.
Gospod mi je dal spoznanje o tem in jaz sem to spoznal; takrat si mi kazal njihova dejanja.
19 Nilikuwa kama mwana-kondoo mpole aliyeongozwa machinjoni; mimi sikutambua kwamba walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yangu, wakisema, “Sisi na tuuangamize mti na matunda yake; nasi tumkatilie mbali kutoka nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena.”
Toda jaz sem bil podoben jagnjetu ali volu, ki je priveden h klanju in nisem vedel, da so zoper mene snovali naklepe, rekoč: »Uničimo drevo skupaj z njegovim sadom in odsekajmo ga iz dežele živih, da se njegovega imena ne bo več spominjalo.«
20 Lakini, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, wewe uhukumuye kwa haki, nawe uchunguzaye moyo na akili, wacha nione ukiwalipiza wao kisasi, kwa maana kwako nimeweka shauri langu.
Toda, oh Gospod nad bojevniki, ki sodiš pravično, ki preizkušaš notranjost in srce, naj vidim tvoje maščevanje na njih, kajti tebi sem razodel svoj primer.
21 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu wa Anathothi wale wanaotafuta uhai wako wakisema, ‘Usitoe unabii kwa jina la Bwana, la sivyo utakufa kwa mikono yetu’:
»Zato tako govori Gospod o možeh iz Anatóta, ki ti strežejo po življenju, rekoč: ›Ne prerokuj v Gospodovem imenu, da ne umreš po naši roki.‹
22 kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu. Vijana wao waume watakufa kwa upanga, wana wao na binti zao kwa njaa.
Zato tako govori Gospod nad bojevniki: ›Glej, kaznoval jih bom; mladenič bo umrl pod mečem, njihovi sinovi in njihove hčere bodo umrli od lakote.
23 Hawatasaziwa hata mabaki kwao, kwa sababu nitaleta maafa kwa watu wa Anathothi katika mwaka wa adhabu yao.’”
Tam ne bo nobenega ostanka izmed njih, kajti nad ljudi iz Anatóta bom privedel zlo, celó leto njihovega obiskanja.‹«