< Yeremia 11 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
La parole qui fut adressée à Jérémie, de la part de l'Éternel, en ces mots:
2 “Sikia maneno ya agano hili, nawe uwaambie watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu.
Écoutez les paroles de cette alliance, et parlez aux hommes de Juda et aux habitants de Jérusalem.
3 Waambie kwamba hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Amelaaniwa mtu ambaye hatayatii maneno ya agano hili,
Tu leur diras: Ainsi a dit l'Éternel, le Dieu d'Israël: Maudit est l'homme qui n'écoute pas les paroles de cette alliance,
4 maneno niliyowaamuru baba zenu nilipowatoa katika nchi ya Misri, kutoka tanuru la kuyeyushia vyuma.’ Nilisema, ‘Nitiini mimi na mfanye kila kitu ninachowaamuru, nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.
Que j'ai prescrite à vos pères le jour où je les ai retirés du pays d'Égypte, de la fournaise de fer, en disant: Écoutez ma voix, et faites toutes les choses que je vous commande, et vous serez mon peuple et je serai votre Dieu;
5 Kisha nitatimiza kiapo nilichowaapia baba zenu, kuwapa nchi itiririkayo maziwa na asali,’ nchi ambayo mnaimiliki leo.” Nikajibu, “Amen, Bwana.”
J'accomplirai le serment que j'ai fait à vos pères, de leur donner un pays où coulent le lait et le miel, comme vous le voyez aujourd'hui. Et je répondis et dis: Amen! ô Éternel!
6 Bwana akaniambia, “Tangaza maneno haya yote katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu: ‘Sikilizeni maneno ya agano hili na kuyafuata.
Et l'Éternel me dit: Crie toutes ces paroles par les villes de Juda et par les rues de Jérusalem, en disant: Écoutez les paroles de cette alliance, et observez-les.
7 Tangu wakati ule niliwapandisha baba zenu kutoka Misri mpaka leo, niliwaonya tena na tena, nikisema “Nitiini mimi.”
Car j'ai sommé vos pères, depuis le jour où je les fis monter du pays d'Égypte jusqu'à ce jour, je les ai sommés dès le matin, disant: Écoutez ma voix!
8 Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Hivyo nikaleta juu yao laana zote za agano nililokuwa nimewaamuru wao kulifuata, lakini wao hawakulishika.’”
Mais ils n'ont pas écouté; ils n'ont pas prêté l'oreille; ils ont marché chacun selon la dureté de son cœur. Et j'ai fait venir sur eux toutes les paroles de cette alliance, que je leur avais commandé de garder et qu'ils n'ont point gardée.
9 Kisha Bwana akaniambia, “Kuna shauri baya linaloendelea miongoni mwa watu wa Yuda na wale wanaoishi Yerusalemu.
Et l'Éternel me dit: Il y a une conjuration entre les hommes de Juda et entre les habitants de Jérusalem.
10 Wamerudia dhambi za baba zao, waliokataa kusikiliza maneno yangu. Wameifuata miungu mingine kuitumikia. Nyumba zote mbili za Israeli na Yuda zimelivunja agano nililofanya na baba zao.
Ils sont retournés aux iniquités de leurs ancêtres qui ont refusé d'écouter mes paroles, et ils sont allés après d'autres dieux pour les servir. La maison d'Israël et la maison de Juda ont violé mon alliance, que j'ai traitée avec leurs pères.
11 Kwa hivyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitaleta juu yao maafa ambayo hawawezi kuyakimbia. Hata kama wakinililia, sitawasikiliza.
C'est pourquoi, ainsi a dit l'Éternel: Voici, je vais faire venir sur eux un mal duquel ils ne pourront sortir; ils crieront vers moi, mais je ne les écouterai point.
12 Miji ya Yuda na watu wa Yerusalemu watakwenda kuililia miungu ambayo wameifukizia uvumba, lakini haitawasaidia kamwe wakati maafa yatakapowapiga.
Et les villes de Juda et les habitants de Jérusalem s'en iront crier vers les dieux auxquels ils offrent leurs parfums; mais ils ne les sauveront point au temps de leur malheur.
13 Mnayo miungu mingi kama miji mliyo nayo, ee Yuda, nazo madhabahu mlizozijenga za kufukizia uvumba huyo mungu wa aibu Baali ni nyingi kama barabara za Yerusalemu.’
Car, ô Juda! tu as autant de dieux que de villes, et, autant il y a de rues à Jérusalem, autant vous avez dressé d'autels à l'infamie, des autels pour offrir des parfums à Baal.
14 “Wewe usiwaombee watu hawa wala kufanya maombezi yoyote au kunisihi kwa ajili yao, kwa sababu sitawasikiliza watakaponiita wakati wa taabu yao.
Et toi, n'intercède pas pour ce peuple, n'élève pour eux ni cri ni prière; car je ne les écouterai pas, lorsqu'ils crieront vers moi à cause de leur malheur.
15 “Mpenzi wangu anafanya nini hekaluni mwangu, anapofanya mashauri yake maovu na wengi? Je, nyama iliyowekwa wakfu yaweza kuondolea mbali adhabu yako? Unapojiingiza katika ubaya wako, ndipo unashangilia.”
Que viendrait faire mon bien-aimé dans ma maison? Cette foule n'y est que pour commettre la fraude! Mais on ôtera de devant toi la chair sacrée. Quand tu fais le mal, c'est alors que tu t'élèves!
16 Bwana alikuita mti wa mzeituni uliostawi ulio na matunda mazuri kwa sura. Lakini kwa ngurumo ya mawimbi makuu atautia moto, nayo matawi yake yatavunjika.
Olivier verdoyant, excellent par la beauté de son fruit, ainsi l'appelait l'Éternel. Au bruit d'un grand fracas il y allume le feu, et ses rameaux sont brisés!
17 Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliyekupanda, ametamka maafa kwa ajili yako, kwa sababu nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda mmefanya maovu na kunikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba.
Et l'Éternel des armées, qui t'a planté, a prononcé le mal contre toi, à cause du mal que se sont fait à elles-mêmes la maison d'Israël et la maison de Juda, en m'irritant par leurs encensements à Baal.
18 Kwa sababu Bwana alinifunulia hila zao mbaya, nilizifahamu, kwa kuwa wakati ule alinionyesha yale waliyokuwa wanayafanya.
L'Éternel me l'a fait connaître, et je l'ai connu; alors tu m'as fait voir leurs œuvres.
19 Nilikuwa kama mwana-kondoo mpole aliyeongozwa machinjoni; mimi sikutambua kwamba walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yangu, wakisema, “Sisi na tuuangamize mti na matunda yake; nasi tumkatilie mbali kutoka nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena.”
Et moi, comme un agneau familier, qu'on mène pour être égorgé, je ne savais pas les mauvais desseins qu'ils méditaient contre moi: “Détruisons l'arbre avec son fruit, et l'exterminons de la terre des vivants, et qu'il ne soit plus fait mention de son nom! “
20 Lakini, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, wewe uhukumuye kwa haki, nawe uchunguzaye moyo na akili, wacha nione ukiwalipiza wao kisasi, kwa maana kwako nimeweka shauri langu.
Mais l'Éternel des armées est un juste juge, qui sonde les reins et les cœurs. Tu me feras voir la vengeance que tu tireras d'eux; car je t'ai découvert ma cause.
21 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu wa Anathothi wale wanaotafuta uhai wako wakisema, ‘Usitoe unabii kwa jina la Bwana, la sivyo utakufa kwa mikono yetu’:
C'est pourquoi, ainsi a dit l'Éternel contre les gens d'Anathoth, qui cherchent ta vie et qui disent: Ne prophétise pas au nom de l'Éternel, et tu ne mourras pas de notre main;
22 kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu. Vijana wao waume watakufa kwa upanga, wana wao na binti zao kwa njaa.
C'est pourquoi, ainsi dit l'Éternel des armées: Voici, je vais les punir; les jeunes hommes mourront par l'épée; leurs fils et leurs filles mourront par la famine.
23 Hawatasaziwa hata mabaki kwao, kwa sababu nitaleta maafa kwa watu wa Anathothi katika mwaka wa adhabu yao.’”
Et il ne restera rien d'eux; car je ferai venir le mal sur les gens d'Anathoth, l'année de leur visitation.

< Yeremia 11 >