< Yeremia 1 >
1 Maneno ya Yeremia mwana wa Hilkia, mmoja wa makuhani katika mji wa Anathothi, katika nchi ya Benyamini.
word Jeremiah son: child Hilkiah from [the] priest which in/on/with Anathoth in/on/with land: country/planet Benjamin
2 Neno la Bwana lilimjia katika mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda,
which to be word LORD to(wards) him in/on/with day Josiah son: child Amon king Judah in/on/with three ten year to/for to reign him
3 na pia wakati wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, mpaka mwezi wa tano wa mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Sedekia mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati watu wa Yerusalemu walipopelekwa uhamishoni.
and to be in/on/with day Jehoiakim son: child Josiah king Judah till to finish eleven ten year to/for Zedekiah son: child Josiah king Judah till to reveal: remove Jerusalem in/on/with month [the] fifth
4 Neno la Bwana lilinijia, kusema,
and to be word LORD to(wards) me to/for to say
5 “Kabla sijakuumba ndani ya tumbo la mama yako, nilikujua; kabla hujazaliwa nilikutenga kwa kazi maalum; nilikuweka uwe nabii kwa mataifa.”
in/on/with before (to form: formed you *Q(k)*) in/on/with belly: womb to know you and in/on/with before to come out: produce from womb to consecrate: dedicate you prophet to/for nation to give: put you
6 Nami nikasema, “Aa, Bwana Mwenyezi, sijui kusema, kwani mimi ni mtoto mdogo tu.”
and to say alas! Lord YHWH/God behold not to know to speak: speak for youth I
7 Lakini Bwana akaniambia, “Usiseme, ‘Mimi ni mtoto mdogo tu.’ Utaenda popote nitakapokutuma na kunena lolote nitakalokuagiza.
and to say LORD to(wards) me not to say youth I for upon all which to send: depart you to go: went and [obj] all which to command you to speak: speak
8 Usiwaogope, kwa maana niko pamoja nawe nikuokoe,” asema Bwana.
not to fear from face of their for with you I to/for to rescue you utterance LORD
9 Kisha Bwana akaunyoosha mkono wake na kugusa kinywa changu, akaniambia, “Sasa nimeyaweka maneno yangu kinywani mwako.
and to send: reach LORD [obj] hand his and to touch upon lip my and to say LORD to(wards) me behold to give: put word my in/on/with lip your
10 Tazama, leo nimekuweka juu ya mataifa na falme ili kungʼoa na kubomoa, kuharibu na kuangamiza, kujenga na kupanda.”
to see: behold! to reckon: overseer you [the] day: today [the] this upon [the] nation and upon [the] kingdom to/for to uproot and to/for to tear and to/for to perish and to/for to overthrow to/for to build and to/for to plant
11 Neno la Bwana likanijia kusema, “Je, Yeremia unaona nini?” Nami nikajibu, “Naona tawi la mti wa mlozi.”
and to be word LORD to(wards) me to/for to say what? you(m. s.) to see: see Jeremiah and to say rod almond I to see: see
12 Bwana akaniambia, “Umeona vyema kwa maana ninaliangalia neno langu ili kuona kwamba limetimizwa.”
and to say LORD to(wards) me be good to/for to see: see for to watch I upon word my to/for to make: do him
13 Neno la Bwana likanijia tena, “Unaona nini?” Nikajibu, “Naona chungu kinachochemka, kikiwa kimeinama kutoka kaskazini.”
and to be word LORD to(wards) me second to/for to say what? you(m. s.) to see: see and to say pot to breathe I to see: see and face: before his from face: before north [to]
14 Bwana akaniambia, “Kutoka kaskazini maafa yatamwagwa kwa wote waishio katika nchi.
and to say LORD to(wards) me from north to open [the] distress: harm upon all to dwell [the] land: country/planet
15 Nitawaita watu wote wa falme za kaskazini,” asema Bwana. “Wafalme wao watakuja na kuweka viti vyao vya enzi katika maingilio ya malango ya Yerusalemu, watakuja dhidi ya kuta zake zote zinazouzunguka, na dhidi ya miji yote ya Yuda.
for look! I to call: call to to/for all family kingdom north [to] utterance LORD and to come (in): come and to give: put man: anyone throne his entrance gate Jerusalem and upon all wall her around and upon all city Judah
16 Nitatoa hukumu zangu kwa watu wangu kwa sababu ya uovu wao wa kuniacha mimi, kwa kufukiza uvumba kwa miungu mingine na kuabudu kile ambacho mikono yao imekitengeneza.
and to speak: promise justice: judgement my with them upon all distress: evil their which to leave: forsake me and to offer: offer to/for God another and to bow to/for deed: work hand their
17 “Jiandae! Simama useme chochote nitakachokuamuru. Usiwaogope, la sivyo nitakufanya uwaogope wao.
and you(m. s.) to gird loin your and to arise: rise and to speak: speak to(wards) them [obj] all which I to command you not to to be dismayed from face: before their lest to to be dismayed you to/for face: before their
18 Leo nimekufanya mji wenye ngome, nguzo ya chuma, na ukuta wa shaba ili kusimama dhidi ya nchi yote: dhidi ya wafalme wa Yuda, maafisa wake, makuhani wake na watu wa nchi hiyo.
and I behold to give: make you [the] day: today to/for city fortification and to/for pillar iron and to/for wall bronze upon all [the] land: country/planet to/for king Judah to/for ruler her to/for priest her and to/for people [the] land: country/planet
19 Watapigana nawe lakini hawatakushinda, kwa kuwa niko pamoja nawe, nami nitakuokoa,” asema Bwana.
and to fight to(wards) you and not be able to/for you for with you I utterance LORD to/for to rescue you