< Yeremia 1 >

1 Maneno ya Yeremia mwana wa Hilkia, mmoja wa makuhani katika mji wa Anathothi, katika nchi ya Benyamini.
本雅明地內阿納托特城的司祭中,希耳克雅的兒子耶肋米亞的言行錄。──
2 Neno la Bwana lilimjia katika mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda,
上主的話傳給,是在阿孟的兒子約史雅為猶大王執政第十三年;
3 na pia wakati wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, mpaka mwezi wa tano wa mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Sedekia mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati watu wa Yerusalemu walipopelekwa uhamishoni.
以後傳給他,是在約史雅的兒子約雅金為猶大王,直到約史雅的兒子漆德雅為猶大王第十一年年底,即直到是年五月,耶路撒冷固民被擄去充軍時為止。
4 Neno la Bwana lilinijia, kusema,
上主對我說:
5 “Kabla sijakuumba ndani ya tumbo la mama yako, nilikujua; kabla hujazaliwa nilikutenga kwa kazi maalum; nilikuweka uwe nabii kwa mataifa.”
「我還沒有在母腹形成你以前,我已認識了你;在你還沒有出離母胎以前,我已祝福了你,選定了你作萬民的先知。」
6 Nami nikasema, “Aa, Bwana Mwenyezi, sijui kusema, kwani mimi ni mtoto mdogo tu.”
我回答說:「哎呀! 我主上主! 你看,我還太年輕,不會說話」。
7 Lakini Bwana akaniambia, “Usiseme, ‘Mimi ni mtoto mdogo tu.’ Utaenda popote nitakapokutuma na kunena lolote nitakalokuagiza.
上主對我說:「你別說:我太年輕,因為我派你到那裏去,你就應到那裏去;我命你說什麼,你就應說什麼。
8 Usiwaogope, kwa maana niko pamoja nawe nikuokoe,” asema Bwana.
你不要害怕他們,因為有我與你同在,保護你──上主的斷語。」
9 Kisha Bwana akaunyoosha mkono wake na kugusa kinywa changu, akaniambia, “Sasa nimeyaweka maneno yangu kinywani mwako.
此後,上主伸出手來,觸摸我的口,對我說:「看,我將我的話放在你口中;
10 Tazama, leo nimekuweka juu ya mataifa na falme ili kungʼoa na kubomoa, kuharibu na kuangamiza, kujenga na kupanda.”
看我今天委派你對萬民和邦列國,執行拔除、破壞、毀滅、推翻、建設和栽培的任務。」
11 Neno la Bwana likanijia kusema, “Je, Yeremia unaona nini?” Nami nikajibu, “Naona tawi la mti wa mlozi.”
上主的話傳給我說:「耶肋米亞,你看見什麼﹖」我回答說:「我看見一棵杏樹枝。」
12 Bwana akaniambia, “Umeona vyema kwa maana ninaliangalia neno langu ili kuona kwamba limetimizwa.”
上主對我說:「你看的對,因為我要警醒,看我的話怎樣實現。」
13 Neno la Bwana likanijia tena, “Unaona nini?” Nikajibu, “Naona chungu kinachochemka, kikiwa kimeinama kutoka kaskazini.”
上主的話二次傳給我說:「你看見什麼﹖」我回答說:「我看見一個沸騰的鍋,它的口由北面傾倒過來。」
14 Bwana akaniambia, “Kutoka kaskazini maafa yatamwagwa kwa wote waishio katika nchi.
上主對我說:「災禍將由北方燒起,一直燒到這地上的一切居民。
15 Nitawaita watu wote wa falme za kaskazini,” asema Bwana. “Wafalme wao watakuja na kuweka viti vyao vya enzi katika maingilio ya malango ya Yerusalemu, watakuja dhidi ya kuta zake zote zinazouzunguka, na dhidi ya miji yote ya Yuda.
看,我必召集北方的一切國家──上主的斷語──叫各國前來,在城門口,在城牆四周以及猶大各城市旁,建立自己的寶座。
16 Nitatoa hukumu zangu kwa watu wangu kwa sababu ya uovu wao wa kuniacha mimi, kwa kufukiza uvumba kwa miungu mingine na kuabudu kile ambacho mikono yao imekitengeneza.
我要向各城市的人民宣告我的判決,懲罰他們的,因為他們離棄我,向別的神祗獻香,崇拜了他們手製的作品。
17 “Jiandae! Simama useme chochote nitakachokuamuru. Usiwaogope, la sivyo nitakufanya uwaogope wao.
至於你,你要束上腰,起來向他們傳示我命令你的一切。在他們面前,你不要畏懼,免得我在他們面前令你畏懼。
18 Leo nimekufanya mji wenye ngome, nguzo ya chuma, na ukuta wa shaba ili kusimama dhidi ya nchi yote: dhidi ya wafalme wa Yuda, maafisa wake, makuhani wake na watu wa nchi hiyo.
看啊! 我今天使你成為堅城、銅牆、鐵壁,以對抗猶大君王和首領,司祭和當地的人民。
19 Watapigana nawe lakini hawatakushinda, kwa kuwa niko pamoja nawe, nami nitakuokoa,” asema Bwana.
他們要攻擊你,卻不能得勝你,因為有我與你同在,協助你──上主的斷語。」

< Yeremia 1 >