< Yakobo 1 >
1 Yakobo, mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo: Kwa makabila kumi na mawili yaliyotawanyika ulimwenguni: Salamu.
Yakobo n'tumwa ghwa K'yara ni ghwa Bwana Yesu Kristu kwa makabila kumi ni mabhele ghaghatabhwanyiki, salaam.
2 Ndugu zangu, hesabuni kuwa ni furaha tupu mnapopatwa na majaribu mbalimbali,
Mubhalangayi kujha ni furaha nesu bhalongo bhangu, pamwip'eta mu malombosi agha ni agha,
3 kwa sababu mnajua ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.
mkamanyayi kujha kujaribibhwa kwa imani jha muenga jhikabhapela bhuvumilivu.
4 Saburi na iwe na kazi timilifu, ili mpate kuwa wakamilifu, mmekamilishwa, bila kupungukiwa na kitu chochote.
Mubhulekayi bhuvumilivu ujhikamilisiajhi mbombo jha muene, kwamba mubhwesiajhi kukomala kinofu, bila kup'ongh'okibhwa mu lyolyoha.
5 Kama mtu yeyote miongoni mwenu amepungukiwa na hekima na amwombe Mungu, yeye awapaye watu wote kwa ukarimu wala hana kinyongo, naye atapewa.
Lakini kama munu kati jha muenga ilonda hekima ajhisokayi kuhoma kwa K'yara ambajhe ipisya kwa bhunofu ni bila kujhwangila kwa bhanu bhabhakan'soka, ni kubhap, ela hekima.
6 Lakini anapoomba, lazima aamini wala asiwe na shaka, kwa sababu mtu aliye na shaka ni kama wimbi la bahari, lililochukuliwa na upepo na kutupwa huku na huku.
Lakini sokayi kwa imani bila bhuogha kwa kujha jhaajhe ni kubheka shaka ndo kama manyegha mu bahari ghitolibhwa ni mp'ongo khoni ni okhu.
7 Mtu kama huyo asidhani ya kuwa atapata kitu chochote kutoka kwa Bwana.
Kwa hakika munu ojhu asifikiriri kwamba ibetakujhop'elibhwa liombi lya muene kuhoma kwa Bwana;
8 Yeye ni mtu mwenye nia mbili, mwenye kusitasita katika njia zake zote.
munu ojho ajhe ni nia sibhele: imaralepi mu njela sya muene syoha.
9 Ndugu asiye na cheo kikubwa yampasa ajivunie hali hiyo maana ametukuzwa.
Bhalongo bhangu bhab'onji bhitondeka kwifuna mu kujhema kwa muene kunani,
10 Lakini yeye aliye tajiri afurahi kwa kuwa ameshushwa, kwa sababu atatoweka kama ua la shambani.
Bhwakati bhobhuobhu ndongo tajiri mu bhunyenyekefu bhwa muene kwa ndabha ibetakubhoka kama liua lya kondeni mu n'gonda lya ip'eta.
11 Kwa maana jua kali lenye kuchoma huchomoza na kuliunguza, likayakausha majani, na ua lake likapukutika, nao uzuri wake huharibika. Vivyo hivyo tajiri naye atanyauka akiwa anaendelea na shughuli zake.
Lijobha lihoma ni joto lya kulalisya kujhomesya mimea, ni maua ghijhoma ghibina ni unofu bhuake bhwifwa. Fefuefu bhanu matajiri bhibetakuchakala pagati mu mbombo sya bhene.
12 Heri mtu anayevumilia wakati wa majaribu, kwa sababu akiisha kushinda hilo jaribio atapewa taji la uzima Mungu alilowaahidia wale wampendao.
Abarikibhu munujhola jhaisindamala majaribu, kwa kujha baada jha kushinda lijaribu e'lu, ibetakujhamb'elela litaji lya uzima, ambajho jhiahidibhu kwa bhala bhabhan'ganili K'yara.
13 Mtu anapojaribiwa asiseme, “Ninajaribiwa na Mungu.” Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu wala yeye hamjaribu mtu yeyote.
Munu jhajhioha ilondekalepi, kujobha paijaribibhwa, “Lijaribu e'le lihomela kwa K'yara.” Kwandabha K'yara ijaribibibhwa lepi ni uovu, ni K'yara muene akan'jaribu jhejhioha.
14 Lakini kila mtu hujaribiwa wakati anapovutwa na kudanganywa na tamaa zake mwenyewe zilizo mbaya.
Khila munu ijaribibhwa ni tamaa sya muene sibhibhi syasikan'shawishi ni kumfuta patali.
15 Basi ile tamaa mbaya ikishachukua mimba, huzaa dhambi, nayo ile dhambi ikikomaa, huzaa mauti.
Ndiponbaada jha tamaa jha dhambi kup'etenda luleme dhambi jhihogoleka, ni baada jha dhambi kukomala kinofu, jhimalikila mu mauti.
16 Ndugu zangu wapendwa, msidanganyike.
Bhalango bhangu bhapendwa, msikofibhu.
17 Kila kitolewacho kilicho chema na kilicho kamili, hutoka juu, na hushuka kutoka kwa Baba wa mianga, ambaye kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeukageuka.
Khilanzawadi jhajhele jhinofu ni khila zawadi jhajhikamilifu jhihomela kunani, jhiselela pasi kuhoma kwa Dadi ghwa nuru. Kabhele ibadilikalepi kama kivuli kyakibadilika.
18 Kwa mapenzi yake mwenyewe alituzaa kwa neno la kweli, kusudi tuwe kama mazao ya kwanza katika viumbe vyake vyote.
K'yara atusalili kutusalili kutupela tete uzima kwa lilobhi lya bhukueli, ili kwamba tubhwesiajhi kujha kama uzao bhwa kuanza miongoni mwa fiumbe fya muene.
19 Ndugu zangu wapendwa, fahamuni jambo hili: Kila mtu awe mwepesi wa kusikiliza, lakini asiwe mwepesi wa kusema wala wa kukasirika.
Mumanyili e'le bhalongo bhangu bhaganwa, khila mmonga ilondeka kujha njojhofu ghwa kup'eteka na sio njojhofu ghwa kulongela bhwala kudada,
20 Kwa maana hasira ya mwanadamu haitendi haki ya Mungu.
kwa kujha ligoga lya mwanadamu libhwesyalepi kubhomba mbombo jha K'yara.
21 Kwa hiyo, ondoleeni mbali uchafu wote na uovu ambao umezidi kuwa mwingi, mkalipokee kwa unyenyekevu lile Neno lililopandwa ndani yenu ambalo laweza kuokoa nafsi zenu.
Henu mubhekayi patali uchafu bhwa dhambi ni bhubhibhi bhuoha bhwabhujhele mahali poha, ni kwa bhunyenyekevu mulijhambolelayi lilobhi lyalipandibhu mugati mwa muenga, ambalyo lijhele ni bhuwesu bhwa kuokola roho sya muenga.
22 Basi kuweni watendaji wa Neno wala msiwe wasikiaji tu, huku mkijidanganya nafsi zenu.
Mulitiajhi lilobhi, msilipeleki tu mwikikifya nafsi sya jhomu mwibhene.
23 Kwa maana kama mtu ni msikiaji tu wa Neno wala hatendi kile linachosema, yeye ni kama mtu ajitazamaye uso wake kwenye kioo
Kwa kujha kama jhehioha jhaakalipeleka lilobhi bila kulibhonibela mbombo ndo sabhwa ni munu jhaikilola pamihu pa muene halisi mu kiibho.
24 na baada ya kujiona alivyo, huenda zake na mara husahau jinsi alivyo.
Ikitathimini pamihu pa muene, na ikwilotela ni baada jha muda udebe ijhebhelela kyaiwaningana.
25 Lakini yeye anayeangalia kwa bidii katika sheria kamilifu, ile iletayo uhuru, naye akaendelea kufanya hivyo bila kusahau alichosikia, bali akalitenda, atabarikiwa katika kile anachofanya.
Bali munu jhola jha ikilanga kwa uangalifu bhwa sheria kamili sheria jha uhuru, ni kujhendelela kujhitii sio kwandabha muene mp'elekesiaji jhaiheb helela, munu ojho ibeta kubarikibhwa paibhomba.
26 Kama mtu akidhani ya kuwa anayo dini lakini hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hujidanganya moyoni mwake, wala dini yake mtu huyo haifai kitu.
Ikajhelayi munu jhejhioha ibetakufikirila muene kujha ndo munu ghwa dini, lazima ibhwesyalepi kubhutabhwala lumilu lwa muene, akabhukofya muoyo bhwa muene ni dini jha muene ndo Pat'op'o.
27 Dini iliyo safi, isiyo na uchafu, inayokubalika mbele za Mungu Baba yetu, ndiyo hii: Kuwasaidia yatima na wajane katika dhiki zao na kujilinda usitiwe madoa na dunia.
Dini jhinofu na jhajhibeli kuharibibhwa palongolo pa K'yara ghwitu ni Dadi ndo ejhe: kubhatangatila bhakhebha ni bhajane mu malombosi gha bhene, ni kwilenda bhene ni bhufisadi bhwa dunia.