< Yakobo 4 >
1 Ni kitu gani kinachosababisha mapigano na ugomvi miongoni mwenu? Je, haya hayatokani na tamaa zenu zinazoshindana ndani yenu?
From whence [come] wars and fightings among you? [come they] not hence, [even] from your lusts that war in your members?
2 Mnatamani lakini hampati, kwa hiyo mwaua. Mwatamani kupata lakini hampati vile mnavyotaka, kwa hiyo mnajitia katika magomvi na mapigano. Mmepungukiwa kwa sababu hammwombi Mungu.
Ye lust and have not: ye kill, and desire to have, and cannot obtain: ye fight and war, yet ye have not, because ye ask not.
3 Mnapoomba hampati kwa sababu mnaomba kwa nia mbaya, ili mpate kuvitumia hivyo mtakavyopata kwa tamaa zenu.
Ye ask, and receive not, because ye ask amiss, that ye may consume [it] upon your lusts.
4 Ninyi wanaume na wanawake wazinzi, hamjui ya kwamba urafiki na dunia ni uadui na Mungu? Kwa hiyo mtu yeyote anayetaka kuwa rafiki wa dunia hufanyika adui wa Mungu.
Ye adulterers and adulteresses, know ye not that the friendship of the world is enmity with God? whoever therefore will be a friend of the world is the enemy of God.
5 Au mwadhani kwamba Andiko lasema bure kuwa huyo Roho ambaye Mungu amemweka ndani yetu hututamani kiasi cha kuona wivu?
Do ye think that the scripture saith in vain, The spirit that dwelleth in us lusteth to envy?
6 Lakini yeye hutupatia neema zaidi. Hii ndiyo sababu Andiko husema: “Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.”
But he giveth more grace. Wherefore he saith, God resisteth the proud, but giveth grace to the humble.
7 Basi mtiini Mungu. Mpingeni ibilisi, naye atawakimbia.
Submit yourselves therefore to God. Resist the devil, and he will flee from you.
8 Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu ninyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu ninyi wenye nia mbili.
Draw nigh to God, and he will draw nigh to you. Cleanse [your] hands, [ye] sinners, and purify [your] hearts, [ye] double-minded.
9 Huzunikeni, ombolezeni na kulia. Kicheko chenu na kigeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa huzuni.
Be afflicted, and mourn, and weep: let your laughter be turned to mourning, and [your] joy to heaviness.
10 Jinyenyekezeni mbele za Bwana, naye atawainua.
Humble yourselves in the sight of the Lord, and he will lift you up.
11 Ndugu, msineneane mabaya ninyi kwa ninyi. Mtu yeyote anayesema mabaya dhidi ya ndugu yake au kumhukumu anasema dhidi ya sheria na kuihukumu. Unapoihukumu sheria, basi huishiki sheria bali umekuwa hakimu wa kuihukumu hiyo sheria.
Speak not evil one of another, brethren. He that speaketh evil of [his] brother, and judgeth his brother, speaketh evil of the law, and judgeth the law: but if thou judgest the law, thou art not a doer of the law, but a judge.
12 Yuko Mtoa sheria mmoja tu na yeye peke yake ndiye Hakimu, ndiye awezaye kuokoa au kuangamiza. Lakini wewe ni nani hata umhukumu jirani yako?
There is one lawgiver, who is able to save, and to destroy: who art thou that judgest another?
13 Basi sikilizeni ninyi msemao, “Leo au kesho tutakwenda katika mji huu ama ule tukae humo mwaka mmoja, tufanye biashara na kupata faida.”
Come now, ye that say, To-day or to-morrow we will go into such a city, and continue there a year, and buy, and sell, and get gain:
14 Lakini hamjui hata litakalotukia kesho. Maisha yenu ni nini? Ninyi ni ukungu ambao huonekana kwa kitambo kidogo kisha hutoweka.
Whereas ye know not what [will be] on the morrow: For what [is] your life? It is even a vapor, that appeareth for a little time, and then vanisheth away.
15 Badala yake, inawapasa kusema, “Kama Bwana akipenda, tutaishi na kufanya hili ama lile.”
Instead of that ye [ought] to say, If the Lord will, we shall live, and do this, or that.
16 Kama ilivyo sasa, mnajisifu na kujigamba. Kujisifu kwa namna hiyo ni uovu.
But now ye rejoice in your boastings: all such rejoicing is evil.
17 Basi mtu yeyote anayejua jema limpasalo kutenda, lakini asilitende, mtu huyo anatenda dhambi.
Therefore to him that knoweth to do good, and doeth [it] not, to him it is sin.