< Yakobo 4 >
1 Ni kitu gani kinachosababisha mapigano na ugomvi miongoni mwenu? Je, haya hayatokani na tamaa zenu zinazoshindana ndani yenu?
Whence wars and fightings among you? Do they not come hence, even from your lusts, which war in your members?
2 Mnatamani lakini hampati, kwa hiyo mwaua. Mwatamani kupata lakini hampati vile mnavyotaka, kwa hiyo mnajitia katika magomvi na mapigano. Mmepungukiwa kwa sababu hammwombi Mungu.
You strongly desire, and have not; you kill, and are zealous, and can not obtain. You fight and war, but have not, because you ask not.
3 Mnapoomba hampati kwa sababu mnaomba kwa nia mbaya, ili mpate kuvitumia hivyo mtakavyopata kwa tamaa zenu.
You ask, and do not receive, because you ask wickedly, that you may spend upon your lusts.
4 Ninyi wanaume na wanawake wazinzi, hamjui ya kwamba urafiki na dunia ni uadui na Mungu? Kwa hiyo mtu yeyote anayetaka kuwa rafiki wa dunia hufanyika adui wa Mungu.
Adulterers, and adulteresses, do you not know that the friendship of the world is enmity against God? Whosoever, therefore, will be a friend of the world, is counted an enemy of God.
5 Au mwadhani kwamba Andiko lasema bure kuwa huyo Roho ambaye Mungu amemweka ndani yetu hututamani kiasi cha kuona wivu?
Do you think that the scripture speaks in vain? And does the spirit, who dwells in us, strongly incline to envy?
6 Lakini yeye hutupatia neema zaidi. Hii ndiyo sababu Andiko husema: “Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.”
But he gives greater favor. For it says, "God resists the proud, but gives favor to the humble."
7 Basi mtiini Mungu. Mpingeni ibilisi, naye atawakimbia.
Therefore, be subject to God. Resist the devil, and he will flee from you.
8 Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu ninyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu ninyi wenye nia mbili.
Draw nigh to God, and he will draw nigh to you. Cleanse your hands, you sinners; and purify your hearts, you men of two minds.
9 Huzunikeni, ombolezeni na kulia. Kicheko chenu na kigeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa huzuni.
Be exceedingly afflicted, and mourn, and weep; and let your laughter be turned into mourning, and your joy into sadness.
10 Jinyenyekezeni mbele za Bwana, naye atawainua.
Be humble in the presence of the Lord, and he will lift you up.
11 Ndugu, msineneane mabaya ninyi kwa ninyi. Mtu yeyote anayesema mabaya dhidi ya ndugu yake au kumhukumu anasema dhidi ya sheria na kuihukumu. Unapoihukumu sheria, basi huishiki sheria bali umekuwa hakimu wa kuihukumu hiyo sheria.
He who speaks against his brother, and condemns his brother, speaks against the law, and condemns the law. But if you condemn the law, you are not a doer of the law, but a judge.
12 Yuko Mtoa sheria mmoja tu na yeye peke yake ndiye Hakimu, ndiye awezaye kuokoa au kuangamiza. Lakini wewe ni nani hata umhukumu jirani yako?
There is one lawgiver, who is able to save, and to destroy. Who are you, that condemn another?
13 Basi sikilizeni ninyi msemao, “Leo au kesho tutakwenda katika mji huu ama ule tukae humo mwaka mmoja, tufanye biashara na kupata faida.”
Come, now, you who say, To-day, or to-morrow, we will go to such a city, and will abide there one year, and traffic in merchandise, and get gain;
14 Lakini hamjui hata litakalotukia kesho. Maisha yenu ni nini? Ninyi ni ukungu ambao huonekana kwa kitambo kidogo kisha hutoweka.
who do not know what shall be to-morrow. For what is your life? It is, indeed, a smoke, which appears for a little while, and then vanishes away.
15 Badala yake, inawapasa kusema, “Kama Bwana akipenda, tutaishi na kufanya hili ama lile.”
Instead of which, you ought to say, If the Lord will, we shall live, and do this, or that.
16 Kama ilivyo sasa, mnajisifu na kujigamba. Kujisifu kwa namna hiyo ni uovu.
But now you boast in your proud speeches: all such boasting is evil.
17 Basi mtu yeyote anayejua jema limpasalo kutenda, lakini asilitende, mtu huyo anatenda dhambi.
Wherefore, to him who know how to do good, and does it not, to him it is sin.