< Yakobo 4 >

1 Ni kitu gani kinachosababisha mapigano na ugomvi miongoni mwenu? Je, haya hayatokani na tamaa zenu zinazoshindana ndani yenu?
ⲁ̅ϩⲛ̅ⲛⲉⲧⲛ̅ϩⲏⲇⲟⲛⲏ. ⲛⲁⲓ ⲉⲧⲥⲧⲣⲁⲧⲉⲩⲉ ϩⲛ̅ⲛⲉⲧⲛ̅ⲙⲉⲗⲟⲥ.
2 Mnatamani lakini hampati, kwa hiyo mwaua. Mwatamani kupata lakini hampati vile mnavyotaka, kwa hiyo mnajitia katika magomvi na mapigano. Mmepungukiwa kwa sababu hammwombi Mungu.
ⲃ̅ⲧⲉⲧⲛ̅ⲉⲡⲓⲑⲩⲙⲉⲓ ⲁⲩⲱ ⲙⲛ̅ⲧⲏⲧⲛ̅. ⲧⲉⲧⲛ̅ϩⲱⲧⲃ̅. ⲧⲉⲧⲛ̅ⲕⲱϩ. ⲙⲛ̅ϭⲟⲙ ⲙ̅ⲙⲱⲧⲛ̅ ⲙ̅ⲙⲁⲧⲉ. ⲧⲉⲧⲛ̅ⲙⲓϣⲉ ⲁⲩⲱ ⲧⲉⲧⲛ̅ⲣ̅ⲡⲟⲗⲉⲙⲟⲥ. ⲙⲛ̅ⲧⲛ̅ ⲙ̅ⲙⲁⲩ. ϫⲉ ⲛ̅ⲧⲉⲧⲛ̅ⲁⲓⲧⲉⲓ ⲁⲛ.
3 Mnapoomba hampati kwa sababu mnaomba kwa nia mbaya, ili mpate kuvitumia hivyo mtakavyopata kwa tamaa zenu.
ⲅ̅ⲧⲉⲧⲛ̅ⲁⲓⲧⲉⲓ ⲁⲩⲱ ⲛ̅ⲧⲉⲧⲛ̅ϫⲓ ⲁⲛ. ϫⲉ ⲧⲉⲧⲛ̅ⲁⲓⲧⲉⲓ ⲕⲁⲕⲱⲥ. ϫⲉⲕⲁⲥ ⲉⲧⲉⲧⲛⲛⲁϫⲟⲟⲩ ⲉⲃⲟⲗ ϩⲛ̅ϩⲏⲇⲟⲛⲏ.
4 Ninyi wanaume na wanawake wazinzi, hamjui ya kwamba urafiki na dunia ni uadui na Mungu? Kwa hiyo mtu yeyote anayetaka kuwa rafiki wa dunia hufanyika adui wa Mungu.
ⲇ̅ⲛ̅ⲛⲟⲉⲓⲕ ⲛ̅ⲧⲉⲧⲛⲥⲟⲟⲩⲛ̅ ⲁⲛ ϫⲉ ⲧⲙⲛ̅ⲧϣⲃⲏⲣ ⲙ̅ⲡⲕⲟⲥⲙⲟⲥ ⲟⲩⲙⲛ̅ⲧϫⲁϫⲉ ⲧⲉ ⲙ̅ⲡⲛⲟⲩⲧⲉ. ⲡⲉⲧⲛⲁⲟⲩⲱϣ ϭⲉ ⲉⲣ̅ϣⲃⲏⲣ ⲉⲡⲕⲟⲥⲙⲟⲥ ϥⲛ̅ⲁϣⲱⲡⲉ ⲛ̅ϫⲁϫⲉ ⲉⲡⲛⲟⲩⲧⲉ.
5 Au mwadhani kwamba Andiko lasema bure kuwa huyo Roho ambaye Mungu amemweka ndani yetu hututamani kiasi cha kuona wivu?
ⲉ̅ⲏ ⲉⲧⲉⲧⲛ̅ⲙⲉⲉⲩⲉ ϫⲉ ⲉⲡϫⲓⲛϫⲏ ⲉⲣⲉⲧⲉⲅⲣⲁⲫⲏ ϣⲁϫⲉ. ϩⲛ̅ⲟⲩⲫⲑⲟⲛⲟⲥ ⲉⲥⲟⲩⲉϣⲡⲉⲡⲛ̅ⲁ ⲛ̅ⲧⲁϥⲟⲩⲱϩ ⲉϩⲣⲁⲓ ⲛ̅ϩⲏⲧⲛ̅.
6 Lakini yeye hutupatia neema zaidi. Hii ndiyo sababu Andiko husema: “Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.”
ⲋ̅ⲥϯ ⲇⲉ ⲛ̅ⲟⲩⲛⲟϭ ⲛ̅ϩⲙⲟⲧ. ⲉⲧⲃⲉⲡⲁⲓ ⲥϫⲱ ⲙ̅ⲙⲟⲥ ϫⲉ ⲡⲛⲟⲩⲧⲉ ϥϯ ⲟⲩⲃⲉⲛ̅ϫⲁⲥⲛ̅ϩⲏⲧ. [ϥⲛⲁϯ] ⲇⲉ ⲛ̅ⲟⲩϩⲙⲟⲧ [ⲛ̅ⲛⲉ]ⲧⲑⲃ̅ⲃⲓⲏⲩ
7 Basi mtiini Mungu. Mpingeni ibilisi, naye atawakimbia.
ⲍ̅ϥⲛⲁⲡⲱⲧ ⲥⲁⲃⲟⲗ ⲙⲙⲱⲧⲛ.
8 Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu ninyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu ninyi wenye nia mbili.
ⲏ̅ϩⲱⲛ ⲉϩⲟⲩⲛ ⲉⲡⲛⲟⲩⲧⲉ ⲛ̅ⲧⲁⲣⲉϥϩⲱⲛ ⲉϩⲟⲩⲛ ⲉⲣⲱⲧⲛ̅. ⲧⲃ̅ⲃⲟ ⲛ̅ⲛⲉⲧⲛ̅ϭⲓϫ. ⲛ̅ⲣⲉϥⲣ̅ⲛⲟⲃⲉ. ⲛ̅ⲧⲉⲧⲛ̅ⲧⲃ̅ⲃⲟ ⲙ̅ⲡⲉⲧⲛ̅ϩⲏⲧ. ⲛ̅ϩⲏⲧ ⲥⲛⲁⲩ.
9 Huzunikeni, ombolezeni na kulia. Kicheko chenu na kigeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa huzuni.
ⲑ̅ⲧⲁⲗⲁⲓⲡⲟⲣⲉⲓ ⲁⲩⲱ ⲛ̅ⲧⲉⲧⲛ̅ⲣ̅ϩⲏⲓϥⲉ ⲛ̅ⲧⲉⲧⲛ̅ⲣⲓⲙⲉ. ⲡⲉⲧⲛ̅ⲥⲱⲃⲉ ⲙⲁⲣⲉϥⲕⲟⲧϥ̅ ⲉⲩϩⲏⲃⲉ ⲁⲩⲱ ⲡⲉⲧⲛ̅ⲣⲁϣⲉ ⲉⲩⲱⲕⲙ̅.
10 Jinyenyekezeni mbele za Bwana, naye atawainua.
ⲓ̅ⲑⲃ̅ⲃⲓⲉⲧⲏⲩⲧⲛ̅ ⲙ̅ⲡⲉⲙⲧⲟ ⲉⲃⲟⲗ ⲙ̅ⲡϫⲟⲉⲓⲥ ⲛ̅ⲧⲁⲣⲉϥϫⲁⲥⲧⲏⲩⲧⲛ̅.
11 Ndugu, msineneane mabaya ninyi kwa ninyi. Mtu yeyote anayesema mabaya dhidi ya ndugu yake au kumhukumu anasema dhidi ya sheria na kuihukumu. Unapoihukumu sheria, basi huishiki sheria bali umekuwa hakimu wa kuihukumu hiyo sheria.
ⲓ̅ⲁ̅ⲛⲁⲥⲛⲏⲩ. ⲙ̅ⲡⲣ̅ⲕⲁⲧⲁⲗⲁⲗⲉⲓ ⲛ̅ⲛⲉⲧⲛ̅ⲉⲣⲏⲩ. ⲡⲉⲧⲕⲁⲧⲁⲗⲁⲗⲉⲓ ⲙ̅ⲡⲉϥⲥⲟⲛ ⲏ ⲉϥⲕⲣⲓⲛⲉ ⲙ̅ⲡⲉϥⲥⲟⲛ. ⲉϥⲕⲁⲧⲁⲗⲁⲗⲉⲓ ⲙ̅ⲡⲛⲟⲙⲟⲥ ⲁⲩⲱ ⲉϥⲕⲣⲓⲛⲉ ⲙ̅ⲡⲛⲟⲙⲟⲥ. ⲉϣϫⲉⲉⲕⲕⲣⲓⲛⲉ ⲇⲉ ⲙ̅ⲡⲛⲟⲙⲟⲥ. ⲉⲓⲉ ⲛ̅ⲧⲕ̅ⲟⲩⲣⲉϥⲉⲓⲣⲉ ⲁⲛ ⲙ̅ⲡⲛⲟⲙⲟⲥ. ⲁⲗⲗⲁ ⲛ̅ⲧⲕ̅ⲟⲩⲕⲣⲓⲧⲏⲥ.
12 Yuko Mtoa sheria mmoja tu na yeye peke yake ndiye Hakimu, ndiye awezaye kuokoa au kuangamiza. Lakini wewe ni nani hata umhukumu jirani yako?
ⲓ̅ⲃ̅ⲟⲩⲁ ⲇⲉ ⲡⲉ ⲡⲛⲟⲙⲟⲑⲉⲧⲏⲥ ⲁⲩⲱ ⲡⲉⲕⲣⲓⲧⲏⲥ ⲡⲉⲧⲉⲩⲛ̅ϭⲟⲙ ⲙ̅ⲙⲟϥ ⲉⲧⲁⲛϩⲟ ⲁⲩⲱ ⲉⲧⲁⲕⲟ. ⲛ̅ⲧⲕ̅ ⲛ̅ⲧⲟⲕⲛⲓⲙ ⲉⲕⲕⲣⲓⲛⲉ ⲙ̅ⲡⲉⲧϩⲓⲧⲟⲩⲱⲕ.
13 Basi sikilizeni ninyi msemao, “Leo au kesho tutakwenda katika mji huu ama ule tukae humo mwaka mmoja, tufanye biashara na kupata faida.”
ⲓ̅ⲅ̅ⲛ̅ⲧⲱⲧⲛ̅ ϭⲉ ⲧⲉⲛⲟⲩ ⲛⲉⲧϫⲱ ⲙ̅ⲙⲟⲥ. ϫⲉ ⲙ̅ⲡⲟⲟⲩ ⲏ ⲣⲁⲥⲧⲉ ⲧⲛ̅ⲛⲁⲃⲱⲕ ⲉϩⲟⲩⲛ ⲉⲧⲉⲓⲡⲟⲗⲓⲥ. ⲛ̅ⲧⲛ̅ⲣ̅ⲟⲩⲣⲟⲙⲡⲉ ⲙ̅ⲙⲁⲩ. ⲛ̅ⲧⲛ̅ⲣ̅ⲉϣⲱⲧ ⲛ̅ⲧⲛ̅ϯϩⲏⲩ.
14 Lakini hamjui hata litakalotukia kesho. Maisha yenu ni nini? Ninyi ni ukungu ambao huonekana kwa kitambo kidogo kisha hutoweka.
ⲓ̅ⲇ̅ⲛ̅ⲧⲉⲧⲛ̅ⲥⲟⲟⲩⲛ̅ ⲁⲛ ϫⲉ ⲟⲩ ⲡⲉⲧⲛⲁϣⲱⲡⲉ ⲙ̅ⲙⲱⲧⲛ̅ ⲛ̅ⲣⲁⲥⲧⲉ. ⲉⲣⲉⲡⲉⲧⲛ̅ⲁϩⲉ ⲅⲁⲣ ⲟ ⲛ̅ⲑⲉ ⲛ̅ⲟⲩⲉⲗϩⲱϥ. ⲉϥⲟⲩⲟⲛϩ̅ ⲉⲃⲟⲗ ⲡⲣⲟⲥⲟⲩⲕⲟⲩⲓ. ⲙⲛ̅ⲛ̅ⲥⲱⲥ ⲇⲉ ⲛϥ̅ⲧⲁⲕⲟ.
15 Badala yake, inawapasa kusema, “Kama Bwana akipenda, tutaishi na kufanya hili ama lile.”
ⲓ̅ⲉ̅ⲉⲡⲙⲁ ⲛ̅ⲧⲟϥ ⲛ̅ⲧⲉⲧⲛ̅ϫⲟⲟⲥ. ϫⲉ ⲉⲣϣⲁⲛⲡϫⲟⲉⲓⲥ ⲣ̅ϩⲛⲁϥ ⲛ̅ⲧⲛ̅ⲱⲛϩ̅ ⲧⲛ̅ⲛⲁⲉⲓⲣⲉ ⲙ̅ⲡⲁⲓ ⲏ ⲡⲉⲓⲕⲉⲟⲩⲁ.
16 Kama ilivyo sasa, mnajisifu na kujigamba. Kujisifu kwa namna hiyo ni uovu.
ⲓ̅ⲋ̅ⲧⲉⲛⲟⲩ ⲇⲉ ⲁⲧⲉⲧⲛ̅ϣⲟⲩϣⲟⲩ ⲙ̅ⲙⲱⲧⲛ̅ ϩⲛ̅ⲛⲉⲧⲛ̅ⲙⲛ̅ⲧϫⲁⲥⲓϩⲏⲧ. ϣⲟⲩϣⲟⲩ ⲛⲓⲙ ⲛ̅ⲧⲉⲓⲙⲓⲛⲉ ϩⲟⲟⲩ.
17 Basi mtu yeyote anayejua jema limpasalo kutenda, lakini asilitende, mtu huyo anatenda dhambi.
ⲓ̅ⲍ̅ⲡⲉⲧⲥⲟⲟⲩⲛ̅ ⲇⲉ ⲛ̅ⲣ̅ⲡⲡⲉⲧⲛⲁⲛⲟⲩϥ ⲛ̅ϥⲉⲓⲣⲉ ⲙ̅ⲙⲟϥ ⲁⲛ. ⲟⲩⲛⲟⲃⲉ ⲛⲁϥ ⲡⲉ.

< Yakobo 4 >