< Isaya 1 >
1 Maono kuhusu Yuda na Yerusalemu ambayo Isaya mwana wa Amozi aliyaona wakati wa utawala wa Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda.
vision Isaiah son: child Amoz which to see upon Judah and Jerusalem in/on/with day Uzziah Jotham Ahaz Hezekiah king Judah
2 Sikieni, enyi mbingu! Sikilizeni, enyi dunia! Kwa maana Bwana amesema: “Nimewalisha watoto na kuwalea, lakini wameniasi mimi.
to hear: hear heaven and to listen land: country/planet for LORD to speak: speak son: child to magnify and to exalt and they(masc.) to transgress in/on/with me
3 Ngʼombe anamjua bwana wake, naye punda anajua hori la mmiliki wake, lakini Israeli hajui, watu wangu hawaelewi.”
to know cattle to buy him and donkey crib master his Israel not to know people my not to understand
4 Lo! Taifa lenye dhambi, watu waliolemewa na uovu, uzao wa watenda mabaya, watoto waliozoelea upotovu! Wamemwacha Bwana, Wamemkataa kwa dharau yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli na kumgeuzia kisogo.
woe! nation to sin people heavy iniquity: crime seed: children be evil son: child to ruin to leave: forsake [obj] LORD to spurn [obj] holy Israel be a stranger back
5 Kwa nini mzidi kupigwa? Kwa nini kudumu katika uasi? Kichwa chako chote kimejeruhiwa, moyo wako wote ni mgonjwa.
upon what? to smite still to add: again revolt all head to/for sickness and all heart faint
6 Kutoka wayo wako wa mguu hadi kwenye utosi wa kichwa chako hakuna uzima: ni majeraha matupu na makovu na vidonda vitokavyo damu, havikusafishwa au kufungwa wala kulainishwa kwa mafuta.
from palm: sole foot and till head nothing in/on/with him soundness wound and wound and wound fresh not to crush and not to saddle/tie and not be tender in/on/with oil
7 Nchi yenu imekuwa ukiwa, miji yenu imeteketezwa kwa moto; nchi yenu imeachwa tupu na wageni mbele ya macho yenu, imeharibiwa kama vile imepinduliwa na wageni.
land: country/planet your devastation city your to burn fire land: soil your to/for before you be a stranger to eat [obj] her and devastation like/as overthrow be a stranger
8 Binti Sayuni ameachwa kama kipenu katika shamba la mizabibu, kama kibanda katika shamba la matikitimaji, kama mji uliohusuriwa.
and to remain daughter Zion like/as booth in/on/with vineyard like/as lodge in/on/with cucumber field like/as city to watch
9 Kama Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asingelituachia walionusurika, tungelikuwa kama Sodoma, tungelifanana na Gomora.
unless LORD Hosts to remain to/for us survivor like/as little like/as Sodom to be to/for Gomorrah to resemble
10 Sikieni neno la Bwana, ninyi watawala wa Sodoma; sikilizeni sheria ya Mungu wetu, enyi watu wa Gomora!
to hear: hear word LORD chief Sodom to listen instruction God our people Gomorrah
11 Bwana anasema, “Wingi wa sadaka zenu, ni kitu gani kwangu? Ninazo sadaka za kuteketezwa nyingi kupita kiasi, za kondoo dume na mafuta ya wanyama walionona. Sipendezwi na damu za mafahali wala za wana-kondoo na mbuzi.
to/for what? to/for me abundance sacrifice your to say LORD to satisfy burnt offering ram and fat fatling and blood bullock and lamb and goat not to delight in
12 Mnapokuja kujihudhurisha mbele zangu, ni nani aliyewataka ninyi mfanye hivyo, huku kuzikanyaga nyua zangu?
for to come (in): come to/for to see: see face: before my who? to seek this from hand: themselves your to trample court my
13 Acheni kuniletea sadaka zisizokuwa na maana! Uvumba wenu ni chukizo kwangu. Miandamo ya Mwezi, Sabato na makusanyiko ya ibada: siwezi kuvumilia makusanyiko yenu maovu.
not to add: again to come (in): bring offering vanity: vain incense abomination he/she/it to/for me month: new moon and Sabbath to call: call to assembly not be able evil: wickedness and assembly
14 Sikukuu zenu za Miandamo ya Mwezi, na sikukuu zenu zilizoamriwa: moyo wangu unazichukia. Zimekuwa mzigo kwangu, nimechoka kuzivumilia.
month: new moon your and meeting: festival your to hate soul my to be upon me to/for burden be weary to lift: bear
15 Mnaponyoosha mikono yenu katika maombi, nitaficha macho yangu nisiwaone; hata mkiomba maombi mengi sitasikiliza. Mikono yenu imejaa damu;
and in/on/with to spread you palm your to conceal eye my from you also for to multiply prayer nothing I to hear: hear hand your blood to fill
16 jiosheni na mkajitakase. Yaondoeni matendo yenu maovu mbele zangu! Acheni kutenda mabaya,
to wash: wash to clean to turn aside: remove evil deed your from before eye my to cease be evil
17 jifunzeni kutenda mema! Tafuteni haki, watieni moyo walioonewa. Teteeni shauri la yatima, wateteeni wajane.
to learn: learn be good to seek justice to bless oppression to judge orphan to contend widow
18 “Njooni basi tuhojiane,” asema Bwana. “Ingawa dhambi zenu ni kama rangi nyekundu, zitakuwa nyeupe kama theluji; ingawa ni nyekundu sana kama damu, zitakuwa nyeupe kama sufu.
to go: come! please and to rebuke to say LORD if to be sin your like/as scarlet like/as snow to whiten if to redden like/as worm like/as wool to be
19 Kama mkikubali na kutii, mtakula mema ya nchi,
if be willing and to hear: obey goodness [the] land: country/planet to eat
20 lakini kama mkikataa na kuasi, mtaangamizwa kwa upanga.” Kwa kuwa kinywa cha Bwana kimenena.
and if to refuse and to rebel sword to eat for lip LORD to speak: speak
21 Tazama jinsi mji uliokuwa mwaminifu umekuwa kahaba! Mwanzoni ulikuwa umejaa unyofu, haki ilikuwa inakaa ndani yake, lakini sasa ni wauaji!
how? to be to/for to fornicate town be faithful full justice righteousness to lodge in/on/with her and now to murder
22 Fedha yenu imekuwa takataka, divai yenu nzuri imechanganywa na maji.
silver: money your to be to/for dross liquor your to weaken in/on/with water
23 Watawala wenu ni waasi, rafiki wa wevi, wote wanapenda rushwa na kukimbilia hongo. Hawatetei yatima, shauri la mjane haliletwi mbele yao lisikilizwe.
ruler your to rebel and companion thief all his to love: lover bribe and to pursue reward orphan not to judge and strife widow not to come (in): come to(wards) them
24 Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mwenye Nguvu wa Israeli, asema hivi: “Lo, nitapata faraja kutoka kwa adui zangu na kujilipizia kisasi juu ya watesi wangu.
to/for so utterance [the] lord LORD Hosts mighty Israel woe! to be sorry: comfort from enemy my and to avenge from enemy my
25 Nitauelekeza mkono wangu dhidi yenu, nitawasafisha takataka zenu zote na kuwaondolea unajisi wenu wote.
and to return: return hand my upon you and to refine like/as lye dross your and to turn aside: remove all tin your
26 Nitawarudishia waamuzi wenu kama ilivyokuwa siku za zamani, nao washauri wenu kama ilivyokuwa mwanzoni. Baadaye utaitwa, Mji wa Haki, Mji Mwaminifu.”
and to return: rescue to judge you like/as in/on/with first and to advise you like/as in/on/with beginning after so to call: call by to/for you city [the] righteousness town be faithful
27 Sayuni itakombolewa kwa haki, wale waliomo ndani yake waliotubu kwa uaminifu.
Zion in/on/with justice to ransom and to return: repent her in/on/with righteousness
28 Lakini waasi na wenye dhambi wote wataangamizwa, nao wanaomwacha Bwana wataangamia.
and breaking to transgress and sinner together and to leave: forsake LORD to end: destroy
29 “Mtaaibika kwa sababu ya hiyo mialoni ambayo mlifurahia, mtafadhaika kwa sababu ya bustani mlizozichagua.
for be ashamed from terebinth which to desire and be ashamed from [the] garden which to choose
30 Mtakuwa kama mwaloni wenye majani yanayonyauka, kama bustani isiyokuwa na maji.
for to be like/as oak to wither leaf her and like/as garden which water nothing to/for her
31 Mtu mwenye nguvu atatoweka kama majani makavu yawakayo moto, na kazi yake kama cheche ya moto; vyote vitaungua pamoja, wala hakuna wa kuuzima huo moto.”
and to be [the] strong to/for tow and work his to/for spark and to burn: burn two their together and nothing to quench