< Isaya 9 >

1 Hata hivyo, hapatakuwepo huzuni tena kwa wale waliokuwa katika dhiki. Wakati uliopita aliidhili nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, lakini katika siku zijazo ataiheshimu Galilaya ya Mataifa, karibu na njia ya bahari, kando ya Yordani:
Dans le premier temps a été allégée la terre de Zabulon, ainsi que la terre de Nephthali; et dans le dernier, a été aggravée la voie de la mer, au-delà du Jourdain, la voie de la Galilée des nations.
2 Watu wanaotembea katika giza wameona nuru kuu, wale wanaoishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.
Le peuple qui marchait dans les ténèbres a vu une grande lumière; pour ceux qui habitaient dans la région de l’ombre de la mort, une lumière s’est levée.
3 Umelikuza taifa, na kuzidisha furaha yao, wanafurahia mbele zako, kama watu wanavyofurahia wakati wa mavuno, kama watu wafurahivyo wagawanyapo nyara.
Vous avez augmenté la nation et vous n’avez pas agrandi sa joie. Ils se réjouiront devant vous, comme ceux qui se réjouissent dans la moisson; et comme exultent les vainqueurs après le butin pris, quand ils partagent les dépouilles.
4 Kama vile siku ya kushindwa kwa Wamidiani, umevunja nira iliyowalemea, ile gongo mabegani mwao na fimbo yake yeye aliyewaonea.
Car le joug de son fardeau, la verge de son épaule, et le sceptre de son exacteur, vous en avez triomphé, comme à la journée de Madian.
5 Kila kiatu cha askari kilichotumiwa vitani, na kila vazi lililovingirishwa katika damu vitawekwa kwa ajili ya kuchomwa, vitakuwa kuni za kuwasha moto.
Parce que tout pillage fait dans le tumulte, et tout vêtement souillé de sang sera en combustion et la pâture du feu.
6 Kwa maana, kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanaume, nao utawala utakuwa mabegani mwake. Naye ataitwa Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mfalme wa Amani.
Car UN ENFANT NOUS EST NÉ, et un fils nous a été donné; et sa principauté est sur son épaule, et son nom sera appelé Admirable, Conseiller, Dieu, Fort, Père du siècle à venir. Prince de la paix.
7 Kuongezeka kwa utawala wake na amani hakutakuwa na mwisho. Atatawala katika kiti cha enzi cha Daudi na juu ya ufalme wake, akiuthibitisha na kuutegemeza kwa haki na kwa adili, tangu wakati huo na hata milele. Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote utatimiza haya.
Son empire s’accroîtra et la paix n’aura pas de fin; sur le trône de David et sur son royaume il s’assiéra pour raffermir et le fortifier dans le jugement et la justice, dès maintenant à tout jamais. Le zèle du Seigneur des armées fera cela.
8 Bwana ametuma ujumbe dhidi ya Yakobo, utamwangukia Israeli.
Le Seigneur a envoyé une parole dans Jacob, et elle est tombée dans Israël.
9 Watu wote watajua hili: Efraimu na wakazi wa Samaria, wanaosema kwa kiburi na majivuno ya mioyo,
Et tout le peuple d’Ephraïm le saura de même que ceux qui habitent Samarie, qui disent dans l’orgueil et l’enflure du cœur:
10 “Matofali yameanguka chini, lakini tutajenga tena kwa mawe yaliyochongwa, mitini imeangushwa, lakini tutapanda mierezi badala yake.”
Les briques sont tombées; mais nous bâtirons avec des pierres de taille; on a coupé nos sycomores, nous y substituerons des cèdres.
11 Lakini Bwana amemtia nguvu adui wa Resini dhidi yao na kuchochea watesi wao.
Et le Seigneur élèvera les ennemis de Rasin sur lui, et il fera venir tous ses ennemis en foule:
12 Waashuru kutoka upande wa mashariki na Wafilisti kutoka upande wa magharibi wameila Israeli kwa kinywa kilichopanuliwa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
La Syrie de l’Orient, les Philistins de l’Occident; et ils dévoreront Israël de toute leur bouche. Avec toutes ces choses sa fureur n’a pas été détournée, mais sa main est encore étendue;
13 Lakini watu hawajamrudia yeye aliyewapiga, wala hawajamtafuta Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Et le peuple n’est pas revenu vers celui qui le frappait, et ils n’ont pas recherché le Seigneur des armées.
14 Kwa hiyo Bwana atakatilia mbali kutoka Israeli kichwa na mkia, tawi la mtende na tete katika siku moja.
Et le Seigneur retranchera d’Israël, dans un même jour, la tête et la queue, celui qui plie et celui qui réfrène.
15 Wazee na watu mashuhuri ndio vichwa, nao manabii wanaofundisha uongo ndio mkia.
Le vieillard et l’homme en dignité, c’est la tête; et le prophète qui enseigne le mensonge, c’est la queue.
16 Wale wanaowaongoza watu hawa wanawapotosha, nao wale wanaoongozwa wamepotoka.
Et ceux qui appellent ce peuple heureux seront des séducteurs; et ceux qui sont appelés heureux seront précipités.
17 Kwa hiyo Bwana hatawafurahia vijana, wala hatawahurumia yatima na wajane, kwa kuwa kila mmoja wao hamchi Mungu, nao ni waovu, na kila kinywa kinanena upotovu. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
À cause de cela le Seigneur ne mettera pas sa joie dans ses jeunes hommes; et de ses orphelins, et de ses veuves, il n’aura pas pitié; parce que tous sont hypocrites et méchants, et que toute bouche a parlé folie. Avec toutes ces choses sa fureur n’a pas été détournée, mais sa main est encore étendue.
18 Hakika uovu huwaka kama moto; huteketeza michongoma na miiba, huwasha moto vichaka vya msituni, hujiviringisha kuelekea juu kama nguzo ya moshi.
Car comme un feu, l’impiété s’est allumée, et elle dévorera la ronce et l’épine; et elle s’embrasera comme dans l’épaisseur d’une forêt; et une fumée formera des tourbillons en s’élevant.
19 Kwa hasira ya Bwana Mwenye Nguvu Zote nchi itachomwa kwa moto, nao watu watakuwa kuni za kuchochea moto. Hakuna mtu atakayemhurumia ndugu yake.
Par la colère du Seigneur des armées, la terre a été bouleversée, et le peuple sera comme la pâture du feu; l’homme n’épargnera pas son frère.
20 Upande wa kuume watakuwa wakitafuna, lakini bado wataona njaa; upande wa kushoto watakuwa wakila, lakini hawatashiba. Kila mmoja atajilisha kwa nyama ya mtoto wake mwenyewe:
Et il se tournera à droite et il aura faim; et il mangera en allant à gauche, et il ne sera pas rassasié; chacun dévorera la chair de son bras: Manassé dévorera Ephraïm, et Ephraïm Manassé; et eux ensemble seront contre Juda.
21 Manase atamla Efraimu, naye Efraimu atamla Manase; nao pamoja watakuwa kinyume na Yuda. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Avec toutes ces choses sa fureur n’a pas été détournée, mais sa main est encore étendue.

< Isaya 9 >