< Isaya 9 >
1 Hata hivyo, hapatakuwepo huzuni tena kwa wale waliokuwa katika dhiki. Wakati uliopita aliidhili nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, lakini katika siku zijazo ataiheshimu Galilaya ya Mataifa, karibu na njia ya bahari, kando ya Yordani:
But the darkness shall not remain where now is distress; Of old he brought the land of Zebulon and the land of Naphtali into contempt; In future times shall he bring the land of the sea beyond Jordan, the circle of the gentiles, into honor.
2 Watu wanaotembea katika giza wameona nuru kuu, wale wanaoishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.
The people that walk in darkness behold a great light; They who dwell in the land of death-like shade, Upon them a light shineth.
3 Umelikuza taifa, na kuzidisha furaha yao, wanafurahia mbele zako, kama watu wanavyofurahia wakati wa mavuno, kama watu wafurahivyo wagawanyapo nyara.
Thou enlargest the nation; Thou increasest their joy; They rejoice before thee with the joy of harvest, With the joy of those who divide the spoil.
4 Kama vile siku ya kushindwa kwa Wamidiani, umevunja nira iliyowalemea, ile gongo mabegani mwao na fimbo yake yeye aliyewaonea.
For thou breakest their heavy yoke, And the rod that smote their backs, And the scourge of the taskmaster, As in the day of Midian.
5 Kila kiatu cha askari kilichotumiwa vitani, na kila vazi lililovingirishwa katika damu vitawekwa kwa ajili ya kuchomwa, vitakuwa kuni za kuwasha moto.
For every greave of the warrior in battle, And the war-garment rolled in blood, Shall be burned; yea, it shall be food for the fire.
6 Kwa maana, kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanaume, nao utawala utakuwa mabegani mwake. Naye ataitwa Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mfalme wa Amani.
For to us a child is born, To us a son is given, And the government shall be upon his shoulder, And he shall be called Wonderful, counsellor, mighty potentate, Everlasting father, prince of peace;
7 Kuongezeka kwa utawala wake na amani hakutakuwa na mwisho. Atatawala katika kiti cha enzi cha Daudi na juu ya ufalme wake, akiuthibitisha na kuutegemeza kwa haki na kwa adili, tangu wakati huo na hata milele. Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote utatimiza haya.
His dominion shall be great, And peace without end shall be upon the throne of David and his kingdom, To fix and establish it Through justice and equity, Henceforth and forever. The zeal of Jehovah of hosts will do this.
8 Bwana ametuma ujumbe dhidi ya Yakobo, utamwangukia Israeli.
The Lord sendeth a word against Jacob; It cometh down to Israel.
9 Watu wote watajua hili: Efraimu na wakazi wa Samaria, wanaosema kwa kiburi na majivuno ya mioyo,
His whole people shall feel it, Ephraim, and the inhabitants of Samaria, Who say in pride and arrogance of heart,
10 “Matofali yameanguka chini, lakini tutajenga tena kwa mawe yaliyochongwa, mitini imeangushwa, lakini tutapanda mierezi badala yake.”
“The bricks are fallen down, but we will build with hewn stones; The sycamores are cut down, but we will replace them with cedars.”
11 Lakini Bwana amemtia nguvu adui wa Resini dhidi yao na kuchochea watesi wao.
Jehovah will raise up the enemies of Rezin against them, And will arm their adversaries;
12 Waashuru kutoka upande wa mashariki na Wafilisti kutoka upande wa magharibi wameila Israeli kwa kinywa kilichopanuliwa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
The Syrians before, the Philistines behind, Who shall devour Israel with wide jaws. For all this his anger is not turned away, But his hand is stretched out still.
13 Lakini watu hawajamrudia yeye aliyewapiga, wala hawajamtafuta Bwana Mwenye Nguvu Zote.
The people turn not to him that smiteth them; Neither do they seek Jehovah of hosts.
14 Kwa hiyo Bwana atakatilia mbali kutoka Israeli kichwa na mkia, tawi la mtende na tete katika siku moja.
Therefore shall Jehovah cut off from Israel the head and the tail, The palm-branch and the rush, in one day.
15 Wazee na watu mashuhuri ndio vichwa, nao manabii wanaofundisha uongo ndio mkia.
[[The aged and the honorable are the head, And the prophet that speaketh falsehood is the tail.]]
16 Wale wanaowaongoza watu hawa wanawapotosha, nao wale wanaoongozwa wamepotoka.
For the leaders of this people lead them astray, And they that are led by them go to destruction.
17 Kwa hiyo Bwana hatawafurahia vijana, wala hatawahurumia yatima na wajane, kwa kuwa kila mmoja wao hamchi Mungu, nao ni waovu, na kila kinywa kinanena upotovu. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Therefore shall the Lord have no joy in their young men, And on their orphans and widows he shall have no compassion; For they are all profane, and evil-doers; Every mouth speaketh folly. For all this his anger is not turned away, But his hand is stretched out still.
18 Hakika uovu huwaka kama moto; huteketeza michongoma na miiba, huwasha moto vichaka vya msituni, hujiviringisha kuelekea juu kama nguzo ya moshi.
For wickedness burneth like a fire, It consumeth the briers and thorns, And it kindleth the thicket of the forest, So that it goeth up in columns of smoke.
19 Kwa hasira ya Bwana Mwenye Nguvu Zote nchi itachomwa kwa moto, nao watu watakuwa kuni za kuchochea moto. Hakuna mtu atakayemhurumia ndugu yake.
Through the wrath of Jehovah of hosts is the land burned, And the people are food for the fire; No one spareth another.
20 Upande wa kuume watakuwa wakitafuna, lakini bado wataona njaa; upande wa kushoto watakuwa wakila, lakini hawatashiba. Kila mmoja atajilisha kwa nyama ya mtoto wake mwenyewe:
They consume on the right hand, and yet are hungry; They devour on the left, and are not satisfied; Every one devoureth the flesh of his arm.
21 Manase atamla Efraimu, naye Efraimu atamla Manase; nao pamoja watakuwa kinyume na Yuda. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Manasseh is against Ephraim, and Ephraim against Manasseh, And both together against Judah. For all this his anger is not turned away, But his hand is stretched out still.