< Isaya 9 >
1 Hata hivyo, hapatakuwepo huzuni tena kwa wale waliokuwa katika dhiki. Wakati uliopita aliidhili nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, lakini katika siku zijazo ataiheshimu Galilaya ya Mataifa, karibu na njia ya bahari, kando ya Yordani:
For [there will be] no gloom on her who [is] distressed as at the former time. The land of Zebulun and the land of Naphtali, So the latter has honored the way of the sea, Beyond the Jordan, Galilee of the nations.
2 Watu wanaotembea katika giza wameona nuru kuu, wale wanaoishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.
The people who are walking in darkness Have seen a great light, Dwellers in a land of death-shade, Light has shone on them.
3 Umelikuza taifa, na kuzidisha furaha yao, wanafurahia mbele zako, kama watu wanavyofurahia wakati wa mavuno, kama watu wafurahivyo wagawanyapo nyara.
You have multiplied the nation, You have made its joy great, They have rejoiced before You as the joy in harvest, As [men] rejoice in their apportioning spoil.
4 Kama vile siku ya kushindwa kwa Wamidiani, umevunja nira iliyowalemea, ile gongo mabegani mwao na fimbo yake yeye aliyewaonea.
Because the yoke of its burden, And the staff of its shoulder, the rod of its exactor, You have broken as [in] the day of Midian.
5 Kila kiatu cha askari kilichotumiwa vitani, na kila vazi lililovingirishwa katika damu vitawekwa kwa ajili ya kuchomwa, vitakuwa kuni za kuwasha moto.
For every battle of a warrior [is] with rushing, and raiment rolled in blood, And it has been for burning—fuel of fire.
6 Kwa maana, kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanaume, nao utawala utakuwa mabegani mwake. Naye ataitwa Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mfalme wa Amani.
For a Child has been born to us, A Son has been given to us, And the dominion is on His shoulder, And He calls His Name Wonderful, Counselor, Mighty God, Father of Eternity, Prince of Peace.
7 Kuongezeka kwa utawala wake na amani hakutakuwa na mwisho. Atatawala katika kiti cha enzi cha Daudi na juu ya ufalme wake, akiuthibitisha na kuutegemeza kwa haki na kwa adili, tangu wakati huo na hata milele. Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote utatimiza haya.
Of the increase of [His] dominion, And of peace, there is no end, On the throne of David, and on His kingdom, To establish it, and to support it, In judgment and in righteousness, From now on, even for all time, The zeal of YHWH of Hosts does this.
8 Bwana ametuma ujumbe dhidi ya Yakobo, utamwangukia Israeli.
The Lord has sent a word into Jacob, And it has fallen in Israel.
9 Watu wote watajua hili: Efraimu na wakazi wa Samaria, wanaosema kwa kiburi na majivuno ya mioyo,
And the people have known—all of it, Ephraim, and the inhabitant of Samaria, In pride and in greatness of heart, saying,
10 “Matofali yameanguka chini, lakini tutajenga tena kwa mawe yaliyochongwa, mitini imeangushwa, lakini tutapanda mierezi badala yake.”
“Bricks have fallen, and we build hewn work, Sycamores have been cut down, and we renew cedars.”
11 Lakini Bwana amemtia nguvu adui wa Resini dhidi yao na kuchochea watesi wao.
And YHWH sets the adversaries of Rezin on high above him, And he joins his enemies together,
12 Waashuru kutoka upande wa mashariki na Wafilisti kutoka upande wa magharibi wameila Israeli kwa kinywa kilichopanuliwa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Aram from before, and Philistia from behind, And they devour Israel with the whole mouth. With all this His anger has not turned back, And His hand is still stretched out.
13 Lakini watu hawajamrudia yeye aliyewapiga, wala hawajamtafuta Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And the people has not turned back to Him who is striking it, And they have not sought YHWH of Hosts.
14 Kwa hiyo Bwana atakatilia mbali kutoka Israeli kichwa na mkia, tawi la mtende na tete katika siku moja.
And YHWH cuts off head and tail from Israel, Branch and reed—the same day.
15 Wazee na watu mashuhuri ndio vichwa, nao manabii wanaofundisha uongo ndio mkia.
Elderly and accepted of faces—he [is] the head, And prophet teaching falsehood—he [is] the tail.
16 Wale wanaowaongoza watu hawa wanawapotosha, nao wale wanaoongozwa wamepotoka.
And the eulogists of this people are causing to err, And its eulogized ones are consumed.
17 Kwa hiyo Bwana hatawafurahia vijana, wala hatawahurumia yatima na wajane, kwa kuwa kila mmoja wao hamchi Mungu, nao ni waovu, na kila kinywa kinanena upotovu. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Therefore, the Lord does not rejoice over its young men, And He does not pity its orphans and its widows, For everyone [is] profane, and an evildoer, And every mouth is speaking folly. With all this His anger has not turned back, And His hand is still stretched out.
18 Hakika uovu huwaka kama moto; huteketeza michongoma na miiba, huwasha moto vichaka vya msituni, hujiviringisha kuelekea juu kama nguzo ya moshi.
For wickedness has burned as a fire, It devours brier and thorn, And it kindles in thickets of the forest, And they lift themselves up, an exaltation of smoke!
19 Kwa hasira ya Bwana Mwenye Nguvu Zote nchi itachomwa kwa moto, nao watu watakuwa kuni za kuchochea moto. Hakuna mtu atakayemhurumia ndugu yake.
In the wrath of YHWH of Hosts The land has been consumed, And the people is as fuel of fire; A man has no pity on his brother,
20 Upande wa kuume watakuwa wakitafuna, lakini bado wataona njaa; upande wa kushoto watakuwa wakila, lakini hawatashiba. Kila mmoja atajilisha kwa nyama ya mtoto wake mwenyewe:
And cuts down on the right, and has been hungry, And he devours on the left, And they have not been satisfied, They each devour the flesh of his own arm.
21 Manase atamla Efraimu, naye Efraimu atamla Manase; nao pamoja watakuwa kinyume na Yuda. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Manasseh—Ephraim, and Ephraim—Manasseh, Together they [are] against Judah, With all this His anger has not turned back. And His hand is still stretched out!