< Isaya 8 >

1 Bwana akaniambia, “Chukua gombo kubwa, uandike juu yake kwa kalamu ya kawaida jina: Maher-Shalal-Hash-Bazi.
RAB bana şöyle dedi: “Büyük bir levha alıp okunaklı harflerle üzerine, ‘Maher-Şalal-Haş-Baz’ yaz.
2 Nami nitawaita kuhani Uria, na Zekaria mwana wa Yeberekia kama mashahidi wangu waaminifu.”
Kâhin Uriya ile Yeverekya oğlu Zekeriya'yı kendime güvenilir tanık seçiyorum.”
3 Kisha nikaenda kwa nabii mke, naye akapata mimba, akazaa mwana. Kisha Bwana akaniambia, “Mwite huyo mtoto Maher-Shalal-Hash-Bazi.
Peygamber olan karım bundan bir süre sonra gebe kaldı ve bir erkek çocuk doğurdu. RAB bana, “Adını ‘Maher-Şalal-Haş-Baz’ koy” dedi,
4 Kabla mtoto hajaweza kusema ‘Baba yangu’ au ‘Mama yangu,’ utajiri wa Dameski na nyara za Samaria zitachukuliwa na mfalme wa Ashuru.”
“Çocuk daha ‘Anne, baba’ demesini öğrenmeden, Şam'ın serveti ve Samiriye'nin ganimeti Asur Kralı'na götürülecek.”
5 Bwana akasema nami tena:
RAB bana yine seslenip dedi ki,
6 “Kwa sababu watu hawa wamekataa maji ya Shilo yatiririkayo taratibu wakamfurahia Resini na mwana wa Remalia,
“Bu halk usul usul akan Şiloah sularını reddettiği, Resin'le Remalya'nın oğluyla mutlu olduğu için,
7 kwa hiyo Bwana yu karibu kuleta dhidi yao mafuriko makubwa ya Mto: yaani mfalme wa Ashuru na fahari yake yote. Yatafurika juu ya mifereji yake yote, yatamwagikia juu ya kingo zake zote,
ben Rab, Fırat'ın kabaran güçlü sularını –bütün dehşetiyle Asur Kralı'nı– üzerlerine salacağım. Yatağından taşan ırmak, kıyılarını su altında bırakacak.
8 na kufika hadi Yuda, yakizunguka kwa kasi juu yake, yakipita katikati na yakifika hadi shingoni. Mabawa yake yaliyokunjuliwa yatafunika upana wa nchi yako, Ee Imanueli!”
Yahuda'yı kaplayan sular her şeyi silip süpürerek adam boyu yükselecek, ülkeni boydan boya dolduracak, ey İmmanuel!”
9 Inueni kilio cha vita, enyi mataifa, na mkavunjwevunjwe! Sikilizeni, enyi nyote nchi za mbali. Jiandaeni kwa vita, nanyi mkavunjwevunjwe! Jiandaeni kwa vita, nanyi mkavunjwevunjwe!
Ey halklar, yıkıma, bozguna uğrayacaksınız. Yeryüzünün en uç köşeleri, kulak verin. Savaşmaya, bozguna uğramaya hazırlanın. Evet, savaşa ve bozguna hazır olun.
10 Wekeni mikakati yenu, lakini itashindwa; fanyeni mipango yenu, lakini haitafanikiwa, kwa maana Mungu yu pamoja nasi.
İstediğinizi tasarlayın, hepsi boşa gidecek. İstediğiniz kadar konuşun, hiçbiri gerçekleşmeyecek. Çünkü Tanrı bizimledir.
11 Bwana alisema nami mkono wake wenye nguvu ukiwa juu yangu, akinionya nisifuate njia za taifa hili. Akasema:
RAB beni halkın tuttuğu yoldan gitmeme konusunda şiddetle uyararak şöyle dedi:
12 “Usiite fitina kila kitu ambacho watu hawa hukiita fitina, usiogope kile wanachokiogopa, wala usikihofu.
“Onların entrika dediği her şeye Siz entrika demeyin; Onların korktuğundan korkmayın, yılmayın.
13 Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye peke yake ikupasaye kumheshimu kuwa mtakatifu, ndiye peke yake utakayemwogopa, ndiye peke yake utakayemhofu,
“Her Şeye Egemen RAB'bi kutsal sayın. Korkunuz, yılgınız O'ndan olsun.
14 naye atakuwa mahali patakatifu; lakini kwa nyumba zote mbili za Israeli atakuwa jiwe lile linalosababisha watu kujikwaa na mwamba wa kuwaangusha. Kwa watu wa Yerusalemu, atakuwa mtego na tanzi.
Tapınak O olacak. İsrail'in iki krallığı içinse Sürçme taşı ve tökezleme kayası, Yeruşalim'de yaşayanlar için Kapan ve tuzak olacak.
15 Wengi wao watajikwaa; wataanguka na kuvunjika, watategwa na kunaswa.”
Birçokları sendeleyip düşecek, parçalanacak, Tuzağa düşüp ele geçecek.”
16 Funga ushuhuda na kutia muhuri sheria miongoni mwa wanafunzi wangu.
Ya RAB, öğrencilerim arasında bildirimi koru, Öğretimi mühürle!
17 Nitamngojea Bwana, ambaye ameificha nyumba ya Yakobo uso wake. Nitaliweka tumaini langu kwake.
Kendini Yakup'un soyundan gizleyen RAB'bi özlemle bekliyorum, umudum O'nda.
18 Niko hapa, pamoja na watoto ambao Bwana amenipa. Sisi ni ishara na mfano wake katika Israeli, kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayeishi juu ya Mlima Sayuni.
Ben ve RAB'bin bana verdiği çocuklar, Siyon Dağı'nda oturan Her Şeye Egemen RAB'bin İsrail'deki belirtileri ve işaretleriyiz.
19 Wakati watu wanapowaambia ninyi kutafuta ushauri kwa waaguzi na wenye kuongea na mizimu, ambao hunongʼona na kunungʼunika, je, watu wasingeuliza kwa Mungu wao? Kwa nini watake shauri kwa wafu kwa ajili ya walio hai?
Birileri size, “Fısıldaşıp mırıldanan medyumlarla ruh çağıranlara danışın” dediğinde, “Halk kendi Tanrısı'na danışmaz mı; yaşayanlar için ölülere mi danışılır?” deyin.
20 Kwa sheria na kwa ushuhuda! Kama hawatasema sawasawa na neno hili, hawana mwanga wa mapambazuko.
Tanrı'nın öğretisine ve bildirisine dönmek gerek! Böyle düşünmezlerse, onlar için hiç şafak sökmeyecek.
21 Watazunguka katika nchi yote, wakiwa na dhiki na njaa. Watakapotaabika kwa njaa, watapatwa na hasira kali, nao, wakiwa wanatazama juu, watamlaani mfalme wao na Mungu wao.
Aç ve çaresiz, ülkede dolanıp duracaklar. Aç kalınca öfkelenip krallarına, Tanrıları'na lanet edecekler. Yukarıya da
22 Kisha wataangalia duniani na kuona tu dhiki na giza, hofu na huzuni tupu, nao watasukumiwa kwenye giza nene kabisa.
dünyaya da baksalar sıkıntıdan, karanlıktan, korkunç karanlıktan başka bir şey görmeyecekler. Kovulacakları yer koyu karanlıktır.

< Isaya 8 >