< Isaya 7 >
1 Wakati Ahazi mwana wa Yothamu, mwana wa Uzia, alipokuwa mfalme wa Yuda, Mfalme Resini wa Aramu, na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli walipanda kupigana dhidi ya Yerusalemu, lakini hawakuweza kuushinda.
Et dans les jours d'Achaz, fils de Joatham, fils d'Ozias, roi de Juda, il arriva que Rasin, roi d'Aram, et Phacée, fils de Romélie, roi d'Israël, marchèrent contre Jérusalem pour lui faire la guerre; mais ils ne purent la tenir assiégée.
2 Wakati huu nyumba ya Daudi iliambiwa, “Aramu wameungana na Efraimu.” Kwa hiyo mioyo ya Ahazi na watu wake ilitikiswa, kama miti ya msituni inavyotikiswa na upepo.
Et un message fut apporté en la maison de David, disant: Aram est coalisé avec Éphraïm. Et l'âme du roi fut saisie de stupeur, ainsi que l'âme de son peuple; comme dans une forêt les feuilles sont agitées par le vent.
3 Ndipo Bwana akamwambia Isaya, “Toka uende, wewe na mwanao Shear-Yashubu, mkutane na Ahazi huko mwisho wa mfereji wa Bwawa la Juu, kwenye barabara iendayo Shamba la Dobi.
Et le Seigneur dit à Isaïe: Va à la rencontre d'Achaz, toi et ton fils Jasub qui te reste; prends le chemin d'en haut dans le champ du Foulon près la piscine;
4 Mwambie, ‘Uwe mwangalifu, utulie na usiogope. Usife moyo kwa ajili ya watu hawa wawili walio kama visiki vya kuni vifukavyo moshi, kwa ajili ya hasira kali ya Resini na Aramu na ya mwana wa Remalia.
Et dis au roi: Tiens-toi en repos, et sois sans crainte; que ton âme ne soit pas abattue par ces deux bouts de tison qui fument; car, lorsque le transport de ma colère éclatera, je te guérirai encore une fois.
5 Aramu, Efraimu na mwana wa Remalia wamepanga shauri baya ili wakuangamize, wakisema,
Quant au fils d'Aram et au fils de Romélie, parce qu'ils ont conçu un mauvais dessein, disant:
6 “Tuishambulie Yuda, naam, tuirarue vipande vipande na kuigawa miongoni mwetu, na kumtawaza mwana wa Tabeeli awe mfalme juu yake.”
Montons en Judée, et, nous liguant contre eux, soumettons-les à nous, et donnons-leur pour roi le fils de Tabéel;
7 Lakini Bwana Mwenyezi asema hivi: “‘Jambo hili halitatendeka, halitatokea,
Voici ce que dit le Seigneur des armées: Ce complot ne subsistera pas, il ne s'accomplira point.
8 kwa kuwa kichwa cha Aramu ni Dameski, na kichwa cha Dameski ni Resini peke yake. Katika muda wa miaka sitini na mitano, Efraimu atakuwa ameharibiwa kiasi kwamba hataweza tena kuwa taifa.
Mais Damas restera la capitale de Syrie, et Rasin, roi de Damas. Et soixante-cinq ans encore, le royaume d'Éphraïm cessera d'être un peuple,
9 Kichwa cha Efraimu ni Samaria, na kichwa cha Samaria ni mwana wa Remalia peke yake. Kama hamtasimama thabiti katika imani yenu, hamtaimarika kamwe.’”
Et Samarie, la capitale d'Éphraïm, et le fils de Romélie, la capitale de Samarie. Et si vous ne me croyez point, c'est que vous manquerez d'intelligence.
10 Bwana akasema na Ahazi tena,
Et le Seigneur continua de parler à Achaz, disant:
11 “Mwombe Bwana Mungu wako ishara, iwe kwenye vina virefu sana, au kwenye vimo virefu sana.” (Sheol )
Demande un signe au Seigneur ton Dieu, soit dans le ciel, soit dans l'abîme. (Sheol )
12 Lakini Ahazi akasema, “Sitaomba; sitamjaribu Bwana.”
Et Achaz dit: Non, je ne demanderai rien, et je ne tenterai point le Seigneur.
13 Ndipo Isaya akasema, “Sikia sasa, ewe nyumba ya Daudi! Je, haitoshi kujaribu uvumilivu wa wanadamu? Je, mtaujaribu uvumilivu wa Mungu wangu pia?
Et le Seigneur reprit: Écoutez donc, maison de David. Est-ce pour vous si peu de chose que de soutenir une lutte contre des hommes? Et comment soutiendrez-vous une lutte contre Dieu?
14 Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara: Bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, na ataitwa Imanueli.
C'est pourquoi le Seigneur lui-même vous donnera un signe. Voilà que la Vierge concevra dans son sein, et elle enfantera un fils, et tu lui donneras le nom d'Emmanuel.
15 Atakula jibini na asali atakapokuwa ameweza kukataa mabaya na kuchagua mema.
Il mangera du beurre et du miel, avant de savoir discerner le mal ou choisir le bien.
16 Lakini kabla mtoto hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, nchi ya wafalme hao wawili unaowaogopa itafanywa ukiwa.
Aussi même avant de connaître le bien et le mal, cet enfant rejettera le mal, pour choisir le bien. Et cette terre, que tu crains, elle sera abandonnée de la présence de ces deux rois.
17 Bwana ataleta juu yako, juu ya watu wako, na juu ya nyumba ya baba yako wakati ambao haujawahi kuwako tangu Efraimu alipojitenga na Yuda: yeye atawaleteeni mfalme wa Ashuru.”
Et le Seigneur enverra sur toi, et sur ton peuple, et sur la maison de ton père, des jours tels qu'il n'en est point venu depuis le jour où Éphraïm a repoussé de Juda le roi des Assyriens.
18 Katika siku ile Bwana atawapigia filimbi mainzi kutoka vijito vya mbali vya Misri, na nyuki kutoka nchi ya Ashuru.
Et voici ce qui arrivera: en ce jour le Seigneur sifflera pour appeler les mouches qui dominent sur une partie du fleuve d'Égypte, et les abeilles qui sont dans la région d'Assyrie.
19 Wote watakuja na kukaa kwenye mabonde yenye miteremko, na kwenye nyufa za miamba, kwenye vichaka vyote vyenye miiba, na kwenye mashimo yote ya maji.
Et elles viendront toutes dans les vallons de la terre, et dans les creux des rochers, et dans les cavernes, et dans tous les ravins.
20 Katika siku ile Bwana atatumia wembe ulioajiriwa kutoka ngʼambo ya Mto, yaani mfalme wa Ashuru, kunyoa nywele za kichwa chako na malaika ya miguu yako, na kuziondoa ndevu zako pia.
Ce jour-là, avec un rasoir loué sur les rives du fleuve du roi assyrien, le Seigneur rasera la tête de son peuple, et lui ôtera les poils de ses pieds et de sa barbe.
21 Katika siku ile, mtu atahifadhi hai ndama mmoja na kondoo wawili.
Et en ce jour un homme à peine nourrira une vache et deux brebis.
22 Kwa ajili ya wingi wa maziwa watakayotoa, atapata jibini ya kula. Wote watakaobakia katika nchi watakula jibini na asali.
Et, au lieu de boire du lait en abondance, tout homme resté dans la contrée à peine y mangera du beurre et du miel.
23 Katika siku ile, kila mahali palipokuwa na mizabibu elfu moja yenye thamani ya shekeli 1,000 za fedha, patakuwa na michongoma na miiba tu.
Et en ce jour il arrivera que tout lieu où il y aura eu des milliers de vignes, estimées des milliers de sicles, sera aride et couvert de ronces.
24 Watu watakwenda huko wakiwa na upinde na mshale, kwa maana nchi itafunikwa na michongoma na miiba.
On y entrera avec l'arc et la flèche, parce que toute la terre sera aride et couverte de ronces;
25 Kuhusu vilima vyote vilivyokuwa vikilimwa kwa jembe, hamtakwenda huko tena kwa ajili ya hofu ya michongoma na miiba. Patakuwa mahali ambapo ngʼombe wataachiwa huru, na kondoo kukimbia kimbia.
Et toute montagne jadis labourée sera inculte. Et la crainte ne l'envahira plus; car, à cause de son aridité et de ses ronces, ce ne sera plus qu'un pâturage pour les brebis et un passage pour les bœufs.