< Isaya 7 >
1 Wakati Ahazi mwana wa Yothamu, mwana wa Uzia, alipokuwa mfalme wa Yuda, Mfalme Resini wa Aramu, na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli walipanda kupigana dhidi ya Yerusalemu, lakini hawakuweza kuushinda.
and to be in/on/with day Ahaz son: child Jotham son: child Uzziah king Judah to ascend: rise Rezin king Syria and Pekah son: child Remaliah king Israel Jerusalem to/for battle upon her and not be able to/for to fight upon her
2 Wakati huu nyumba ya Daudi iliambiwa, “Aramu wameungana na Efraimu.” Kwa hiyo mioyo ya Ahazi na watu wake ilitikiswa, kama miti ya msituni inavyotikiswa na upepo.
and to tell to/for house: household David to/for to say to rest Syria upon Ephraim and to shake heart his and heart people his like/as to shake tree wood from face: before spirit: breath
3 Ndipo Bwana akamwambia Isaya, “Toka uende, wewe na mwanao Shear-Yashubu, mkutane na Ahazi huko mwisho wa mfereji wa Bwawa la Juu, kwenye barabara iendayo Shamba la Dobi.
and to say LORD to(wards) Isaiah to come out: come please to/for to encounter: meet Ahaz you(m. s.) and Shear-jashub Shear-jashub son: child your to(wards) end conduit [the] pool [the] high to(wards) highway Field (of the Launderer) Washer's
4 Mwambie, ‘Uwe mwangalifu, utulie na usiogope. Usife moyo kwa ajili ya watu hawa wawili walio kama visiki vya kuni vifukavyo moshi, kwa ajili ya hasira kali ya Resini na Aramu na ya mwana wa Remalia.
and to say to(wards) him to keep: careful and to quiet not to fear and heart your not be tender from two tail [the] firebrand [the] smoking [the] these in/on/with burning face: anger Rezin and Syria and son: child Remaliah
5 Aramu, Efraimu na mwana wa Remalia wamepanga shauri baya ili wakuangamize, wakisema,
because for to advise upon you Syria distress: evil Ephraim and son: child Remaliah to/for to say
6 “Tuishambulie Yuda, naam, tuirarue vipande vipande na kuigawa miongoni mwetu, na kumtawaza mwana wa Tabeeli awe mfalme juu yake.”
to ascend: rise in/on/with Judah and to loathe her and to break up/open her to(wards) us and to reign king in/on/with midst her [obj] son: child Tabeal
7 Lakini Bwana Mwenyezi asema hivi: “‘Jambo hili halitatendeka, halitatokea,
thus to say Lord YHWH/God not to arise: establish and not to be
8 kwa kuwa kichwa cha Aramu ni Dameski, na kichwa cha Dameski ni Resini peke yake. Katika muda wa miaka sitini na mitano, Efraimu atakuwa ameharibiwa kiasi kwamba hataweza tena kuwa taifa.
for head: leader Syria Damascus and head: leader Damascus Rezin and in/on/with still sixty and five year to to be dismayed Ephraim from people
9 Kichwa cha Efraimu ni Samaria, na kichwa cha Samaria ni mwana wa Remalia peke yake. Kama hamtasimama thabiti katika imani yenu, hamtaimarika kamwe.’”
and head: leader Ephraim Samaria and head: leader Samaria son: child Remaliah if not be faithful for not be faithful
10 Bwana akasema na Ahazi tena,
and to add: again LORD to speak: speak to(wards) Ahaz to/for to say
11 “Mwombe Bwana Mungu wako ishara, iwe kwenye vina virefu sana, au kwenye vimo virefu sana.” (Sheol )
to ask to/for you sign: miraculous from from with LORD God your be deep hell: Sheol or to exult to/for above [to] (Sheol )
12 Lakini Ahazi akasema, “Sitaomba; sitamjaribu Bwana.”
and to say Ahaz not to ask and not to test [obj] LORD
13 Ndipo Isaya akasema, “Sikia sasa, ewe nyumba ya Daudi! Je, haitoshi kujaribu uvumilivu wa wanadamu? Je, mtaujaribu uvumilivu wa Mungu wangu pia?
and to say to hear: hear please house: household David little from you be weary human for be weary also [obj] God my
14 Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara: Bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, na ataitwa Imanueli.
to/for so to give: give Lord he/she/it to/for you sign: miraculous behold [the] maiden pregnant and to beget son: child and to call: call by name his Immanuel Immanuel
15 Atakula jibini na asali atakapokuwa ameweza kukataa mabaya na kuchagua mema.
curd and honey to eat to/for to know him to reject in/on/with bad: evil and to choose in/on/with good
16 Lakini kabla mtoto hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, nchi ya wafalme hao wawili unaowaogopa itafanywa ukiwa.
for in/on/with before to know [the] youth to reject in/on/with bad: evil and to choose in/on/with good to leave: forsake [the] land: soil which you(m. s.) to loathe from face of two king her
17 Bwana ataleta juu yako, juu ya watu wako, na juu ya nyumba ya baba yako wakati ambao haujawahi kuwako tangu Efraimu alipojitenga na Yuda: yeye atawaleteeni mfalme wa Ashuru.”
to come (in): bring LORD upon you and upon people your and upon house: household father your day which not to come (in): come to/for from day to turn aside: depart Ephraim from upon Judah [obj] king Assyria
18 Katika siku ile Bwana atawapigia filimbi mainzi kutoka vijito vya mbali vya Misri, na nyuki kutoka nchi ya Ashuru.
and to be in/on/with day [the] he/she/it to whistle LORD to/for fly which in/on/with end stream Egypt and to/for bee which in/on/with land: country/planet Assyria
19 Wote watakuja na kukaa kwenye mabonde yenye miteremko, na kwenye nyufa za miamba, kwenye vichaka vyote vyenye miiba, na kwenye mashimo yote ya maji.
and to come (in): come and to rest all their in/on/with torrent: valley [the] precipice and in/on/with cleft [the] crag and in/on/with all [the] thorn bush and in/on/with all [the] watering
20 Katika siku ile Bwana atatumia wembe ulioajiriwa kutoka ngʼambo ya Mto, yaani mfalme wa Ashuru, kunyoa nywele za kichwa chako na malaika ya miguu yako, na kuziondoa ndevu zako pia.
in/on/with day [the] he/she/it to shave Lord in/on/with razor [the] hired in/on/with side: beyond River in/on/with king Assyria [obj] [the] head and hair [the] foot and also [obj] [the] beard to snatch
21 Katika siku ile, mtu atahifadhi hai ndama mmoja na kondoo wawili.
and to be in/on/with day [the] he/she/it to live man heifer cattle and two flock
22 Kwa ajili ya wingi wa maziwa watakayotoa, atapata jibini ya kula. Wote watakaobakia katika nchi watakula jibini na asali.
and to be from abundance to make: offer milk to eat curd for curd and honey to eat all [the] to remain in/on/with entrails: among [the] land: country/planet
23 Katika siku ile, kila mahali palipokuwa na mizabibu elfu moja yenye thamani ya shekeli 1,000 za fedha, patakuwa na michongoma na miiba tu.
and to be in/on/with day [the] he/she/it to be all place which to be there thousand vine in/on/with thousand silver: money to/for thorn and to/for thornbush to be
24 Watu watakwenda huko wakiwa na upinde na mshale, kwa maana nchi itafunikwa na michongoma na miiba.
in/on/with arrow and in/on/with bow to come (in): come there [to] for thorn and thornbush to be all [the] land: country/planet
25 Kuhusu vilima vyote vilivyokuwa vikilimwa kwa jembe, hamtakwenda huko tena kwa ajili ya hofu ya michongoma na miiba. Patakuwa mahali ambapo ngʼombe wataachiwa huru, na kondoo kukimbia kimbia.
and all [the] mountain: mount which in/on/with hoe to hoe [emph?] not to come (in): come there [to] fear thorn and thornbush and to be to/for sending cattle and to/for trampling sheep