< Isaya 66 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana, “Mbingu ni kiti changu cha enzi, nayo dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu. Iko wapi nyumba mtakayoijenga kwa ajili yangu? Mahali pangu pa kupumzikia patakuwa wapi?
Tak mówi PAN: Niebo jest moim tronem, a ziemia podnóżkiem moich stóp. Gdzie więc będzie ten dom, który mi zbudujecie? Gdzie będzie miejsce mego odpoczynku?
2 Je, mkono wangu haukufanya vitu hivi vyote, hivyo vikapata kuwepo?” asema Bwana. “Mtu huyu ndiye ninayemthamini: yeye ambaye ni mnyenyekevu na mwenye roho yenye toba, atetemekaye asikiapo neno langu.
Bo to wszystko moja ręka uczyniła i dzięki niej powstało to wszystko, mówi PAN. Lecz ja patrzę na tego, który jest ubogi i skruszony w duchu i który drży na moje słowo.
3 Lakini yeyote atoaye dhabihu ya fahali ni kama yeye auaye mtu, na yeyote atoaye sadaka ya mwana-kondoo, ni kama yule avunjaye shingo ya mbwa. Yeyote atoaye sadaka ya nafaka, ni kama yule aletaye damu ya nguruwe, na yeyote afukizaye uvumba wa kumbukumbu, ni kama yule aabuduye sanamu. Wamejichagulia njia zao wenyewe, nazo nafsi zao zinafurahia machukizo yao.
Ten, kto zabija wołu [na] ofiarę, to jakby zabił człowieka; kto zabija na ofiarę barana, to jakby ściął psu [głowę]; kto przynosi ofiarę, to jakby ofiarował krew świni; kto pali kadzidło, to jakby błogosławił bożkowi. Lecz jak oni wybrali sobie swoje drogi i ich dusza ma upodobanie w obrzydliwościach;
4 Hivyo, mimi pia nitawachagulia mapigo makali, nami nitaleta juu yao kile wanachokiogopa. Kwa maana nilipoita, hakuna yeyote aliyejibu, niliposema, hakuna yeyote aliyesikiliza. Walifanya maovu machoni pangu na kuchagua lile linalonichukiza.”
Tak i ja wybiorę ich zmyślenia i sprowadzę na nich to, czego się boją, ponieważ gdy wołałem, nikt się nie odezwał, gdy mówiłem, nie słuchali, ale czynili to, co złe w moich oczach, i wybrali to, co mi się nie podobało.
5 Sikieni neno la Bwana, ninyi mtetemekao kwa neno lake: “Ndugu zenu wanaowachukia ninyi na kuwatenga ninyi kwa sababu ya Jina langu, wamesema, ‘Bwana na atukuzwe, ili tupate kuona furaha yenu!’ Hata sasa wataaibika.
Słuchajcie słowa PANA, wy, którzy drżycie na jego słowo. Wasi bracia, którzy was nienawidzą, którzy wypędzają was ze względu na moje imię, mówią: Niech PAN pokaże swoją chwałę. Ukaże się jednak dla waszej radości, a oni będą zawstydzeni.
6 Sikieni hizo ghasia kutoka mjini, sikieni hizo kelele kutoka hekaluni! Ni sauti ya Bwana ikiwalipa adui zake yote wanayostahili.
Odgłos zgiełku z miasta, głos ze świątyni, głos PANA oddającego zapłatę swoim wrogom.
7 “Kabla hajasikia utungu, alizaa; kabla hajapata maumivu, alizaa mtoto mwanaume.
Zanim odczuła bóle porodu, urodziła, zanim ogarnął ją ból, urodziła chłopca.
8 Ni nani amepata kusikia jambo kama hili? Ni nani amepata kuona mambo kama haya? Je, nchi yaweza kuzaliwa kwa siku moja, au taifa laweza kutokea mara? Mara Sayuni alipoona utungu, alizaa watoto wake.
Kto słyszał o czymś takim? Kto widział coś podobnego? Czy ziemia może urodzić w jednym dniu? Czy naród rodzi się od razu? Ale Syjon ledwie zaczął odczuwać bóle, a już urodził swoich synów.
9 Je, nilete mwana hadi wakati wa kuzaliwa na nisizalishe?” asema Bwana. “Je, nifunge tumbo la uzazi wakati mimi ndiye nizalishaye?” asema Mungu wako.
Czyżbym ja, który otwieram łono, nie doprowadził do rodzenia? – mówi PAN. Czyżbym ja, który doprowadzam do rodzenia, zamknął [łono]? – mówi twój Bóg.
10 “Shangilieni pamoja na Yerusalemu na mfurahi kwa ajili yake, ninyi nyote mnaompenda, shangilieni kwa nguvu pamoja naye, ninyi nyote mnaoomboleza juu yake.
Weselcie się z Jerozolimą i radujcie się z nią wszyscy, którzy ją miłujecie. Cieszcie się z nią wielce wszyscy, którzy nad nią płaczecie;
11 Kwa kuwa mtanyonya na kutosheka katika faraja ya matiti yake; mtakunywa sana, na kuufurahia wingi wa mafuriko ya ustawi wake.”
Aby ssać do syta z piersi jej pociech; abyście ssali i rozkoszowali się pełnią jej chwały.
12 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Nitamwongezea amani kama mto, nao utajiri wa mataifa kama kijito kifurikacho; utanyonya na kuchukuliwa mikononi mwake na kubembelezwa magotini pake.
Tak bowiem mówi PAN: Oto skieruję do niej pokój jak rzekę i chwałę narodów jak strumień wezbrany. Wtedy będziecie ssać, będziecie noszeni na rękach i pieszczeni na kolanach.
13 Kama mama anavyomfariji mtoto wake, ndivyo nitakavyokufariji wewe, nawe utafarijiwa huko Yerusalemu.”
Jak tego, którego pociesza matka, tak ja was będę pocieszał; i tak w Jerozolimie doznacie pociechy.
14 Wakati mtakapoona jambo hili, mioyo yenu itashangilia, nanyi mtastawi kama majani; mkono wa Bwana utajulikana kwa watumishi wake, bali ghadhabu yake kali itaonyeshwa kwa adui zake.
Ujrzycie to i rozraduje się wasze serce, a wasze kości zakwitną jak trawa. I będzie rozpoznana ręka PANA wobec jego sług, a jego gniew – wobec jego wrogów.
15 Tazama, Bwana anakuja na moto, magari yake ya vita ni kama upepo wa kisulisuli, atateremsha hasira yake kwa ghadhabu kali, na karipio lake pamoja na miali ya moto.
Oto bowiem PAN przyjdzie w ogniu, a jego rydwany będą jak wicher, by wylać zapalczywość swego gniewu i [ukazać] swoją grozę w płomieniu ognia;
16 Kwa maana kwa moto na kwa upanga wake Bwana atatekeleza hukumu juu ya watu wote, nao wengi watakuwa ni wale waliouawa na Bwana.
Gdyż PAN będzie sądził ogniem i mieczem wszelkie ciało, a wielu będzie pobitych przez PANA.
17 “Watu wote wanaojiweka wakfu na kujitakasa wenyewe ili kwenda bustanini, wakimfuata aliye katikati ya wale ambao hula nyama za nguruwe na panya pamoja na vitu vingine vilivyo machukizo, watafikia mwisho wao pamoja,” asema Bwana.
I ci, którzy się uświęcają i oczyszczają w środku ogrodów, jeden za drugim, którzy jedzą mięso wieprzowe oraz inną obrzydliwość, a także myszy, wszyscy razem zginą – mówi PAN.
18 “Nami, kwa sababu ya matendo yao na mawazo yao, niko karibu kuja na kukusanya mataifa yote na lugha zote, nao watakuja na kuuona utukufu wangu.
Ja znam bowiem ich uczynki i myśli. I przyjdzie czas, że zgromadzę wszystkie narody i języki, a one przyjdą i ujrzą moją chwałę.
19 “Nitaweka ishara katikati yao, nami nitapeleka baadhi ya hao walionusurika kwa mataifa, hadi Tarshishi, kwa Puli na Waludi (wanaojulikana kama wapiga upinde), kwa Tubali na Uyunani, hadi visiwa vya mbali ambavyo havijasikia juu ya sifa zangu au kuuona utukufu wangu. Watatangaza utukufu wangu miongoni mwa mataifa.
I ustanowię wśród nich znak i wyślę ocalałych spośród nich do narodów do Tarszisz, Pul i Lud, a tych, którzy naciągają łuk – do Tubala i Jawan, do wysp dalekich, które nic o mnie nie słyszały i nie widziały mojej chwały; i będą głosić moją chwałę wśród narodów.
20 Nao watawaleta ndugu zenu wote, kutoka mataifa yote, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu katika Yerusalemu kama sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, katika magari ya vita na magari makubwa, juu ya nyumbu na ngamia,” asema Bwana. “Watawaleta, kama Waisraeli waletavyo sadaka zao za nafaka, katika Hekalu la Bwana, katika vyombo safi kwa kufuata desturi za ibada.
I przyprowadzą wszystkich waszych braci jako dar dla PANA ze wszystkich narodów, na koniach, na rydwanach, w lektykach, na mułach i na wielbłądach, na moją świętą górę, do Jerozolimy, mówi PAN, tak jak synowie Izraela przynoszą dar w czystym naczyniu do domu PANA.
21 Nami nitachagua baadhi yao pia wawe makuhani na Walawi,” asema Bwana.
I z nich także wezmę sobie kapłanów i Lewitów, mówi PAN.
22 “Kama vile mbingu mpya na nchi mpya ninazozifanya zitakavyodumu mbele zangu,” asema Bwana, “ndivyo jina lenu na wazao wenu watakavyodumu.
Jak bowiem to nowe niebo i ta nowa ziemia, które ja uczynię, będą trwać przede mną, mówi PAN, tak będzie trwać wasze potomstwo i wasze imię.
23 Kutoka Mwezi Mpya hata mwingine, na kutoka Sabato hadi nyingine, wanadamu wote watakuja na kusujudu mbele zangu,” asema Bwana.
I stanie się tak, że od nowiu do nowiu księżyca i od szabatu do szabatu przychodzić będzie wszelkie ciało, aby oddać pokłon przede mną, mówi PAN.
24 “Nao watatoka nje na kuona maiti za wale walioniasi mimi. Funza wao hawatakufa, wala moto wao hautazimika, nao watakuwa kitu cha kuchukiza sana kwa wanadamu wote.”
I gdy wyjdą, zobaczą trupy ludzi, którzy wystąpili przeciwko mnie. Ich robak bowiem nie zdechnie i ich ogień nie zgaśnie, i będą obrzydliwością dla wszelkiego ciała.

< Isaya 66 >