< Isaya 66 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana, “Mbingu ni kiti changu cha enzi, nayo dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu. Iko wapi nyumba mtakayoijenga kwa ajili yangu? Mahali pangu pa kupumzikia patakuwa wapi?
Yahweh [also] said this: “[All of] heaven is [like] my throne, and the whole earth is [like] my footstool. So you could certainly not [RHQ] build a house [that would be adequate] for me to live in and rest!
2 Je, mkono wangu haukufanya vitu hivi vyote, hivyo vikapata kuwepo?” asema Bwana. “Mtu huyu ndiye ninayemthamini: yeye ambaye ni mnyenyekevu na mwenye roho yenye toba, atetemekaye asikiapo neno langu.
I [MTY] have created everything; all things exist because I made them. [That is true because I], Yahweh, have said it. The people I am [most] pleased with are those who are humble, who [patiently endure it when they] (suffer/are afflicted), and who tremble when they hear me [rebuking them].
3 Lakini yeyote atoaye dhabihu ya fahali ni kama yeye auaye mtu, na yeyote atoaye sadaka ya mwana-kondoo, ni kama yule avunjaye shingo ya mbwa. Yeyote atoaye sadaka ya nafaka, ni kama yule aletaye damu ya nguruwe, na yeyote afukizaye uvumba wa kumbukumbu, ni kama yule aabuduye sanamu. Wamejichagulia njia zao wenyewe, nazo nafsi zao zinafurahia machukizo yao.
You have enjoyed [continually] doing the things that you want to do: [Some of] you slaughter oxen [to sacrifice them to me], but you also bring human sacrifices [to your idols]! You sacrifice lambs [to me], but you kill dogs [to offer them to your gods]. You offer grain to me, but you also bring pigs’ blood [to your idols]. You burn incense [to me], but you also praise your idols. You enjoy doing those disgusting things.
4 Hivyo, mimi pia nitawachagulia mapigo makali, nami nitaleta juu yao kile wanachokiogopa. Kwa maana nilipoita, hakuna yeyote aliyejibu, niliposema, hakuna yeyote aliyesikiliza. Walifanya maovu machoni pangu na kuchagua lile linalonichukiza.”
When I called [out to you], you did not answer. When I spoke, you did not pay attention. You did [many] things that I say are evil; you chose [to do] things that I did not like. So [now] I will punish you by causing you to experience the things that you are [very] afraid of.”
5 Sikieni neno la Bwana, ninyi mtetemekao kwa neno lake: “Ndugu zenu wanaowachukia ninyi na kuwatenga ninyi kwa sababu ya Jina langu, wamesema, ‘Bwana na atukuzwe, ili tupate kuona furaha yenu!’ Hata sasa wataaibika.
But you people who tremble when you hear what Yahweh says, listen to what he says [now]: “Some of your people hate you and reject you because you belong to me. They make fun of you, and they say, ‘Yahweh should show his glorious power! We want to see him [do something to cause] you to be truly happy.’ But [some day] those people will be [very] disgraced.”
6 Sikieni hizo ghasia kutoka mjini, sikieni hizo kelele kutoka hekaluni! Ni sauti ya Bwana ikiwalipa adui zake yote wanayostahili.
[At that time], you will listen to the noise in the city. You will hear the shouting in the temple. It will be the sound of Yahweh shouting while he is punishing his enemies!
7 “Kabla hajasikia utungu, alizaa; kabla hajapata maumivu, alizaa mtoto mwanaume.
No one [RHQ] ever heard that a woman gave birth to a baby when she was just starting to have birth pains.
8 Ni nani amepata kusikia jambo kama hili? Ni nani amepata kuona mambo kama haya? Je, nchi yaweza kuzaliwa kwa siku moja, au taifa laweza kutokea mara? Mara Sayuni alipoona utungu, alizaa watoto wake.
Certainly no one [RHQ] ever heard about such a thing happening, and no one has ever seen it happen. [Similarly], no one ever [RHQ] heard that a nation was created in one instant, not even in one day. But Jerusalem is like [MET] [a woman who] gives birth to children as soon as she starts to have birth pains.
9 Je, nilete mwana hadi wakati wa kuzaliwa na nisizalishe?” asema Bwana. “Je, nifunge tumbo la uzazi wakati mimi ndiye nizalishaye?” asema Mungu wako.
Women certainly do not [RHQ] bring infants to the time when they are ready to be born and then do not allow them to be born. [Similarly, he will do for Jerusalem] [MET] [what he has promised to do]: [He will cause Jerusalem to be full of people again]. [That will happen because] Yahweh has said it.
10 “Shangilieni pamoja na Yerusalemu na mfurahi kwa ajili yake, ninyi nyote mnaompenda, shangilieni kwa nguvu pamoja naye, ninyi nyote mnaoomboleza juu yake.
You people in [APO] Jerusalem, rejoice! And all you people who love Jerusalem should also be happy. You people who were sad because of [what happened to Jerusalem], you should now be glad.
11 Kwa kuwa mtanyonya na kutosheka katika faraja ya matiti yake; mtakunywa sana, na kuufurahia wingi wa mafuriko ya ustawi wake.”
[You people in Jerusalem] will [have everything that you need] like [MET] a baby that gets all it needs from its mother’s breasts. You will enjoy all the abundant and glorious things [MET] in the city.
12 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Nitamwongezea amani kama mto, nao utajiri wa mataifa kama kijito kifurikacho; utanyonya na kuchukuliwa mikononi mwake na kubembelezwa magotini pake.
Yahweh has promised, “I will cause Jerusalem to be full of valuable things that come from other nations; those things will pour into Jerusalem; it will be like [SIM] a big flood. I will take care of the people of Jerusalem like women care for the babies that they nurse.
13 Kama mama anavyomfariji mtoto wake, ndivyo nitakavyokufariji wewe, nawe utafarijiwa huko Yerusalemu.”
I will comfort you people in Jerusalem like [MET] mothers comfort their children.”
14 Wakati mtakapoona jambo hili, mioyo yenu itashangilia, nanyi mtastawi kama majani; mkono wa Bwana utajulikana kwa watumishi wake, bali ghadhabu yake kali itaonyeshwa kwa adui zake.
When you see [those things happen], you [SYN] will rejoice. Your [old] bones will become strong [again] like [SIM] grass [that grows quickly/well in the springtime]. [When that happens, everyone] will know that Yahweh has power [MTY] to help those who worship and obey him, but that he is angry with his enemies.
15 Tazama, Bwana anakuja na moto, magari yake ya vita ni kama upepo wa kisulisuli, atateremsha hasira yake kwa ghadhabu kali, na karipio lake pamoja na miali ya moto.
Yahweh will come down with flames of fire, and his chariots [will come down] like [SIM] a whirlwind; he will be extremely angry, and he will punish [his enemies] by burning them in a fire.
16 Kwa maana kwa moto na kwa upanga wake Bwana atatekeleza hukumu juu ya watu wote, nao wengi watakuwa ni wale waliouawa na Bwana.
[It is as though] [MET] Yahweh has a [big] sword, and he will judge and execute many people.
17 “Watu wote wanaojiweka wakfu na kujitakasa wenyewe ili kwenda bustanini, wakimfuata aliye katikati ya wale ambao hula nyama za nguruwe na panya pamoja na vitu vingine vilivyo machukizo, watafikia mwisho wao pamoja,” asema Bwana.
Yahweh says, “Some of you people purify/bathe yourselves and [then] go to a garden to worship your gods. You eat the meat of pigs and lizards and mice, [and other things that I have forbidden you to eat]. So I will get rid of you [for doing that].
18 “Nami, kwa sababu ya matendo yao na mawazo yao, niko karibu kuja na kukusanya mataifa yote na lugha zote, nao watakuja na kuuona utukufu wangu.
I know [all] the [evil] things that you think and do. [It is now time] for me to gather together the people who live in all nations and who speak all languages, and to show them that I am very great.
19 “Nitaweka ishara katikati yao, nami nitapeleka baadhi ya hao walionusurika kwa mataifa, hadi Tarshishi, kwa Puli na Waludi (wanaojulikana kama wapiga upinde), kwa Tubali na Uyunani, hadi visiwa vya mbali ambavyo havijasikia juu ya sifa zangu au kuuona utukufu wangu. Watatangaza utukufu wangu miongoni mwa mataifa.
I will put a mark on them, and those whom I have spared will go to various [distant] countries: to Tarshish, Put, Lud, Meshech, Tubal, Javan, and to distant islands. I will send them to proclaim to nations that have never heard about me that I am very great and glorious.
20 Nao watawaleta ndugu zenu wote, kutoka mataifa yote, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu katika Yerusalemu kama sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, katika magari ya vita na magari makubwa, juu ya nyumbu na ngamia,” asema Bwana. “Watawaleta, kama Waisraeli waletavyo sadaka zao za nafaka, katika Hekalu la Bwana, katika vyombo safi kwa kufuata desturi za ibada.
Then they will bring back here your relatives [who have been (exiled/forced to go to other countries)], to be like [SIM] an offering to me. They will come on horses, in chariots, on mules, and on camels. They will come to [Zion, ] my sacred hill in Jerusalem. That will be like [SIM] the offerings that [my] Israeli people used to bring in the correct manner to the temple.
21 Nami nitachagua baadhi yao pia wawe makuhani na Walawi,” asema Bwana.
[I solemnly promise that] I will appoint some of them to be priests, and others to do other work in my temple. [That will surely happen because I], Yahweh, have said it.
22 “Kama vile mbingu mpya na nchi mpya ninazozifanya zitakavyodumu mbele zangu,” asema Bwana, “ndivyo jina lenu na wazao wenu watakavyodumu.
I [also] promise that just like the new heaven and the new earth will last forever, you will always have descendants, and you [MTY] will always be honored.
23 Kutoka Mwezi Mpya hata mwingine, na kutoka Sabato hadi nyingine, wanadamu wote watakuja na kusujudu mbele zangu,” asema Bwana.
At every festival to celebrate the Sabbath [each week] and the new moon [each month], everyone will [come and] worship me. [That will surely happen because] I, Yahweh, have said it.
24 “Nao watatoka nje na kuona maiti za wale walioniasi mimi. Funza wao hawatakufa, wala moto wao hautazimika, nao watakuwa kitu cha kuchukiza sana kwa wanadamu wote.”
Then they will go out [of Jerusalem] and look at the corpses of those who rebelled against me. The maggots in those corpses will never die, the fire will never stop burning them, and everyone [who sees their corpses] will detest them.”

< Isaya 66 >