< Isaya 66 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana, “Mbingu ni kiti changu cha enzi, nayo dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu. Iko wapi nyumba mtakayoijenga kwa ajili yangu? Mahali pangu pa kupumzikia patakuwa wapi?
thus to say LORD [the] heaven throne my and [the] land: country/planet footstool foot my where? this house: temple which to build to/for me and where? this place resting my
2 Je, mkono wangu haukufanya vitu hivi vyote, hivyo vikapata kuwepo?” asema Bwana. “Mtu huyu ndiye ninayemthamini: yeye ambaye ni mnyenyekevu na mwenye roho yenye toba, atetemekaye asikiapo neno langu.
and [obj] all these hand my to make and to be all these utterance LORD and to(wards) this to look to(wards) afflicted and crippled spirit and trembling upon word my
3 Lakini yeyote atoaye dhabihu ya fahali ni kama yeye auaye mtu, na yeyote atoaye sadaka ya mwana-kondoo, ni kama yule avunjaye shingo ya mbwa. Yeyote atoaye sadaka ya nafaka, ni kama yule aletaye damu ya nguruwe, na yeyote afukizaye uvumba wa kumbukumbu, ni kama yule aabuduye sanamu. Wamejichagulia njia zao wenyewe, nazo nafsi zao zinafurahia machukizo yao.
to slaughter [the] cattle to smite man to sacrifice [the] sheep to break the neck dog to ascend: offer up offering blood swine to remember frankincense to bless evil: wickedness also they(masc.) to choose in/on/with way: conduct their and in/on/with abomination their soul their to delight in
4 Hivyo, mimi pia nitawachagulia mapigo makali, nami nitaleta juu yao kile wanachokiogopa. Kwa maana nilipoita, hakuna yeyote aliyejibu, niliposema, hakuna yeyote aliyesikiliza. Walifanya maovu machoni pangu na kuchagua lile linalonichukiza.”
also I to choose in/on/with caprice their and fear their to come (in): bring to/for them because to call: call to and nothing to answer to speak: speak and not to hear: hear and to make: do [the] bad: evil in/on/with eye my and in/on/with in which not to delight in to choose
5 Sikieni neno la Bwana, ninyi mtetemekao kwa neno lake: “Ndugu zenu wanaowachukia ninyi na kuwatenga ninyi kwa sababu ya Jina langu, wamesema, ‘Bwana na atukuzwe, ili tupate kuona furaha yenu!’ Hata sasa wataaibika.
to hear: hear word LORD [the] trembling to(wards) word his to say brother: male-sibling your to hate you to put away you because name my to honor: honour LORD and to see: see in/on/with joy your and they(masc.) be ashamed
6 Sikieni hizo ghasia kutoka mjini, sikieni hizo kelele kutoka hekaluni! Ni sauti ya Bwana ikiwalipa adui zake yote wanayostahili.
voice: sound roar from city voice: sound from temple voice: sound LORD to complete recompense to/for enemy his
7 “Kabla hajasikia utungu, alizaa; kabla hajapata maumivu, alizaa mtoto mwanaume.
in/on/with before to twist: writh in pain to beget in/on/with before to come (in): come pain to/for her and to escape male
8 Ni nani amepata kusikia jambo kama hili? Ni nani amepata kuona mambo kama haya? Je, nchi yaweza kuzaliwa kwa siku moja, au taifa laweza kutokea mara? Mara Sayuni alipoona utungu, alizaa watoto wake.
who? to hear: hear like/as this who? to see: see like/as these to twist: writh in pain land: country/planet in/on/with day one if: surely no to beget nation beat one for to twist: writh in pain also to beget Zion [obj] son: child her
9 Je, nilete mwana hadi wakati wa kuzaliwa na nisizalishe?” asema Bwana. “Je, nifunge tumbo la uzazi wakati mimi ndiye nizalishaye?” asema Mungu wako.
I to break and not to beget to say LORD if: surely no I [the] to beget and to restrain to say God your
10 “Shangilieni pamoja na Yerusalemu na mfurahi kwa ajili yake, ninyi nyote mnaompenda, shangilieni kwa nguvu pamoja naye, ninyi nyote mnaoomboleza juu yake.
to rejoice with Jerusalem and to rejoice in/on/with her all to love: lover her to rejoice with her rejoicing all [the] to mourn upon her
11 Kwa kuwa mtanyonya na kutosheka katika faraja ya matiti yake; mtakunywa sana, na kuufurahia wingi wa mafuriko ya ustawi wake.”
because to suckle and to satisfy from breast consolation her because to drink deeply and to delight from abundance glory her
12 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Nitamwongezea amani kama mto, nao utajiri wa mataifa kama kijito kifurikacho; utanyonya na kuchukuliwa mikononi mwake na kubembelezwa magotini pake.
for thus to say LORD look! I to stretch to(wards) her like/as river peace and like/as torrent: river to overflow glory nation and to suckle upon side to lift: bear and upon knee to delight
13 Kama mama anavyomfariji mtoto wake, ndivyo nitakavyokufariji wewe, nawe utafarijiwa huko Yerusalemu.”
like/as man which mother his to be sorry: comfort him so I to be sorry: comfort you and in/on/with Jerusalem to be sorry: comfort
14 Wakati mtakapoona jambo hili, mioyo yenu itashangilia, nanyi mtastawi kama majani; mkono wa Bwana utajulikana kwa watumishi wake, bali ghadhabu yake kali itaonyeshwa kwa adui zake.
and to see: see and to rejoice heart your and bone your like/as grass to sprout and to know hand: power LORD with servant/slave his and be indignant [obj] enemy his
15 Tazama, Bwana anakuja na moto, magari yake ya vita ni kama upepo wa kisulisuli, atateremsha hasira yake kwa ghadhabu kali, na karipio lake pamoja na miali ya moto.
for behold LORD in/on/with fire to come (in): come and like/as whirlwind chariot his to/for to return: turn back in/on/with rage face: anger his and rebuke his in/on/with flame fire
16 Kwa maana kwa moto na kwa upanga wake Bwana atatekeleza hukumu juu ya watu wote, nao wengi watakuwa ni wale waliouawa na Bwana.
for in/on/with fire LORD to judge and in/on/with sword his with all flesh and to multiply slain: killed LORD
17 “Watu wote wanaojiweka wakfu na kujitakasa wenyewe ili kwenda bustanini, wakimfuata aliye katikati ya wale ambao hula nyama za nguruwe na panya pamoja na vitu vingine vilivyo machukizo, watafikia mwisho wao pamoja,” asema Bwana.
[the] to consecrate: consecate and [the] be pure to(wards) [the] garden after (one *Q(K)*) in/on/with midst to eat flesh [the] swine and [the] detestation and [the] mouse together to cease utterance LORD
18 “Nami, kwa sababu ya matendo yao na mawazo yao, niko karibu kuja na kukusanya mataifa yote na lugha zote, nao watakuja na kuuona utukufu wangu.
and I deed their and plot their to come (in): come to/for to gather [obj] all [the] nation and [the] tongue: language and to come (in): come and to see: see [obj] glory my
19 “Nitaweka ishara katikati yao, nami nitapeleka baadhi ya hao walionusurika kwa mataifa, hadi Tarshishi, kwa Puli na Waludi (wanaojulikana kama wapiga upinde), kwa Tubali na Uyunani, hadi visiwa vya mbali ambavyo havijasikia juu ya sifa zangu au kuuona utukufu wangu. Watatangaza utukufu wangu miongoni mwa mataifa.
and to set: make in/on/with them sign: indicator and to send: depart from them survivor to(wards) [the] nation Tarshish Pul and Lud to draw bow Tubal and Greece [the] coastland [the] distant which not to hear: hear [obj] report my and not to see: see [obj] glory my and to tell [obj] glory my in/on/with Gentile
20 Nao watawaleta ndugu zenu wote, kutoka mataifa yote, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu katika Yerusalemu kama sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, katika magari ya vita na magari makubwa, juu ya nyumbu na ngamia,” asema Bwana. “Watawaleta, kama Waisraeli waletavyo sadaka zao za nafaka, katika Hekalu la Bwana, katika vyombo safi kwa kufuata desturi za ibada.
and to come (in): bring [obj] all brother: compatriot your from all [the] nation offering to/for LORD in/on/with horse and in/on/with chariot and in/on/with litter and in/on/with mule and in/on/with dromedary upon mountain: mount holiness my Jerusalem to say LORD like/as as which to come (in): bring son: descendant/people Israel [obj] [the] offering in/on/with article/utensil pure house: temple LORD
21 Nami nitachagua baadhi yao pia wawe makuhani na Walawi,” asema Bwana.
and also from them to take: take to/for priest to/for Levi to say LORD
22 “Kama vile mbingu mpya na nchi mpya ninazozifanya zitakavyodumu mbele zangu,” asema Bwana, “ndivyo jina lenu na wazao wenu watakavyodumu.
for like/as as which [the] heaven [the] new and [the] land: country/planet [the] new which I to make to stand: stand to/for face: before my utterance LORD so to stand: stand seed: children your and name your
23 Kutoka Mwezi Mpya hata mwingine, na kutoka Sabato hadi nyingine, wanadamu wote watakuja na kusujudu mbele zangu,” asema Bwana.
and to be from sufficiency month: new moon in/on/with month: new moon his and from sufficiency Sabbath in/on/with Sabbath his to come (in): come all flesh to/for to bow to/for face: before my to say LORD
24 “Nao watatoka nje na kuona maiti za wale walioniasi mimi. Funza wao hawatakufa, wala moto wao hautazimika, nao watakuwa kitu cha kuchukiza sana kwa wanadamu wote.”
and to come out: come and to see: see in/on/with corpse [the] human [the] to transgress in/on/with me for worm their not to die and fire their not to quench and to be abhorrence to/for all flesh

< Isaya 66 >