< Isaya 66 >
1 Hili ndilo asemalo Bwana, “Mbingu ni kiti changu cha enzi, nayo dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu. Iko wapi nyumba mtakayoijenga kwa ajili yangu? Mahali pangu pa kupumzikia patakuwa wapi?
Takto praví Hospodin: Nebe jest mi stolice, a země podnože noh mých. Kdež ten dům bude, kterýž mi vzděláte? Aneb kde bude místo odpočívání mého?
2 Je, mkono wangu haukufanya vitu hivi vyote, hivyo vikapata kuwepo?” asema Bwana. “Mtu huyu ndiye ninayemthamini: yeye ambaye ni mnyenyekevu na mwenye roho yenye toba, atetemekaye asikiapo neno langu.
Nebo všecko to ruka má učinila, a jí stojí všecko, praví Hospodin. I však na toho patřím, kdož jest chudý a skroušeného ducha, a třese se před slovem mým.
3 Lakini yeyote atoaye dhabihu ya fahali ni kama yeye auaye mtu, na yeyote atoaye sadaka ya mwana-kondoo, ni kama yule avunjaye shingo ya mbwa. Yeyote atoaye sadaka ya nafaka, ni kama yule aletaye damu ya nguruwe, na yeyote afukizaye uvumba wa kumbukumbu, ni kama yule aabuduye sanamu. Wamejichagulia njia zao wenyewe, nazo nafsi zao zinafurahia machukizo yao.
Sic jinak ten, kdož zabijí vola, zabil člověka; kdo zabijí hovádko, psa sťal; kdo obětuje obět suchou, krev sviňskou obětoval; kdo kadí kadidlem, dary dával modle. To oni vyvolili na cestách svých, proto že, v ohavnostech svých duše jejich se kochá.
4 Hivyo, mimi pia nitawachagulia mapigo makali, nami nitaleta juu yao kile wanachokiogopa. Kwa maana nilipoita, hakuna yeyote aliyejibu, niliposema, hakuna yeyote aliyesikiliza. Walifanya maovu machoni pangu na kuchagua lile linalonichukiza.”
I jáť také vyvolím za nešlechetnosti jejich, a to, čehož se strachují, na ně uvedu, proto že, když jsem volal, žádný se neohlásil, když jsem mluvil, neslyšeli, ale činili to, což zlého jest před očima mýma, a to, čehož neoblibuji, vyvolili.
5 Sikieni neno la Bwana, ninyi mtetemekao kwa neno lake: “Ndugu zenu wanaowachukia ninyi na kuwatenga ninyi kwa sababu ya Jina langu, wamesema, ‘Bwana na atukuzwe, ili tupate kuona furaha yenu!’ Hata sasa wataaibika.
Slyšte slovo Hospodinovo, kteříž se třesete před slovem jeho: Říkávají bratří vaši, v nenávisti majíce vás, a vypovídajíce vás pro jméno mé: Nechť se zjeví sláva Hospodinova. Ukážeť se zajisté ku potěšení vašemu, ale oni zahanbeni budou.
6 Sikieni hizo ghasia kutoka mjini, sikieni hizo kelele kutoka hekaluni! Ni sauti ya Bwana ikiwalipa adui zake yote wanayostahili.
Hlas hřmotu z města, hlas z chrámu, hlas Hospodinův, an odplatu dává nepřátelům svým.
7 “Kabla hajasikia utungu, alizaa; kabla hajapata maumivu, alizaa mtoto mwanaume.
Prvé než pracovala ku porodu, porodila; prvé než přišla na ni bolest, porodila pacholátko.
8 Ni nani amepata kusikia jambo kama hili? Ni nani amepata kuona mambo kama haya? Je, nchi yaweza kuzaliwa kwa siku moja, au taifa laweza kutokea mara? Mara Sayuni alipoona utungu, alizaa watoto wake.
Kdo slýchal co takového? Kdo vídal co podobného? Zdaliž může způsobeno býti, aby země zplodila lid dne jednoho? Zdaliž zplozen bývá národ pojednou? Ale Sion jen počal pracovati ku porodu, a porodil syny své.
9 Je, nilete mwana hadi wakati wa kuzaliwa na nisizalishe?” asema Bwana. “Je, nifunge tumbo la uzazi wakati mimi ndiye nizalishaye?” asema Mungu wako.
Což bych já, kterýž otvírám život matky, neplodil? praví Hospodin. Což bych já, kterýž činím to, aby rodily, zavřín byl? praví Bůh tvůj.
10 “Shangilieni pamoja na Yerusalemu na mfurahi kwa ajili yake, ninyi nyote mnaompenda, shangilieni kwa nguvu pamoja naye, ninyi nyote mnaoomboleza juu yake.
Veselte se s Jeruzalémem, a plésejte v něm všickni, kteříž jej milujete. Radujte se s ním velice, kteříž jste koli kvílili nad ním,
11 Kwa kuwa mtanyonya na kutosheka katika faraja ya matiti yake; mtakunywa sana, na kuufurahia wingi wa mafuriko ya ustawi wake.”
Proto že ssáti budete, a sytiti se z prs potěšení jeho, ssáti budete, a rozkoš míti v blesku slávy jeho.
12 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Nitamwongezea amani kama mto, nao utajiri wa mataifa kama kijito kifurikacho; utanyonya na kuchukuliwa mikononi mwake na kubembelezwa magotini pake.
Nebo takto praví Hospodin: Aj, já obrátím na něj jako řeku pokoj, a jako potok rozvodnilý slávu národů. I budete ssáti, na rukou pěstováni a na klíně rozkošně chováni budete.
13 Kama mama anavyomfariji mtoto wake, ndivyo nitakavyokufariji wewe, nawe utafarijiwa huko Yerusalemu.”
Jako ten, kteréhož matka jeho těší, tak já vás těšiti budu, a tak v Jeruzalémě potěšováni budete.
14 Wakati mtakapoona jambo hili, mioyo yenu itashangilia, nanyi mtastawi kama majani; mkono wa Bwana utajulikana kwa watumishi wake, bali ghadhabu yake kali itaonyeshwa kwa adui zake.
Uzříte zajisté, a radovati se bude srdce vaše, a kosti vaše jako bylinka zkvetnou. I seznána bude ruka Hospodinova při služebnících jeho, a prchlivost proti nepřátelům jeho.
15 Tazama, Bwana anakuja na moto, magari yake ya vita ni kama upepo wa kisulisuli, atateremsha hasira yake kwa ghadhabu kali, na karipio lake pamoja na miali ya moto.
Nebo aj, Hospodin v ohni přijde, a jako vichřice budou vozové jeho, aby vypustil v prchlivosti hněv svůj, a žehrání své v plameni ohně.
16 Kwa maana kwa moto na kwa upanga wake Bwana atatekeleza hukumu juu ya watu wote, nao wengi watakuwa ni wale waliouawa na Bwana.
Hospodin, pravím, ohněm mstíti bude, a mečem svým nad všelikým tělem, tak že mnoho bude zbitých od Hospodina.
17 “Watu wote wanaojiweka wakfu na kujitakasa wenyewe ili kwenda bustanini, wakimfuata aliye katikati ya wale ambao hula nyama za nguruwe na panya pamoja na vitu vingine vilivyo machukizo, watafikia mwisho wao pamoja,” asema Bwana.
I ti, kteříž se posvěcují a očišťují v zahradách, jeden po druhém zjevně, kteříž jedí maso sviňské, a věc ohavnou i myši, též konec vezmou, praví Hospodin.
18 “Nami, kwa sababu ya matendo yao na mawazo yao, niko karibu kuja na kukusanya mataifa yote na lugha zote, nao watakuja na kuuona utukufu wangu.
Nebo já, když skutkové a myšlení jejich přijdou, shromáždím všecky národy a jazyky. I přijdou, a uzří slávu mou.
19 “Nitaweka ishara katikati yao, nami nitapeleka baadhi ya hao walionusurika kwa mataifa, hadi Tarshishi, kwa Puli na Waludi (wanaojulikana kama wapiga upinde), kwa Tubali na Uyunani, hadi visiwa vya mbali ambavyo havijasikia juu ya sifa zangu au kuuona utukufu wangu. Watatangaza utukufu wangu miongoni mwa mataifa.
A položím na ně znamení, a pošli z nich, kteříž zachováni budou, k národům do Tarsu, Pul a Lud, jenž natahují lučiště, do Tubal a Javan, na ostrovy daleké, kteříž neslýchali pověsti o mně, aniž vídali slávy mé. I budou zvěstovati slávu mou mezi národy.
20 Nao watawaleta ndugu zenu wote, kutoka mataifa yote, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu katika Yerusalemu kama sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, katika magari ya vita na magari makubwa, juu ya nyumbu na ngamia,” asema Bwana. “Watawaleta, kama Waisraeli waletavyo sadaka zao za nafaka, katika Hekalu la Bwana, katika vyombo safi kwa kufuata desturi za ibada.
A přivedou všecky bratří vaše ze všech národů za dar Hospodinu, na koních a na vozích, a na nůších a na mezcích, a na dromedářích, na horu svatosti mé do Jeruzaléma, praví Hospodin, tak jako přinášejí synové Izraelští dar v nádobě čisté do domu Hospodinova.
21 Nami nitachagua baadhi yao pia wawe makuhani na Walawi,” asema Bwana.
A z těchť také vezmu za kněží a za Levíty, praví Hospodin.
22 “Kama vile mbingu mpya na nchi mpya ninazozifanya zitakavyodumu mbele zangu,” asema Bwana, “ndivyo jina lenu na wazao wenu watakavyodumu.
Nebo jakož ta nebesa nová, a země ta nová, kterouž já učiním, stane přede mnou, praví Hospodin, tak stane símě vaše a jméno vaše.
23 Kutoka Mwezi Mpya hata mwingine, na kutoka Sabato hadi nyingine, wanadamu wote watakuja na kusujudu mbele zangu,” asema Bwana.
I stane se, že od novměsíce do novměsíce, od soboty do soboty přicházeti bude všeliké tělo, aby se klanělo přede mnou, praví Hospodin.
24 “Nao watatoka nje na kuona maiti za wale walioniasi mimi. Funza wao hawatakufa, wala moto wao hautazimika, nao watakuwa kitu cha kuchukiza sana kwa wanadamu wote.”
A vyjdouce, uzří těla mrtvá lidí těch, kteříž se mi zpronevěřili; nebo červ jejich neumře, a oheň jejich neuhasne. I budouť v ošklivosti všelikému tělu.