< Isaya 65 >

1 “Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia. Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu, nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’
Potražiše me koji ne pitahu za me; naðoše me koji me ne tražahu; rekoh narodu koji se ne zove mojim imenom: evo me, evo me.
2 Mchana kutwa nimeinyoosha mikono yangu kwa watu wakaidi, wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri, wafuatao mawazo yao wenyewe:
Vas dan pružah ruke svoje narodu nepokornu, koji ide za svojim mislima putem koji nije dobar,
3 taifa ambalo daima hunikasirisha machoni pangu, wakitoa dhabihu katika bustani na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;
Narodu, koji me jednako gnjevi u oèi, koji prinosi žrtve u vrtovima i kadi na opekama;
4 watu waketio katikati ya makaburi na kukesha mahali pa siri, walao nyama za nguruwe, nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,
Koji sjede kod grobova i noæuju u peæinama, jedu meso svinjeæe i juha im je neèista u sudovima;
5 wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie, kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’ Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu, ni moto uwakao mchana kutwa.
Koji govore: odlazi, ne dohvataj me se, jer sam svetiji od tebe. Ti su dim u nozdrvama mojim, oganj koji gori vas dan.
6 “Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu: sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu; nitalipiza mapajani mwao:
Eto, napisano je preda mnom: neæu muèati, nego æu platiti, platiæu im u njedra.
7 dhambi zenu na dhambi za baba zenu,” asema Bwana. “Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima na kunichokoza mimi juu ya vilima, nitawapimia mapajani mwao malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”
Za bezakonja vaša i za bezakonja otaca vaših, veli Gospod, koji kadiše na gorama, i na humovima ružiše me, izmjeriæu im u njedra platu za djela koja èiniše od poèetka.
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana katika kishada cha zabibu, nao watu husema, ‘Usikiharibu, kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’ hivyo ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.
Ovako veli Gospod: kao kad ko naðe vina u grozdu, pa reèe: ne kvari ga, jer je blagoslov u njemu, tako æu uèiniti radi sluga svojih, neæu ih potrti svijeh,
9 Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo, na kutoka kwa Yuda wale watakaomiliki milima yangu, nao watu wangu wateule watairithi, nako huko wataishi watumishi wangu.
Jer æu izvesti sjeme iz Jakova i iz Jude našljednika gorama svojim, i naslijediæe ih izbranici moji, i sluge moje naseliæe se ondje.
10 Sharoni itakuwa malisho kwa ajili ya makundi ya kondoo, na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia kwa makundi ya ngʼombe, kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.
A Saron æe biti tor za ovce i dolina Ahorska poèivalište za goveda narodu mojemu koji me traži.
11 “Bali kwenu ninyi mnaomwacha Bwana na kuusahau mlima wangu mtakatifu, ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati, na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa kwa ajili ya Ajali,
A vi, koji ostavljate Gospoda, koji zaboravljate svetu goru moju, koji postavljate sto Gadu i ljevate naljev Meniju,
12 nitawaagiza mfe kwa upanga, nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa; kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika, nilisema lakini hamkusikiliza. Mlitenda maovu machoni pangu, nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”
Vas æu izbrojiti pod maè, i svi æete pripasti na klanje, jer zvah a vi se ne odzivaste, govorih a vi ne slušaste, nego èiniste što je zlo preda mnom i izabraste što meni nije po volji.
13 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mtaona njaa; watumishi wangu watakunywa lakini ninyi mtaona kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mtaona haya.
Zato ovako veli Gospod Gospod: gle, sluge æe moje jesti, a vi æete gladovati; gle, sluge æe moje piti, a vi æete biti žedni; gle, sluge æe se moje veseliti, a vi æete se stidjeti.
14 Watumishi wangu wataimba kwa furaha ya mioyo yao, lakini ninyi mtalia kutokana na uchungu wa moyoni, na kupiga yowe kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.
Gle, sluge æe moje pjevati od radosti u srcu, a vi æete vikati od žalosti u srcu i ridaæete od tuge u duhu.
15 Mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa; Bwana Mwenyezi atawaua ninyi, lakini watumishi wake atawapa jina jingine.
I ostaviæete ime svoje izbranima mojim za uklin; i Gospod æe te Bog ubiti, a sluge æe svoje nazvati drugim imenom.
16 Yeye aombaye baraka katika nchi atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli; yeye aapaye katika nchi ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika na kufichwa kutoka machoni pangu.
Ko se uzblagosilja na zemlji, blagosiljaæe se Bogom istinijem; a ko se uskune na zemlji, kleæe se Bogom istinijem; jer æe se prve nevolje zaboraviti i sakrivene æe biti od oèiju mojih.
17 “Tazama, nitaumba mbingu mpya na dunia mpya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayatakuja akilini.
Jer, gle, ja æu stvoriti nova nebesa i novu zemlju, i što je prije bilo neæe se pominjati niti æe na um dolaziti.
18 Lakini furahini na kushangilia daima katika hivi nitakavyoumba, kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza, nao watu wake wawe furaha.
Nego se radujte i veselite se dovijeka radi onoga što æu ja stvoriti; jer gle, ja æu stvoriti Jerusalim da bude veselje i narod njegov da bude radost.
19 Nami nitaifurahia Yerusalemu na kuwafurahia watu wangu; sauti ya maombolezo na ya kilio haitasikika humo tena.
I ja æu se veseliti radi Jerusalima, i radovaæu se radi naroda svojega, i neæe se više èuti u njemu plaè ni jauk.
20 “Kamwe hatakuwepo tena ndani yake mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu, au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake. Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja atahesabiwa kwamba ni kijana tu, yeye ambaye hatafika miaka mia moja, atahesabiwa kuwa amelaaniwa.
Neæe više biti ondje maloga djeteta ni starca koji ne bi navršio dana svojih; jer æe dijete umirati od sto godina, a grješnik od sto godina biæe proklet.
21 Watajenga nyumba na kuishi ndani yake; watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.
I oni æe graditi kuæe i sjedjeæe u njima; i sadiæe vinograde i ješæe rod njihov.
22 Hawatajenga nyumba, nao watu wengine waishi ndani yake, au kupanda mazao na wengine wale. Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti, ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi kazi za mikono yao.
Neæe oni graditi a drugi se naseliti, neæe saditi a drugi jesti, jer æe dani narodu mojemu biti kao dani drvetu, i izbranicima æe mojim ovetšati djela ruku njihovijeh.
23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga, kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa na Bwana, wao na wazao wao pamoja nao.
Neæe raditi uzalud, niti æe raðati za strah, jer æe biti sjeme blagoslovenijeh od Gospoda, i natražje æe njihovo biti s njima.
24 Kabla hawajaita, nitajibu, nao wakiwa katika kunena, nitasikia.
I prije nego povièu, ja æu se odazvati; još æe govoriti, a ja æu uslišiti.
25 Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, naye simba atakula nyasi kama maksai, lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote,” asema Bwana.
Vuk i jagnje zajedno æe pasti, i lav æe jesti slamu kao vo; a zmiji æe biti hrana prah; neæe uditi ni potirati na svoj svetoj gori mojoj, veli Gospod.

< Isaya 65 >