< Isaya 65 >
1 “Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia. Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu, nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’
Objawiłem się tym, którzy się o mię nie pytali; znalezionym jest od tych, którzy mię nie szukali; do narodu, który się nie nazywał imieniem mojem. rzekłem: Otom Ja! otom Ja!
2 Mchana kutwa nimeinyoosha mikono yangu kwa watu wakaidi, wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri, wafuatao mawazo yao wenyewe:
Rozciągnąłem ręce moje na każdy dzień do ludu upornego, który chodzi drogą nie dobrą za myślami swemi;
3 taifa ambalo daima hunikasirisha machoni pangu, wakitoa dhabihu katika bustani na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;
Do ludu, który mię jawnie wzrusza do gniewu, ustawicznie ofiarując w ogrodach, a kadząc na cegłach;
4 watu waketio katikati ya makaburi na kukesha mahali pa siri, walao nyama za nguruwe, nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,
Którzy siadają przy grobach, a przy bałwanach swoich nocują; którzy jedzą świnie mięso, i polewkę obrzydłą z naczynia swego.
5 wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie, kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’ Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu, ni moto uwakao mchana kutwa.
Mówiąc: Odstąp precz, nie przystępuj do mnie; bom jest świętobliwszy niżeli ty. Cić są dymem w nozdrzach moich, i ogniem pałającym przez cały dzień.
6 “Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu: sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu; nitalipiza mapajani mwao:
Oto zapisano to przedemną: Nie zamilczę, ale oddam i odpłacę na łono ich.
7 dhambi zenu na dhambi za baba zenu,” asema Bwana. “Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima na kunichokoza mimi juu ya vilima, nitawapimia mapajani mwao malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”
Nieprawości wasze, także i nieprawości ojców waszych, mówi Pan, którzy kadzili po górach, a na pagórkach hańbili mię; przetoż odmierzę sprawę ich pierwszą na łono ich.
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana katika kishada cha zabibu, nao watu husema, ‘Usikiharibu, kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’ hivyo ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.
Tak mówi Pan: Jako gdyby kto znalazł wino w gronie, i rzekłby: Nie psuj go, bo błogosławieństwo jest w niem; tak i Ja uczynię dla sług moich, że ich wszystkich nie wygubię.
9 Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo, na kutoka kwa Yuda wale watakaomiliki milima yangu, nao watu wangu wateule watairithi, nako huko wataishi watumishi wangu.
Bo wywiodę z Jakóba nasienie, a z Judy dzierżawcę gór moich; i posiędą ją wybrani moi, a słudzy moi tam mieszkać będą.
10 Sharoni itakuwa malisho kwa ajili ya makundi ya kondoo, na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia kwa makundi ya ngʼombe, kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.
A Saron będzie za pastwisko owcom, a dolina Achor za legowisko wołów ludu mojego, którzy mię szukali.
11 “Bali kwenu ninyi mnaomwacha Bwana na kuusahau mlima wangu mtakatifu, ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati, na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa kwa ajili ya Ajali,
Ale was, którzyście opuścili Pana, którzy zapominacie na górę świętobliwości mojej, którzy gotujecie temu wojsku stół, a którzy oddawacie temu pocztowi mokre ofiary:
12 nitawaagiza mfe kwa upanga, nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa; kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika, nilisema lakini hamkusikiliza. Mlitenda maovu machoni pangu, nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”
Was, mówię policzę pod miecz, tak, że wy wszyscy do zabicia schylać się będziecie, przeto, żem wołał, a nie ozwaliście mi się, mówiłem, a nie słyszeliście, aleście czynili, co złego jest przed oczyma mojemi, a czegom Ja nie chciał, obieraliście.
13 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mtaona njaa; watumishi wangu watakunywa lakini ninyi mtaona kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mtaona haya.
Przetoż tak mówi panujący Pan: Oto słudzy moi jeść będą, a wy łaknąć będziecie; oto słudzy moi pić będą, a wy pragnąć będziecie; oto słudzy moi weselić się będą, a wy zawstydzeni będziecie.
14 Watumishi wangu wataimba kwa furaha ya mioyo yao, lakini ninyi mtalia kutokana na uchungu wa moyoni, na kupiga yowe kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.
Oto słudzy moi wykrzykać będą od radości serdecznej, a wy będziecie wołać od boleści serca, i od skruszenia ducha wyć będziecie.
15 Mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa; Bwana Mwenyezi atawaua ninyi, lakini watumishi wake atawapa jina jingine.
I zostawicie imię wasze na przeklinanie wybranym moim, gdy was pomorduje panujący Pan, a sługi swe nazwie innem imieniem.
16 Yeye aombaye baraka katika nchi atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli; yeye aapaye katika nchi ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika na kufichwa kutoka machoni pangu.
Ten, który sobie będzie błogosławił na ziemi, będzie sobie błogosławił w Bogu prawdziwym; a kto będzie przysięgał na ziemi, będzie przysięgał przez Boga prawdziwego; w zapomnienie zaiste przyjdą te uciski pierwsze, a będą zakryte od oczów moich.
17 “Tazama, nitaumba mbingu mpya na dunia mpya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayatakuja akilini.
Albowiem oto Ja tworzę niebiosa nowe, i ziemię nową, a nie będą wspominane rzeczy pierwsze, ani wstąpią na serce.
18 Lakini furahini na kushangilia daima katika hivi nitakavyoumba, kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza, nao watu wake wawe furaha.
Owszem weselcie się, a radujcie się na wieki wieków z tego, co Ja stworzę; bo oto Ja stworzę Jeruzalem na radość, a lud jego na wesele.
19 Nami nitaifurahia Yerusalemu na kuwafurahia watu wangu; sauti ya maombolezo na ya kilio haitasikika humo tena.
I rozraduję się w Jeruzalemie, a weselić się będę w ludu moim; a nie będzie słychać w nim głosu płaczu i głosu narzekania.
20 “Kamwe hatakuwepo tena ndani yake mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu, au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake. Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja atahesabiwa kwamba ni kijana tu, yeye ambaye hatafika miaka mia moja, atahesabiwa kuwa amelaaniwa.
Nie będzie tam więcej nikogo w wieku dziecinnym, ani starca, któryby nie dopełnił dni swoich; bo dziecię we stu latach umrze; ale grzesznik, choćby miał i sto lat, przeklęty będzie.
21 Watajenga nyumba na kuishi ndani yake; watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.
Pobudują też domy, a będą w nich mieszkali; nasadzą też winnic, a będą jeść owoce ich.
22 Hawatajenga nyumba, nao watu wengine waishi ndani yake, au kupanda mazao na wengine wale. Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti, ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi kazi za mikono yao.
Nie będą budować tak, aby tam inszy mieszkał; nie będą szczepić, aby inny jadł; bo dni ludu mojego będą jako dni drzewa, a dzieła rąk swoich do zwietszenia używać będą wybrani moi.
23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga, kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa na Bwana, wao na wazao wao pamoja nao.
Nie będą robić próżno, ani płodzić będą na postrach; bo będą nasieniem błogosławionych od Pana, oni i potomkowie ich z nimi.
24 Kabla hawajaita, nitajibu, nao wakiwa katika kunena, nitasikia.
Nadto stanie się, że pierwej niż zawołają, Ja się ozwę; jeszcze mówić będą, a Ja wysłucham.
25 Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, naye simba atakula nyasi kama maksai, lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote,” asema Bwana.
Wilk z barankiem paść się będą społem; lew jako wół plewy jeść będzie, a wężowi proch będzie chlebem jego; nie będą szkodzić ani zatracać na wszystkiej górze świętej mojej, mówi Pan.