< Isaya 65 >

1 “Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia. Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu, nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’
خداوند می‌فرماید: «به آنانی که مرا نمی‌جستند، خود را آشکار ساختم؛ و مردمانی که در جستجوی من نبودند، مرا یافتند.
2 Mchana kutwa nimeinyoosha mikono yangu kwa watu wakaidi, wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri, wafuatao mawazo yao wenyewe:
تمام روز دستهایم را به سوی قومی سرکش دراز کردم. اما آنها به راههای گناه‌آلود و طریقهای کج خود می‌روند.
3 taifa ambalo daima hunikasirisha machoni pangu, wakitoa dhabihu katika bustani na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;
آنها دائم مرا خشمگین می‌سازند. در مذبحهای باغهایشان به بتهای خویش قربانی تقدیم می‌کنند و برای آنها بخور می‌سوزانند.
4 watu waketio katikati ya makaburi na kukesha mahali pa siri, walao nyama za nguruwe, nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,
شبها به قبرستانهای داخل غارها می‌روند تا ارواح مردگان را پرستش کنند. گوشت خوک و خوراکهای حرام دیگر می‌خورند،
5 wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie, kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’ Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu, ni moto uwakao mchana kutwa.
ولی به دیگران می‌گویند: به ما نزدیک نشوید، ما را نجس نکنید، ما از شما مقدّس‌تر هستیم.» این مردم مرا از خود سخت بیزار کرده‌اند و به آتش خشم من دامن زده‌اند.
6 “Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu: sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu; nitalipiza mapajani mwao:
«حکم محکومیت این قوم در حضور من نوشته شده است. من دیگر تصمیم خود را گرفته‌ام و ساکت نخواهم نشست و آنان را به سزای اعمالشان خواهم رساند.
7 dhambi zenu na dhambi za baba zenu,” asema Bwana. “Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima na kunichokoza mimi juu ya vilima, nitawapimia mapajani mwao malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”
آنان را برای گناهانی که خود و اجدادشان مرتکب شده‌اند مجازات خواهم کرد. آنان بر روی کوهها برای بتها بخور سوزانده‌اند و به من اهانت کرده‌اند. بنابراین، آنان را به سزای اعمالشان خواهم رساند.»
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana katika kishada cha zabibu, nao watu husema, ‘Usikiharibu, kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’ hivyo ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.
خداوند می‌فرماید: «هیچ‌کس انگور خوب را از بین نمی‌برد، بلکه از آن شراب تهیه می‌کند. من هم تمام قوم خود را از بین نخواهم برد، بلکه کسانی را که مرا خدمت می‌کنند، حفظ خواهم کرد.
9 Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo, na kutoka kwa Yuda wale watakaomiliki milima yangu, nao watu wangu wateule watairithi, nako huko wataishi watumishi wangu.
اسرائیلی‌هایی را که از قبیلهٔ یهودا هستند برکت خواهم داد و نسل آنان سرزمین کوهستانی مرا تصرف خواهند کرد. قوم برگزیدهٔ من که مرا خدمت می‌کنند در این سرزمین زندگی خواهند کرد.
10 Sharoni itakuwa malisho kwa ajili ya makundi ya kondoo, na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia kwa makundi ya ngʼombe, kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.
آنان مرا خواهند پرستید و بار دیگر گله‌های خود را در دشتهای شارون و درهٔ عاکور خواهند چرانید.»
11 “Bali kwenu ninyi mnaomwacha Bwana na kuusahau mlima wangu mtakatifu, ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati, na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa kwa ajili ya Ajali,
اما خداوند به بقیهٔ قوم خود که او را ترک کرده‌اند چنین می‌گوید: «شما عبادتگاه مرا به دست فراموشی سپرده‌اید و خدایان”بخت“و”سرنوشت“را می‌پرستید.
12 nitawaagiza mfe kwa upanga, nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa; kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika, nilisema lakini hamkusikiliza. Mlitenda maovu machoni pangu, nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”
پس بدانید که تیره بخت شده، به سرنوشت شومی دچار خواهید شد و از بین خواهید رفت! هنگامی که شما را صدا کردم جواب ندادید، و وقتی سخن گفتم گوش ندادید؛ بلکه آنچه را که در نظرم ناپسند بود انجام دادید.»
13 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mtaona njaa; watumishi wangu watakunywa lakini ninyi mtaona kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mtaona haya.
بنابراین خداوند لشکرهای آسمان می‌فرماید: «به شما می‌گویم که خدمتگزاران من سیر خواهند شد، ولی شما گرسنه خواهید ماند؛ آنان آب خواهند نوشید، اما شما تشنه خواهید بود؛ آنان شادی خواهند کرد، ولی شما غمگین و شرمنده خواهید شد؛
14 Watumishi wangu wataimba kwa furaha ya mioyo yao, lakini ninyi mtalia kutokana na uchungu wa moyoni, na kupiga yowe kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.
آنان از خوشحالی آواز خواهند خواند، اما شما از غم و ناراحتی فریاد خواهید زد.
15 Mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa; Bwana Mwenyezi atawaua ninyi, lakini watumishi wake atawapa jina jingine.
نام شما در بین قوم من نامی ملعون خواهد بود. من که خداوند هستم شما را خواهم کشت و به خدمتگزاران راستین خود نامی جدید خواهم داد.»
16 Yeye aombaye baraka katika nchi atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli; yeye aapaye katika nchi ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika na kufichwa kutoka machoni pangu.
خداوند می‌فرماید: «روزی خواهد آمد که هر کس بخواهد برکتی بطلبد یا سوگندی یاد کند، تنها نام خدای حق را بر زبان خواهد راند. سختیهای گذشته به کلی فراموش شده، از بین خواهد رفت،
17 “Tazama, nitaumba mbingu mpya na dunia mpya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayatakuja akilini.
زیرا من زمین جدیدی می‌سازم. هر چه در گذشته بوده کاملاً فراموش شده، دیگر به یاد آورده نخواهد شد.
18 Lakini furahini na kushangilia daima katika hivi nitakavyoumba, kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza, nao watu wake wawe furaha.
ای قوم من، از این آفرینش جدید، تا ابد شاد و مسرور باشید، زیرا اورشلیم را نیز از نو می‌آفرینم تا شهر شادی و سرور شما باشد.
19 Nami nitaifurahia Yerusalemu na kuwafurahia watu wangu; sauti ya maombolezo na ya kilio haitasikika humo tena.
من خود نیز برای وجود اورشلیم و ساکنانش شادی خواهم کرد. در آنجا دیگر صدای گریه و زاری شنیده نخواهد شد.
20 “Kamwe hatakuwepo tena ndani yake mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu, au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake. Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja atahesabiwa kwamba ni kijana tu, yeye ambaye hatafika miaka mia moja, atahesabiwa kuwa amelaaniwa.
«نوزادان دیگر در سن کم نخواهند مرد و صد سالگان جوان محسوب خواهند شد. تنها کسانی پیش از وقت خواهند مرد که گناه می‌کنند و زیر لعنت هستند.
21 Watajenga nyumba na kuishi ndani yake; watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.
در آن روزها، هر که خانه‌ای بسازد خود در آن ساکن خواهد شد و هر که باغ انگوری غرس کند خود از میوهٔ آن خواهد خورد، زیرا دیگر خانه‌ها و باغهای انگور قوم من به دست دشمن نخواهند افتاد. ایشان مانند درختان، عمر طولانی خواهند کرد و از دسترنج خود بهره‌مند خواهند شد و لذت خواهند برد.
22 Hawatajenga nyumba, nao watu wengine waishi ndani yake, au kupanda mazao na wengine wale. Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti, ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi kazi za mikono yao.
23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga, kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa na Bwana, wao na wazao wao pamoja nao.
دیگر زحمتهایشان بر باد نخواهد رفت و فرزندانشان رنگ مصیبت را نخواهند دید، زیرا هم آنان را و هم فرزندانشان را برکت خواهم داد.
24 Kabla hawajaita, nitajibu, nao wakiwa katika kunena, nitasikia.
حتی پیش از آنکه مرا بخوانند به آنان جواب خواهم داد، و پیش از اینکه دعایشان را تمام کنند آن را اجابت خواهم کرد.
25 Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, naye simba atakula nyasi kama maksai, lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote,” asema Bwana.
گرگ و بره با هم خواهند چرید، شیر مانند گاو کاه خواهد خورد، اما خوراک مار خاک خواهد بود. در کوه مقدّس من هیچ چیز و هیچ‌کس صدمه نخواهد دید و نابود نخواهد شد.»

< Isaya 65 >