< Isaya 65 >

1 “Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia. Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu, nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’
Ils m’ont cherché, ceux qui auparavant ne m’interrogeaient pas; ils m’ont trouvé, ceux qui ne m’ont pas cherché; j’ai dit: Me voici, me voici, à une nation qui n’invoquait pas mon nom.
2 Mchana kutwa nimeinyoosha mikono yangu kwa watu wakaidi, wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri, wafuatao mawazo yao wenyewe:
J’ai étendu mes mains tout le jour à un peuple incrédule, qui marche dans une voie qui n’est pas bonne, à la suite de ses pensées.
3 taifa ambalo daima hunikasirisha machoni pangu, wakitoa dhabihu katika bustani na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;
C’est un peuple qui me provoque au courroux devant ma face sans cesse; qui immolent dans les jardins, et sacrifient sur les briques;
4 watu waketio katikati ya makaburi na kukesha mahali pa siri, walao nyama za nguruwe, nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,
Qui habitent dans les sépulcres, qui dorment dans les temples des idoles; qui mangent de la chair de porc, et mettent du jus profane dans leurs vases;
5 wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie, kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’ Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu, ni moto uwakao mchana kutwa.
Qui disent: Retire-toi de moi, ne m’approche pas, parce que tu es impur; ceux-là seront une fumée dans ma fureur, un feu brûlant tout le jour.
6 “Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu: sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu; nitalipiza mapajani mwao:
Voilà que c’est écrit devant moi; je ne me tairai pas, mais je rendrai, et je verserai dans leur sein
7 dhambi zenu na dhambi za baba zenu,” asema Bwana. “Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima na kunichokoza mimi juu ya vilima, nitawapimia mapajani mwao malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”
Vos iniquités, dit le Seigneur, en même temps que les iniquités de vos pères, qui ont sacrifié sur les montagnes, et m’ont outragé sur les collines, et je verserai leurs premières œuvres à égale mesure dans leur sein.
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana katika kishada cha zabibu, nao watu husema, ‘Usikiharibu, kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’ hivyo ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.
Voici ce que dit le Seigneur: De même que si on trouve un grain dans une grappe de raisin, et Sion dit: Ne le perds pas, parce que c’est une bénédiction, de même aussi je ferai en sorte, à cause de mes serviteurs, que je ne perde pas entièrement tout Israël.
9 Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo, na kutoka kwa Yuda wale watakaomiliki milima yangu, nao watu wangu wateule watairithi, nako huko wataishi watumishi wangu.
Je ferai sortir de Jacob une postérité, et de Juda celui qui possédera mes montagnes; mes élus hériteront de cette terre et mes serviteurs y habiteront.
10 Sharoni itakuwa malisho kwa ajili ya makundi ya kondoo, na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia kwa makundi ya ngʼombe, kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.
Et les campagnes serviront de parcs aux troupeaux de menu bétail, et la vallée d’Achor, de retraite aux troupeaux de gros bétail, en faveur de ceux de mon peuple qui m’ont recherché.
11 “Bali kwenu ninyi mnaomwacha Bwana na kuusahau mlima wangu mtakatifu, ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati, na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa kwa ajili ya Ajali,
Mais vous qui avez abandonné le Seigneur, qui avez oublié ma montagne sainte, qui dressez une table à la Fortune, et y faites des libations,
12 nitawaagiza mfe kwa upanga, nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa; kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika, nilisema lakini hamkusikiliza. Mlitenda maovu machoni pangu, nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”
Je vous compterai avec le glaive, et tous vous tomberez dans ce carnage, parce que j’ai appelé, et vous n’avez pas répondu; j’ai parlé, et vous n’avez pas écouté; vous faisiez le mal à mes yeux, et tout ce que je n’ai pas voulu, vous l’avez choisi.
13 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mtaona njaa; watumishi wangu watakunywa lakini ninyi mtaona kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mtaona haya.
À cause de cela voici ce que dit le Seigneur Dieu: Voilà que mes serviteurs mangeront, et vous, vous aurez faim; voilà que mes serviteurs boiront, et vous, vous aurez soif;
14 Watumishi wangu wataimba kwa furaha ya mioyo yao, lakini ninyi mtalia kutokana na uchungu wa moyoni, na kupiga yowe kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.
Voilà que mes serviteurs se réjouiront, et vous, vous serez confus; voilà que mes serviteurs chanteront des louanges dans l’exultation de leur cœur, et vous, vous jetterez des cris dans la douleur de votre cœur, et dans le brisement de votre esprit vous pousserez des hurlements.
15 Mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa; Bwana Mwenyezi atawaua ninyi, lakini watumishi wake atawapa jina jingine.
Et vous laisserez votre nom à mes serviteurs comme un objet d’imprécation; et le Seigneur Dieu te détruira, et il appellera ses serviteurs d’un autre nom,
16 Yeye aombaye baraka katika nchi atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli; yeye aapaye katika nchi ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika na kufichwa kutoka machoni pangu.
Dans lequel celui qui est béni sur la terre sera béni dans le Dieu de vérité, et celui qui jure sur la terre jurera par le Dieu de vérité; parce qu’à l’oubli ont été livrées les premières angoisses, et qu’elles ont été cachées à ma face.
17 “Tazama, nitaumba mbingu mpya na dunia mpya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayatakuja akilini.
Car voici que je crée des cieux nouveaux et une terre nouvelle; les choses passées ne seront pas dans la mémoire, et elles ne monteront pas sur le cœur.
18 Lakini furahini na kushangilia daima katika hivi nitakavyoumba, kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza, nao watu wake wawe furaha.
Mais vous vous réjouirez, vous exulterez à jamais dans les choses que je crée; parce que voici que je crée Jérusalem exultation, et son peuple joie.
19 Nami nitaifurahia Yerusalemu na kuwafurahia watu wangu; sauti ya maombolezo na ya kilio haitasikika humo tena.
Et j’exulterai en Jérusalem, et je me réjouirai en mon peuple; et on n’y entendra plus la voix du pleur et la voix du cri.
20 “Kamwe hatakuwepo tena ndani yake mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu, au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake. Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja atahesabiwa kwamba ni kijana tu, yeye ambaye hatafika miaka mia moja, atahesabiwa kuwa amelaaniwa.
Il n’y aura plus là d’enfants de peu de jours, et de vieillard qui ne remplisse ses jours; parce que l’enfant mourra à cent ans, et que le pécheur de cent ans sera maudit.
21 Watajenga nyumba na kuishi ndani yake; watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.
Et ils bâtiront des maisons et ils les habiteront; ils planteront des vignes et ils en mangeront les fruits.
22 Hawatajenga nyumba, nao watu wengine waishi ndani yake, au kupanda mazao na wengine wale. Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti, ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi kazi za mikono yao.
Ils ne bâtiront pas pour qu’un autre habite; ils ne planteront pas pour qu’un autre mange; car à l’égal des jours de l’arbre, seront les jours de mon peuple; et les ouvrages de leurs mains auront une longue durée;
23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga, kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa na Bwana, wao na wazao wao pamoja nao.
Mes élus ne travailleront pas en vain, et ils n’engendreront pas dans le trouble; parce qu’ils sont la race des bénis du Seigneur, et que leurs descendants seront bénis avec eux.
24 Kabla hawajaita, nitajibu, nao wakiwa katika kunena, nitasikia.
Et il arrivera qu’avant qu’ils crient, moi je les exaucerai; eux parlant encore, j’écouterai.
25 Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, naye simba atakula nyasi kama maksai, lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote,” asema Bwana.
Le loup et l’agneau paîtront ensemble; le lion et le bœuf mangeront la paille, et pour le serpent, la poussière sera son pain; ils ne nuiront point, et ils ne tueront point sur toute ma montagne sainte, dit le Seigneur.

< Isaya 65 >