< Isaya 65 >

1 “Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia. Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu, nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’
Je me suis fait rechercher de ceux qui ne me demandaient point, et je me suis fait trouver à ceux qui ne me cherchaient point; j'ai dit à la nation qui ne s'appelait point de mon Nom; me voici, me voici.
2 Mchana kutwa nimeinyoosha mikono yangu kwa watu wakaidi, wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri, wafuatao mawazo yao wenyewe:
J'ai tout le jour étendu mes mains au peuple rebelle, à ceux qui marchent dans le mauvais chemin, [savoir] après leurs pensées;
3 taifa ambalo daima hunikasirisha machoni pangu, wakitoa dhabihu katika bustani na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;
Au peuple de ceux qui m'irritent continuellement en face, qui sacrifient dans les jardins, et qui font des parfums sur les [autels de] briques.
4 watu waketio katikati ya makaburi na kukesha mahali pa siri, walao nyama za nguruwe, nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,
Qui se tiennent dans les sépulcres, et passent la nuit dans les lieux désolés; qui mangent la chair de pourceau, et qui [ont dans] leurs vaisseaux le jus des choses abominables.
5 wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie, kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’ Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu, ni moto uwakao mchana kutwa.
Qui disent; retire toi, n'approche point de moi, car je suis plus saint que toi; ceux-là sont une fumée à mes narines, un feu ardent tout le jour.
6 “Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu: sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu; nitalipiza mapajani mwao:
Voici, ceci est écrit devant moi, je ne m'en tairai point, mais je le rendrai, oui je le rendrai dans leur sein,
7 dhambi zenu na dhambi za baba zenu,” asema Bwana. “Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima na kunichokoza mimi juu ya vilima, nitawapimia mapajani mwao malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”
[A savoir] vos iniquités, et les iniquités de vos pères ensemble, a dit l'Eternel; lesquels ont fait des parfums sur les montagnes, et m'ont déshonoré sur les coteaux; c'est pourquoi je leur mesurerai aussi dans leur sein le salaire de ce qu'ils ont fait au commencement.
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana katika kishada cha zabibu, nao watu husema, ‘Usikiharibu, kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’ hivyo ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.
Ainsi a dit l'Eternel; comme quand on trouve dans une grappe du vin [à épreindre], et qu'on dit; ne la gâte pas, car il y a en elle de la bénédiction; j'en ferai de même à cause de mes serviteurs, afin que le tout ne soit point détruit.
9 Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo, na kutoka kwa Yuda wale watakaomiliki milima yangu, nao watu wangu wateule watairithi, nako huko wataishi watumishi wangu.
Et je ferai sortir de la postérité de Jacob et de Juda celui qui héritera mes montagnes, et mes élus hériteront le pays, et mes serviteurs y habiteront.
10 Sharoni itakuwa malisho kwa ajili ya makundi ya kondoo, na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia kwa makundi ya ngʼombe, kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.
Et Saron sera pour les cabanes du menu bétail, et la vallée de Hachor sera le gîte du gros bétail, pour mon peuple qui m'aura recherché.
11 “Bali kwenu ninyi mnaomwacha Bwana na kuusahau mlima wangu mtakatifu, ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati, na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa kwa ajili ya Ajali,
Mais vous, qui abandonnez l'Eternel, et qui oubliez la montagne de ma sainteté, qui dressez la table à l'armée des cieux, et qui fournissez l'aspersion à autant qu'on en peut compter;
12 nitawaagiza mfe kwa upanga, nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa; kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika, nilisema lakini hamkusikiliza. Mlitenda maovu machoni pangu, nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”
Je vous compterai aussi avec l'épée, et vous serez tous courbés, pour être égorgés; parce que j'ai appelé, et que vous n'avez point répondu; j'ai parlé, et vous n'avez point écouté; mais vous avez fait ce qui me déplaît, et vous avez choisi les choses auxquelles je ne prends point de plaisir.
13 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mtaona njaa; watumishi wangu watakunywa lakini ninyi mtaona kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mtaona haya.
C'est pourquoi, ainsi a dit le Seigneur l'Eternel; voici, mes serviteurs mangeront, et vous aurez faim; voici, mes serviteurs boiront, et vous aurez soif; voici mes serviteurs se réjouiront, et vous serez honteux.
14 Watumishi wangu wataimba kwa furaha ya mioyo yao, lakini ninyi mtalia kutokana na uchungu wa moyoni, na kupiga yowe kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.
Voici, mes serviteurs se réjouiront avec chant de triomphe pour la joie qu'ils auront au cœur, mais vous crierez pour la douleur que vous aurez au cœur, et vous hurlerez à cause de l'accablement de votre esprit.
15 Mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa; Bwana Mwenyezi atawaua ninyi, lakini watumishi wake atawapa jina jingine.
Et vous laisserez votre nom à mes élus pour s'en servir dans les exécrations, et le Seigneur l'Eternel te fera mourir; mais il appellera ses serviteurs d'un autre nom.
16 Yeye aombaye baraka katika nchi atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli; yeye aapaye katika nchi ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika na kufichwa kutoka machoni pangu.
Celui qui se bénira en la terre, se bénira par le Dieu de Vérité; et celui qui jurera sur la terre, jurera par le Dieu de Vérité; car les angoisses du passé seront oubliées, et même elles seront cachées devant mes yeux.
17 “Tazama, nitaumba mbingu mpya na dunia mpya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayatakuja akilini.
Car voici, je m'en vais créer de nouveaux cieux, et une nouvelle terre; et on ne se souviendra plus des choses précédentes, et elles ne reviendront plus au cœur.
18 Lakini furahini na kushangilia daima katika hivi nitakavyoumba, kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza, nao watu wake wawe furaha.
Mais plutôt vous vous réjouirez, et vous vous égayerez à toujours en ce que je m'en vais créer; car voici, je m'en vais créer Jérusalem, pour n'être que joie, et son peuple, pour n'être qu'allégresse.
19 Nami nitaifurahia Yerusalemu na kuwafurahia watu wangu; sauti ya maombolezo na ya kilio haitasikika humo tena.
Je m'égayerai donc sur Jérusalem, et je me réjouirai sur mon peuple; et on n'y entendra plus de voix de pleurs, ni de voix de clameurs.
20 “Kamwe hatakuwepo tena ndani yake mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu, au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake. Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja atahesabiwa kwamba ni kijana tu, yeye ambaye hatafika miaka mia moja, atahesabiwa kuwa amelaaniwa.
Il n'y aura plus désormais aucun enfant né depuis peu de jours, ni aucun vieillard qui n'accomplisse ses jours; car celui qui mourra âgé de cent ans [sera encore] jeune; mais le pécheur âgé de cent ans sera maudit.
21 Watajenga nyumba na kuishi ndani yake; watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.
Même ils bâtiront des maisons, et y habiteront; ils planteront des vignes, et ils en mangeront le fruit.
22 Hawatajenga nyumba, nao watu wengine waishi ndani yake, au kupanda mazao na wengine wale. Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti, ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi kazi za mikono yao.
Ils ne bâtiront pas des maisons afin qu'un autre y habite; ils ne planteront pas [des vignes] afin qu'un autre en mange le fruit; car les jours de mon peuple seront comme les jours des arbres; et mes élus perpétueront le travail de leurs mains.
23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga, kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa na Bwana, wao na wazao wao pamoja nao.
Ils ne travailleront plus en vain, et n'engendreront [plus des enfants pour être exposés] à la frayeur; car ils seront la postérité des bénis de l'Eternel, et ceux qui sortiront d'eux seront avec eux.
24 Kabla hawajaita, nitajibu, nao wakiwa katika kunena, nitasikia.
Et il arrivera qu'avant qu'ils crient, je les exaucerai; et lorsque encore ils parleront, je les aurai [déjà] ouïs.
25 Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, naye simba atakula nyasi kama maksai, lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote,” asema Bwana.
Le loup et l'agneau paîtront ensemble, et le lion mangera du fourrage comme le bœuf, et la poudre sera la nourriture du serpent; on ne nuira point, et on ne fera aucun dommage dans toute la montagne de ma sainteté; a dit l'Eternel.

< Isaya 65 >