< Isaya 65 >

1 “Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia. Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu, nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’
Je me suis manifesté à ceux qui ne me demandaient point; j'ai été trouvé par ceux qui ne me cherchaient pas; j'ai dit à un peuple qui n'avait point invoqué mon nom: Me voici.
2 Mchana kutwa nimeinyoosha mikono yangu kwa watu wakaidi, wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri, wafuatao mawazo yao wenyewe:
Durant tout le jour j'ai tendu les mains à un peuple désobéissant et contradicteur, à des hommes qui marchaient non dans la bonne voie, mais à la suite de leurs péchés.
3 taifa ambalo daima hunikasirisha machoni pangu, wakitoa dhabihu katika bustani na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;
Ce peuple est celui qui ne cesse pas de m'irriter en face; ils sacrifient dans leurs jardins, et ils brûlent de l'encens sur des briques, pour des divinités qui n'existent pas.
4 watu waketio katikati ya makaburi na kukesha mahali pa siri, walao nyama za nguruwe, nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,
Ils se couchent sur des sépulcres ou des cavernes, à propos de leurs songes; et ils mangent de la chair de porc avec le jus de leurs victimes; et tous leurs vases sont souillés.
5 wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie, kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’ Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu, ni moto uwakao mchana kutwa.
Ce sont eux qui disent: Loin de moi, ne m'approche pas; car je suis pur. Mon courroux les réduira en fumée, et en eux brûlera un feu éternel.
6 “Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu: sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu; nitalipiza mapajani mwao:
Voilà qu'il est écrit devant mes yeux: Je ne garderai point le silence jusqu'à ce que j'aie puni dans leur sein
7 dhambi zenu na dhambi za baba zenu,” asema Bwana. “Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima na kunichokoza mimi juu ya vilima, nitawapimia mapajani mwao malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”
Leurs péchés et ceux de leurs pères, dit le Seigneur. Ceux qui ont sacrifié sur les montagnes, ceux qui m'ont outragé sur les collines, recevront dans leur sein la punition de leurs œuvres.
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana katika kishada cha zabibu, nao watu husema, ‘Usikiharibu, kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’ hivyo ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.
Ainsi dit le Seigneur: De même que s'il se trouve un grain mûr dans un verjus, on dit: Ne le gâtez point, parce que la bénédiction est en lui; ainsi ferai-je pour l'amour d'un seul qui me sert; pour l'amour de celui-là je ne les détruirai pas tous.
9 Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo, na kutoka kwa Yuda wale watakaomiliki milima yangu, nao watu wangu wateule watairithi, nako huko wataishi watumishi wangu.
Et je délivrerai la postérité de Jacob et de Juda; elle aura pour héritage ma montagne sainte; mes élus et mes serviteurs l'auront pour héritage, et ils y demeureront.
10 Sharoni itakuwa malisho kwa ajili ya makundi ya kondoo, na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia kwa makundi ya ngʼombe, kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.
Et il y aura dans la forêt des bergeries pour les menus troupeaux; et dans la vallée d'Achor se reposeront les bœufs de mon peuple, de ceux qui m'auront cherché.
11 “Bali kwenu ninyi mnaomwacha Bwana na kuusahau mlima wangu mtakatifu, ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati, na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa kwa ajili ya Ajali,
Et vous qui m'abandonnez et qui oubliez ma montagne sainte, qui dressez une table pour le démon et qui mêlez le vin pour faire des libations à la fortune,
12 nitawaagiza mfe kwa upanga, nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa; kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika, nilisema lakini hamkusikiliza. Mlitenda maovu machoni pangu, nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”
Je vous livrerai au glaive, vous tomberez sous le couteau; car je vous ai appelés, et vous ne m'avez point obéi; j'ai parlé, et vous n'avez pas entendu, et devant moi vous avez fait le mal, et ce que je rejetais, vous l'avez choisi.
13 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mtaona njaa; watumishi wangu watakunywa lakini ninyi mtaona kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mtaona haya.
C'est pourquoi, voici ce que dit le Seigneur: Ceux qui me servent mangeront; et vous, vous aurez faim; ceux qui me servent boiront, et vous, vous aurez soif.
14 Watumishi wangu wataimba kwa furaha ya mioyo yao, lakini ninyi mtalia kutokana na uchungu wa moyoni, na kupiga yowe kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.
Ceux qui me servent vivront dans la joie, et vous, vous serez confondus; ceux qui me servent tressailliront d'allégresse, et vous, vous crierez dans la tristesse de votre cœur, et vous hurlerez dans le déchirement de votre esprit.
15 Mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa; Bwana Mwenyezi atawaua ninyi, lakini watumishi wake atawapa jina jingine.
Et vous laisserez votre nom comme un objet de dégoût à mes élus, et le Seigneur vous détruira, et un nom nouveau sera donné à ceux qui le servent.
16 Yeye aombaye baraka katika nchi atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli; yeye aapaye katika nchi ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika na kufichwa kutoka machoni pangu.
Et ce nom sera béni sur la terre; car ils béniront le Dieu véritable; et ceux qui jureront sur la terre jureront par le Dieu véritable; ils oublieront leur ancienne affliction, qui ne reviendra plus en leur cœur.
17 “Tazama, nitaumba mbingu mpya na dunia mpya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayatakuja akilini.
Car il y aura un ciel nouveau et une terre nouvelle; on ne se souviendra plus des choses d'autrefois, et le souvenir n'en reviendra plus en leur cœur.
18 Lakini furahini na kushangilia daima katika hivi nitakavyoumba, kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza, nao watu wake wawe furaha.
Mais ils y trouveront la joie et l'allégresse; car moi-même je ferai de Jérusalem l'allégresse, et de mon peuple la joie.
19 Nami nitaifurahia Yerusalemu na kuwafurahia watu wangu; sauti ya maombolezo na ya kilio haitasikika humo tena.
Et à mon tour je ferai de Jérusalem mes délices, et de mon peuple ma joie; et l'on n'y entendra plus la voix des pleurs, ni celle des gémissements.
20 “Kamwe hatakuwepo tena ndani yake mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu, au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake. Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja atahesabiwa kwamba ni kijana tu, yeye ambaye hatafika miaka mia moja, atahesabiwa kuwa amelaaniwa.
Il n'y aura plus là ni enfant qui meure avant l'âge, ni vieillard qui ne remplisse son temps. Le jeune homme vivra cent ans, et le pécheur à sa mort aura aussi cent ans; mais celui-là sera maudit.
21 Watajenga nyumba na kuishi ndani yake; watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.
Et ils bâtiront des maisons, et ils y demeureront, et ils y planteront des vignes, et ils en mangeront les fruits.
22 Hawatajenga nyumba, nao watu wengine waishi ndani yake, au kupanda mazao na wengine wale. Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti, ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi kazi za mikono yao.
Et ils ne bâtiront plus pour autrui, et ils ne planteront plus pour que d'autres mangent. Les jours de mon peuple seront comme les jours de l'arbre de vie, et les travaux où ils auront pris de la peine atteindront la vieillesse.
23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga, kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa na Bwana, wao na wazao wao pamoja nao.
Mes élus ne se fatigueront pas en vain; ils n'auront point d'enfants pour leur malédiction, car c'est une race bénie de Dieu; et leurs petits enfants comme eux seront bénis.
24 Kabla hawajaita, nitajibu, nao wakiwa katika kunena, nitasikia.
Et avant qu'ils aient crié je les aurai exaucés; pendant qu'ils parleront encore, je dirai: Qu'y a-t-il?
25 Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, naye simba atakula nyasi kama maksai, lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote,” asema Bwana.
Alors les loups et les agneaux viendront paître ensemble; le lion mangera de la paille comme le bœuf, et le serpent mangera la terre comme du pain. Ils ne nuiront à personne; ils ne détruiront rien sur ma montagne sainte, dit le Seigneur.

< Isaya 65 >