< Isaya 65 >

1 “Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia. Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu, nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’
to seek to/for not to ask to find to/for not to seek me to say look! I look! I to(wards) nation not to call: call by in/on/with name my
2 Mchana kutwa nimeinyoosha mikono yangu kwa watu wakaidi, wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri, wafuatao mawazo yao wenyewe:
to spread hand my all [the] day to(wards) people to rebel [the] to go: walk [the] way: conduct not pleasant after plot their
3 taifa ambalo daima hunikasirisha machoni pangu, wakitoa dhabihu katika bustani na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;
[the] people [the] to provoke [obj] me upon face my continually to sacrifice in/on/with garden and to offer: offer upon [the] brick
4 watu waketio katikati ya makaburi na kukesha mahali pa siri, walao nyama za nguruwe, nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,
[the] to dwell in/on/with grave and in/on/with to watch to lodge [the] to eat flesh [the] swine (and broth *Q(K)*) refuse article/utensil their
5 wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie, kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’ Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu, ni moto uwakao mchana kutwa.
[the] to say to present: come to(wards) you not to approach: approach in/on/with me for to consecrate: consecate you these smoke in/on/with face: nose my fire to burn all [the] day
6 “Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu: sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu; nitalipiza mapajani mwao:
behold to write to/for face: before my not be silent that if: except if: except to complete and to complete upon bosom: lap their
7 dhambi zenu na dhambi za baba zenu,” asema Bwana. “Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima na kunichokoza mimi juu ya vilima, nitawapimia mapajani mwao malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”
iniquity: crime your and iniquity: crime father your together to say LORD which to offer: offer upon [the] mountain: mount and upon [the] hill to taunt me and to measure wages their first: previous (to(wards) *Q(K)*) bosom: lap their
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana katika kishada cha zabibu, nao watu husema, ‘Usikiharibu, kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’ hivyo ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.
thus to say LORD like/as as which to find [the] new wine in/on/with cluster and to say not to ruin him for blessing in/on/with him so to make: do because servant/slave my to/for lest to ruin [the] all
9 Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo, na kutoka kwa Yuda wale watakaomiliki milima yangu, nao watu wangu wateule watairithi, nako huko wataishi watumishi wangu.
and to come out: send from Jacob seed: children and from Judah to possess: possess mountain: mount my and to possess: take her chosen my and servant/slave my to dwell there [to]
10 Sharoni itakuwa malisho kwa ajili ya makundi ya kondoo, na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia kwa makundi ya ngʼombe, kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.
and to be [the] Sharon to/for pasture flock and Valley (of Achor) (Valley of) Achor to/for rest cattle to/for people my which to seek me
11 “Bali kwenu ninyi mnaomwacha Bwana na kuusahau mlima wangu mtakatifu, ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati, na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa kwa ajili ya Ajali,
and you(m. p.) to leave: forsake LORD [the] forgetful [obj] mountain: mount holiness my [the] to arrange to/for Fortune table and [the] to fill to/for Destiny mixed drink
12 nitawaagiza mfe kwa upanga, nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa; kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika, nilisema lakini hamkusikiliza. Mlitenda maovu machoni pangu, nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”
and to count [obj] you to/for sword and all your to/for slaughter to bow because to call: call to and not to answer to speak: speak and not to hear: hear and to make: do [the] bad: evil in/on/with eye my and in/on/with in which not to delight in to choose
13 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mtaona njaa; watumishi wangu watakunywa lakini ninyi mtaona kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mtaona haya.
to/for so thus to say Lord YHWH/God behold servant/slave my to eat and you(m. p.) be hungry behold servant/slave my to drink and you(m. p.) to thirst behold servant/slave my to rejoice and you(m. p.) be ashamed
14 Watumishi wangu wataimba kwa furaha ya mioyo yao, lakini ninyi mtalia kutokana na uchungu wa moyoni, na kupiga yowe kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.
behold servant/slave my to sing from goodness heart and you(m. p.) to cry from pain heart and from breaking spirit to wail
15 Mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa; Bwana Mwenyezi atawaua ninyi, lakini watumishi wake atawapa jina jingine.
and to rest name your to/for oath to/for chosen my and to die you Lord YHWH/God and to/for servant/slave his to call: call by name another
16 Yeye aombaye baraka katika nchi atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli; yeye aapaye katika nchi ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika na kufichwa kutoka machoni pangu.
which [the] to bless in/on/with land: country/planet to bless in/on/with God amen and [the] to swear in/on/with land: country/planet to swear in/on/with God amen for to forget [the] distress [the] first: previous and for to hide from eye my
17 “Tazama, nitaumba mbingu mpya na dunia mpya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayatakuja akilini.
for look! I to create heaven new and land: country/planet new and not to remember [the] first: previous and not to ascend: rise upon heart
18 Lakini furahini na kushangilia daima katika hivi nitakavyoumba, kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza, nao watu wake wawe furaha.
for if: except to rejoice and to rejoice till perpetuity which I to create for look! I to create [obj] Jerusalem rejoicing and people her rejoicing
19 Nami nitaifurahia Yerusalemu na kuwafurahia watu wangu; sauti ya maombolezo na ya kilio haitasikika humo tena.
and to rejoice in/on/with Jerusalem and to rejoice in/on/with people my and not to hear: hear in/on/with her still voice: sound weeping and voice outcry
20 “Kamwe hatakuwepo tena ndani yake mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu, au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake. Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja atahesabiwa kwamba ni kijana tu, yeye ambaye hatafika miaka mia moja, atahesabiwa kuwa amelaaniwa.
not to be from there still infant day and old which not to fill [obj] day his for [the] youth son: aged hundred year to die and [the] to sin son: aged hundred year to lighten
21 Watajenga nyumba na kuishi ndani yake; watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.
and to build house: home and to dwell and to plant vineyard and to eat fruit their
22 Hawatajenga nyumba, nao watu wengine waishi ndani yake, au kupanda mazao na wengine wale. Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti, ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi kazi za mikono yao.
not to build and another to dwell not to plant and another to eat for like/as day [the] tree day people my and deed: work hand their to become old chosen my
23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga, kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa na Bwana, wao na wazao wao pamoja nao.
not be weary/toil to/for vain and not to beget to/for dismay for seed: children to bless LORD they(masc.) and offspring their with them
24 Kabla hawajaita, nitajibu, nao wakiwa katika kunena, nitasikia.
and to be before to call: call to and I to answer still they(masc.) to speak: speak and I to hear: hear
25 Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, naye simba atakula nyasi kama maksai, lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote,” asema Bwana.
wolf and lamb to pasture like/as one and lion like/as cattle to eat straw and serpent dust food his not be evil and not to ruin in/on/with all mountain: mount holiness my to say LORD

< Isaya 65 >