< Isaya 65 >

1 “Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia. Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu, nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’
I gave access to them that asked not for Me, I was at hand to them that sought Me not; I said: 'Behold Me, behold Me', unto a nation that was not called by My name.
2 Mchana kutwa nimeinyoosha mikono yangu kwa watu wakaidi, wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri, wafuatao mawazo yao wenyewe:
I have spread out My hands all the day unto a rebellious people, that walk in a way that is not good, after their own thoughts;
3 taifa ambalo daima hunikasirisha machoni pangu, wakitoa dhabihu katika bustani na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;
A people that provoke Me to My face continually, that sacrifice in gardens, and burn incense upon bricks;
4 watu waketio katikati ya makaburi na kukesha mahali pa siri, walao nyama za nguruwe, nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,
That sit among the graves, and lodge in the vaults; that eat swine's flesh, and broth of abominable things is in their vessels;
5 wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie, kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’ Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu, ni moto uwakao mchana kutwa.
That say: 'Stand by thyself, come not near to me, for I am holier than thou'; these are a smoke in My nose, a fire that burneth all the day.
6 “Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu: sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu; nitalipiza mapajani mwao:
Behold, it is written before Me; I will not keep silence, except I have requited, yea, I will requite into their bosom,
7 dhambi zenu na dhambi za baba zenu,” asema Bwana. “Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima na kunichokoza mimi juu ya vilima, nitawapimia mapajani mwao malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”
Your own iniquities, and the iniquities of your fathers together, saith the LORD, that have offered upon the mountains, and blasphemed Me upon the hills; therefore will I first measure their wage into their bosom.
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana katika kishada cha zabibu, nao watu husema, ‘Usikiharibu, kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’ hivyo ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.
Thus saith the LORD: As, when wine is found in the cluster, one saith: 'Destroy it not, for a blessing is in it'; so will I do for My servants' sakes, that I may not destroy all.
9 Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo, na kutoka kwa Yuda wale watakaomiliki milima yangu, nao watu wangu wateule watairithi, nako huko wataishi watumishi wangu.
And I will bring forth a seed out of Jacob, and out of Judah an inheritor of My mountains; and Mine elect shall inherit it, and My servants shall dwell there.
10 Sharoni itakuwa malisho kwa ajili ya makundi ya kondoo, na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia kwa makundi ya ngʼombe, kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.
And Sharon shall be a fold of flocks, and the valley of Achor a place for herds to lie down in, for My people that have sought Me;
11 “Bali kwenu ninyi mnaomwacha Bwana na kuusahau mlima wangu mtakatifu, ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati, na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa kwa ajili ya Ajali,
But ye that forsake the LORD, that forget My holy mountain, that prepare a table for Fortune, and that offer mingled wine in full measure unto Destiny,
12 nitawaagiza mfe kwa upanga, nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa; kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika, nilisema lakini hamkusikiliza. Mlitenda maovu machoni pangu, nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”
I will destine you to the sword, and ye shall all bow down to the slaughter; because when I called, ye did not answer, when I spoke, ye did not hear; but ye did that which was evil in Mine eyes, and chose that wherein I delighted not.
13 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mtaona njaa; watumishi wangu watakunywa lakini ninyi mtaona kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mtaona haya.
Therefore thus saith the Lord GOD: Behold, My servants shall eat, but ye shall be hungry; Behold, My servants shall drink, but ye shall be thirsty; Behold, My servants shall rejoice, but ye shall be ashamed;
14 Watumishi wangu wataimba kwa furaha ya mioyo yao, lakini ninyi mtalia kutokana na uchungu wa moyoni, na kupiga yowe kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.
Behold, My servants shall sing for joy of heart, but ye shall cry for sorrow of heart, and shall wail for vexation of spirit.
15 Mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa; Bwana Mwenyezi atawaua ninyi, lakini watumishi wake atawapa jina jingine.
And ye shall leave your name for a curse unto Mine elect: 'So may the Lord GOD slay thee'; but He shall call His servants by another name;
16 Yeye aombaye baraka katika nchi atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli; yeye aapaye katika nchi ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika na kufichwa kutoka machoni pangu.
So that he who blesseth himself in the earth shall bless himself by the God of truth; and he that sweareth in the earth shall swear by the God of truth; because the former troubles are forgotten, and because they are hid from Mine eyes.
17 “Tazama, nitaumba mbingu mpya na dunia mpya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayatakuja akilini.
For, behold, I create new heavens and a new earth; and the former things shall not be remembered, nor come into mind.
18 Lakini furahini na kushangilia daima katika hivi nitakavyoumba, kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza, nao watu wake wawe furaha.
But be ye glad and rejoice for ever in that which I create; for, behold, I create Jerusalem a rejoicing, and her people a joy.
19 Nami nitaifurahia Yerusalemu na kuwafurahia watu wangu; sauti ya maombolezo na ya kilio haitasikika humo tena.
And I will rejoice in Jerusalem, and joy in My people; and the voice of weeping shall be no more heard in her, nor the voice of crying.
20 “Kamwe hatakuwepo tena ndani yake mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu, au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake. Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja atahesabiwa kwamba ni kijana tu, yeye ambaye hatafika miaka mia moja, atahesabiwa kuwa amelaaniwa.
There shall be no more thence an infant of days, nor an old man, that hath not filled his days; for the youngest shall die a hundred years old, and the sinner being a hundred years old shall be accursed.
21 Watajenga nyumba na kuishi ndani yake; watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.
And they shall build houses, and inhabit them; and they shall plant vineyards, and eat the fruit of them.
22 Hawatajenga nyumba, nao watu wengine waishi ndani yake, au kupanda mazao na wengine wale. Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti, ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi kazi za mikono yao.
They shall not build, and another inhabit, they shall not plant, and another eat; for as the days of a tree shall be the days of My people, and Mine elect shall long enjoy the work of their hands.
23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga, kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa na Bwana, wao na wazao wao pamoja nao.
They shall not labour in vain, nor bring forth for terror; for they are the seed blessed of the LORD, and their offspring with them.
24 Kabla hawajaita, nitajibu, nao wakiwa katika kunena, nitasikia.
And it shall come to pass that, before they call, I will answer, and while they are yet speaking, I will hear.
25 Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, naye simba atakula nyasi kama maksai, lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote,” asema Bwana.
The wolf and the lamb shall feed together, and the lion shall eat straw like the ox; and dust shall be the serpent's food. They shall not hurt nor destroy in all My holy mountain, saith the LORD.

< Isaya 65 >