< Isaya 64 >

1 Laiti ungelipasua mbingu na kushuka chini, ili milima ingelitetemeka mbele zako!
I wolde that thou brakist heuenes, and camest doun, that hillis fletiden awei fro thi face,
2 Kama vile moto uteketezavyo vijiti na kusababisha maji kuchemka, shuka ukafanye jina lako lijulikane kwa adui zako, na kusababisha mataifa yatetemeke mbele zako!
and failiden as brennyng of fier, and brente in fier; that thi name were made knowun to thin enemyes, and folkis weren disturblid of thi face.
3 Kwa maana ulipofanya mambo ya kutisha ambayo hatukuyatazamia, ulishuka, nayo milima ikatetemeka mbele zako.
Whanne thou schalt do merueils, we schulen not abide. Thou camest doun, and hillis fletiden awei fro thi face.
4 Tangu nyakati za zamani hakuna yeyote aliyesikia, hakuna sikio lililotambua, hakuna jicho lililomwona Mungu mwingine ila wewe, anayetenda mambo kwa ajili ya wale wamngojeao.
Fro the world thei herden not, nethir perseyueden with eeris; God, non iye siy, withouten thee, what thingis thou hast maad redi to hem that abiden thee.
5 Uliwasaidia watu wale watendao yaliyo haki kwa furaha, wale wazikumbukao njia zako. Lakini wakati tulipoendelea kutenda dhambi kinyume na njia zako, ulikasirika. Tutawezaje basi kuokolewa?
Thou mettist hym that is glad, and doith riytfulnesse; in thi weies thei schulen bithenke on thee. Lo! thou art wrooth, and we synneden; in tho synnes we weren euere, and we schulen be saued.
6 Sisi sote tumekuwa kama mtu aliye najisi, nayo matendo yetu yote ya uadilifu ni kama matambaa machafu; sisi sote tunasinyaa kama jani, na kama upepo maovu yetu hutupeperusha.
And alle we ben maad as an vncleene man; alle oure riytfulnessis ben as the cloth of a womman in vncleene blood; and alle we fellen doun as a leef, and our wickidnessis as wynd han take awei vs.
7 Hakuna yeyote anayeliitia jina lako wala anayejitahidi kukushika, kwa kuwa umetuficha uso wako na kutuacha tudhoofike kwa sababu ya dhambi zetu.
Noon is, that clepith thi name to help, that risith, and holdith thee; thou hast hid thi face fro vs, and thou hast hurtlid doun vs in the hond of oure wickidnesse.
8 Lakini, Ee Bwana, wewe ndiwe Baba yetu. Sisi ni udongo, wewe ndiye mfinyanzi; sisi sote tu kazi ya mkono wako.
And now, Lord, thou art oure fadir; forsothe we ben cley, and thou art oure maker, and alle we ben the werkis of thin hondis.
9 Ee Bwana, usikasirike kupita kiasi, usizikumbuke dhambi zetu milele. Ee Bwana, utuangalie, twakuomba, kwa kuwa sisi sote tu watu wako.
Lord, be thou not wrooth ynow, and haue thou no more mynde on oure wickidnesse. Lo! Lord, biholde thou, alle we ben thi puple.
10 Miji yako mitakatifu imekuwa jangwa; hata Sayuni ni jangwa, Yerusalemu ni ukiwa.
The citee of thi seyntuarie is forsakun, Sion is maad deseert, Jerusalem is desolat;
11 Hekalu letu takatifu na tukufu, mahali ambapo baba zetu walikusifu wewe, limechomwa kwa moto, navyo vitu vyote tulivyovithamini vimeharibika.
the hous of oure halewyng and of oure glorie, where oure fadris herieden thee, is maad in to brennyng of fier; and alle oure desirable thingis ben turned in to fallyngis.
12 Ee Bwana, baada ya haya yote, utajizuia? Je, utanyamaza kimya na kutuadhibu kupita kiasi?
Lord, whether on these thingis thou schalt witholde thee? schalt thou be stille, and schalt thou turmente vs greetli?

< Isaya 64 >