< Isaya 63 >
1 Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu? Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari, anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake? “Mimi ndimi, nisemaye katika haki, mwenye nguvu wa kuokoa.”
Kim jest ten, który przybywa z Edomu, w farbowanych szatach z Bosry? Ten wspaniały w swoich szatach, kroczący w swojej wielkiej mocy? To ja jestem, który mówię w sprawiedliwości, potężny w wybawieniu.
2 Kwa nini mavazi yako ni mekundu, kama ya yule akanyagaye shinikizo la zabibu?
Dlaczego twoja odzież jest czerwona? A twoje szaty jak u tego, który tłoczy w prasie?
3 “Nimekanyaga shinikizo la zabibu peke yangu; kutoka mataifa hakuna mtu aliyekuwa pamoja nami. Nimewaponda kwa miguu katika hasira yangu na kuwakanyaga chini katika ghadhabu yangu; damu yao ilitia matone kwenye mavazi yangu, na kutia madoa nguo zangu zote.
Sam jeden tłoczyłem prasę i spośród ludu nie było ze mną nikogo. Tłoczyłem go w swoim gniewie i deptałem go w swojej zapalczywości, aż pryskała jego krew na moje szaty, poplamiłem całą swą odzież.
4 Kwa kuwa siku ya kisasi ilikuwa moyoni mwangu, mwaka wa ukombozi wangu umefika.
Dzień pomsty był bowiem w moim sercu, a rok moich odkupionych nadszedł.
5 Nilitazama, lakini hakuwepo yeyote wa kunisaidia, nilishangaa kwa kuwa hakuwepo yeyote aliyetoa msaada; hivyo mkono wangu wenyewe ndio ulionifanyia wokovu, na ghadhabu yangu mwenyewe ndiyo iliyonitegemeza.
Rozglądałem się, ale nie było pomocnika, zdumiałem się, że nikogo nie było, kto by mnie podparł. Dlatego moje ramię przyniosło mi zbawienie, a moja zapalczywość – ona mnie podparła.
6 Nilikanyaga mataifa kwa miguu katika hasira yangu, katika ghadhabu yangu niliwalewesha, na kumwaga damu yao juu ya ardhi.”
Zdeptałem narody w swoim gniewie, upoiłem je w swojej zapalczywości i uderzyłem o ziemię ich mocarzy.
7 Nitasimulia juu ya wema wa Bwana, kwa matendo ambayo apaswa kusifiwa, sawasawa na yote ambayo Bwana ametenda kwa ajili yetu: naam, mambo mengi mema aliyoyatenda kwa ajili ya nyumba ya Israeli, sawasawa na huruma zake na wema wake mwingi.
Będę wspominać miłosierdzie PANA i chwałę PANA za wszystko, co nam PAN wyświadczył, i za wielką dobroć, którą okazał domowi Izraela według swego miłosierdzia i według swojej wielkiej łaskawości.
8 Alisema, “Hakika wao ni watu wangu, wana ambao hawatanidanganya”; hivyo akawa Mwokozi wao.
Powiedział bowiem: Na pewno są moim ludem, synami, którzy mi się nie sprzeniewierzą. I tak stał się ich Zbawicielem.
9 Katika taabu zao zote naye alitaabika, na malaika wa uso wake akawaokoa. Katika upendo wake na rehema zake aliwakomboa, akawainua na kuwachukua siku zote zilizopita.
We wszelkim ich ucisku i on był uciśniony, a Anioł jego oblicza zbawił ich. W swojej miłości i litości on ich odkupił. Troszczył się o nich i nosił ich przez wszystkie dni wieków.
10 Lakini waliasi, na kumhuzunisha Roho Mtakatifu wake. Hivyo aligeuka na kuwa adui yao, na yeye mwenyewe akapigana dhidi yao.
Ale oni się zbuntowali i zasmucili jego Świętego Ducha. Dlatego zamienił się w ich wroga i walczył przeciwko nim.
11 Ndipo watu wake wakazikumbuka siku zilizopita, siku za Mose na watu wake: yuko wapi yeye aliyewaleta kupitia katikati ya bahari, pamoja na wachungaji wa kundi lake? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mtakatifu katikati yao,
Wówczas wspomniał dawne dni, Mojżesza i jego lud, mówiąc: Gdzież jest ten, który ich wyprowadził z morza, z pasterzem swojej trzody? Gdzież jest ten, który włożył w jego wnętrze swego Świętego Ducha?
12 aliyetuma mkono wake uliotukuka wenye nguvu kuwa katika mkono wa kuume wa Mose, aliyegawa maji ya bahari mbele yao, ili kujipatia jina milele,
Który prowadził ich prawicą Mojżesza dzięki swemu chwalebnemu ramieniu i rozdzielił wody przed nimi, aby uczynić sobie wieczne imię?
13 aliyewaongoza kupitia kwenye vilindi? Kama farasi katika nchi iliyo wazi, wao hawakujikwaa,
Który ich przeprowadził przez głębiny, jak konia na pustyni, tak że się nie potknęli?
14 kama ngʼombe washukao bondeni kwenye malisho, walipewa pumziko na Roho wa Bwana. Hivi ndivyo ulivyowaongoza watu wako ili kujipatia mwenyewe jina tukufu.
Jak bydło schodzące w dolinę tak Duch PANA spokojnie ich prowadził. Tak prowadziłeś swój lud, aby uczynić sobie chwalebne imię.
15 Tazama chini kutoka mbinguni ukaone kutoka kiti chako cha enzi kilichoinuliwa juu, kitakatifu na kitukufu. Uko wapi wivu wako na uweza wako? Umetuzuilia wema wako na huruma zako.
Spójrz z nieba i popatrz z przybytku swojej świętości i chwały. Gdzie twoja gorliwość i twoja wielka siła? Gdzie poruszenie twoich uczuć i litości przede mną? Czy powstrzymałeś [je]?
16 Lakini wewe ni Baba yetu, ingawa Abrahamu hatufahamu sisi wala Israeli hatutambui; wewe, Ee Bwana, ndiwe Baba yetu, Mkombozi wetu tangu zamani za kale ndilo jina lako.
Przecież ty jesteś naszym ojcem, bo Abraham nas nie zna, a Izrael nas nie uznaje. Ty, PANIE, jesteś naszym ojcem, naszym Odkupicielem; twoje imię jest od wieków.
17 Ee Bwana, kwa nini unatuacha twende mbali na njia zako, na kuifanya mioyo yetu migumu hata hatukukuheshimu? Rudi kwa ajili ya watumishi wako, yale makabila ambayo ni urithi wako.
Czemu, PANIE, pozwoliłeś nam zboczyć z twoich dróg i zatwardziłeś nasze serce, abyśmy się ciebie nie bali? Odwróć się ze względu na twoje sługi, pokolenia twego dziedzictwa.
18 Kwa maana kwa muda mfupi watu wako walimiliki mahali pako patakatifu, lakini sasa adui zetu wamepakanyaga mahali patakatifu pako.
Lud posiadł [ją] na krótki [czas], nasi wrogowie zaś zdeptali twoją świątynię.
19 Sisi tumekuwa kama wale ambao hujawatawala kamwe, kama wale ambao hawajaitwa kwa jina lako.
My jesteśmy twoi. Nad nimi nigdy nie panowałeś ani nie byli nazywani twoimi imieniem.