< Isaya 63 >

1 Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu? Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari, anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake? “Mimi ndimi, nisemaye katika haki, mwenye nguvu wa kuokoa.”
Who is this that cometh fro Edom, in died clothis fro Bosra? this fair man in his `long cloth, goynge in the multitude of his vertu? Y that speke riytfulnesse, and am a forfiytere for to saue.
2 Kwa nini mavazi yako ni mekundu, kama ya yule akanyagaye shinikizo la zabibu?
Whi therfor is thi clothing reed? and thi clothis ben as of men stampynge in a pressour?
3 “Nimekanyaga shinikizo la zabibu peke yangu; kutoka mataifa hakuna mtu aliyekuwa pamoja nami. Nimewaponda kwa miguu katika hasira yangu na kuwakanyaga chini katika ghadhabu yangu; damu yao ilitia matone kwenye mavazi yangu, na kutia madoa nguo zangu zote.
Y aloone stampide the presse, and of folkis no man is with me; Y stampide hem in my stronge veniaunce, and Y defoulide hem in my wraththe; and her blood is spreynt on my clothis, and Y made foul alle my clothis.
4 Kwa kuwa siku ya kisasi ilikuwa moyoni mwangu, mwaka wa ukombozi wangu umefika.
For whi a dai of veniaunce is in myn herte, and the yeer of my yeldyng cometh.
5 Nilitazama, lakini hakuwepo yeyote wa kunisaidia, nilishangaa kwa kuwa hakuwepo yeyote aliyetoa msaada; hivyo mkono wangu wenyewe ndio ulionifanyia wokovu, na ghadhabu yangu mwenyewe ndiyo iliyonitegemeza.
I lokide aboute, and noon helpere was; Y souyte, and noon was that helpide; and myn arm sauyde to me, and myn indignacioun, that helpide me.
6 Nilikanyaga mataifa kwa miguu katika hasira yangu, katika ghadhabu yangu niliwalewesha, na kumwaga damu yao juu ya ardhi.”
And Y defoulide puplis in my stronge veniaunce; and Y made hem drunkun in myn indignacioun, and Y drow doun her vertu in to erthe.
7 Nitasimulia juu ya wema wa Bwana, kwa matendo ambayo apaswa kusifiwa, sawasawa na yote ambayo Bwana ametenda kwa ajili yetu: naam, mambo mengi mema aliyoyatenda kwa ajili ya nyumba ya Israeli, sawasawa na huruma zake na wema wake mwingi.
I schal haue mynde on the merciful doyngis of the Lord, Y schal preche the heriyng of the Lord on alle thingis whiche the Lord yeldide to vs, and on the multitude `of goodis of the hous of Israel, whiche he yaf to hem bi his foryyuenesse, and bi the multitude of hise mercies.
8 Alisema, “Hakika wao ni watu wangu, wana ambao hawatanidanganya”; hivyo akawa Mwokozi wao.
And the Lord seide, Netheles it is my puple, sones not denyynge, and he was maad a sauyour to hem in al the tribulacioun of hem.
9 Katika taabu zao zote naye alitaabika, na malaika wa uso wake akawaokoa. Katika upendo wake na rehema zake aliwakomboa, akawainua na kuwachukua siku zote zilizopita.
It was not set in tribulacioun, and the aungel of his face sauyde hem. In his loue and in his foryyuenesse he ayenbouyte hem, and he bar hem, and reiside hem in alle daies of the world.
10 Lakini waliasi, na kumhuzunisha Roho Mtakatifu wake. Hivyo aligeuka na kuwa adui yao, na yeye mwenyewe akapigana dhidi yao.
Forsothe thei excitiden hym to wrathfulnesse, and turmentiden the spirit of his hooli; and he was turned in to an enemye to hem, and he ouercam hem in batel.
11 Ndipo watu wake wakazikumbuka siku zilizopita, siku za Mose na watu wake: yuko wapi yeye aliyewaleta kupitia katikati ya bahari, pamoja na wachungaji wa kundi lake? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mtakatifu katikati yao,
And he hadde mynde on the daies of the world, of Moises, and of his puple. Where is he, that ledde hem out of the see, with the scheepherdis of his floc? Where is he, that settide the spirit of his holi in the myddil therof;
12 aliyetuma mkono wake uliotukuka wenye nguvu kuwa katika mkono wa kuume wa Mose, aliyegawa maji ya bahari mbele yao, ili kujipatia jina milele,
whiche ledde out Moises to the riyt half in the arm of his maieste? which departide watris bifore hem, that he schulde make to hym silf a name euerlastynge;
13 aliyewaongoza kupitia kwenye vilindi? Kama farasi katika nchi iliyo wazi, wao hawakujikwaa,
whiche ledde hem out thoruy depthis of watris, as an hors not stumblynge in desert,
14 kama ngʼombe washukao bondeni kwenye malisho, walipewa pumziko na Roho wa Bwana. Hivi ndivyo ulivyowaongoza watu wako ili kujipatia mwenyewe jina tukufu.
as a beeste goynge doun in the feeld? The Spirit of the Lord was the ledere therof; so thou leddist thi puple, that thou madist to thee a name of glorie.
15 Tazama chini kutoka mbinguni ukaone kutoka kiti chako cha enzi kilichoinuliwa juu, kitakatifu na kitukufu. Uko wapi wivu wako na uweza wako? Umetuzuilia wema wako na huruma zako.
Biholde thou fro heuene, and se fro thin hooli dwellyng place, and fro the seete of thi glorie. Where is thi feruent loue, and thi strengthe, the multitude of thin entrailis, and of thi merciful doyngis?
16 Lakini wewe ni Baba yetu, ingawa Abrahamu hatufahamu sisi wala Israeli hatutambui; wewe, Ee Bwana, ndiwe Baba yetu, Mkombozi wetu tangu zamani za kale ndilo jina lako.
Tho withelden hem silf on me. Forsothe thou art oure fadir, and Abraham knew not vs, and Israel knew not vs.
17 Ee Bwana, kwa nini unatuacha twende mbali na njia zako, na kuifanya mioyo yetu migumu hata hatukukuheshimu? Rudi kwa ajili ya watumishi wako, yale makabila ambayo ni urithi wako.
Thou, Lord, art oure fadir, and oure ayenbiere; thi name is fro the world. Lord, whi hast thou maad vs to erre fro thi weies? thou hast made hard oure herte, that we dredden not thee? be thou conuertid, for thi seruauntis, the lynages of thin eritage.
18 Kwa maana kwa muda mfupi watu wako walimiliki mahali pako patakatifu, lakini sasa adui zetu wamepakanyaga mahali patakatifu pako.
Thei hadden as nouyt thin hooli puple in possessioun, and oure enemyes defouliden thin halewyng.
19 Sisi tumekuwa kama wale ambao hujawatawala kamwe, kama wale ambao hawajaitwa kwa jina lako.
We ben maad as in the bigynnyng, whanne thou were not Lord of vs, nethir thi name was clepid to help on vs.

< Isaya 63 >