< Isaya 63 >
1 Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu? Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari, anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake? “Mimi ndimi, nisemaye katika haki, mwenye nguvu wa kuokoa.”
who? this to come (in): come from Edom be red garment from Bozrah this to honor in/on/with clothing his to march in/on/with abundance strength his I to speak: speak in/on/with righteousness many to/for to save
2 Kwa nini mavazi yako ni mekundu, kama ya yule akanyagaye shinikizo la zabibu?
why? red to/for clothing your and garment your like/as to tread in/on/with wine press
3 “Nimekanyaga shinikizo la zabibu peke yangu; kutoka mataifa hakuna mtu aliyekuwa pamoja nami. Nimewaponda kwa miguu katika hasira yangu na kuwakanyaga chini katika ghadhabu yangu; damu yao ilitia matone kwenye mavazi yangu, na kutia madoa nguo zangu zote.
winepress to tread to/for alone me and from people nothing man: anyone with me and to tread them in/on/with face: anger my and to trample them in/on/with rage my and to sprinkle lifeblood their upon garment my and all garment my to defile
4 Kwa kuwa siku ya kisasi ilikuwa moyoni mwangu, mwaka wa ukombozi wangu umefika.
for day vengeance in/on/with heart my and year redemption my to come (in): come
5 Nilitazama, lakini hakuwepo yeyote wa kunisaidia, nilishangaa kwa kuwa hakuwepo yeyote aliyetoa msaada; hivyo mkono wangu wenyewe ndio ulionifanyia wokovu, na ghadhabu yangu mwenyewe ndiyo iliyonitegemeza.
and to look and nothing to help and be desolate: appalled and nothing to support and to save to/for me arm my and rage my he/she/it to support me
6 Nilikanyaga mataifa kwa miguu katika hasira yangu, katika ghadhabu yangu niliwalewesha, na kumwaga damu yao juu ya ardhi.”
and to trample people in/on/with face: anger my and be drunk them in/on/with rage my and to go down to/for land: country/planet lifeblood their
7 Nitasimulia juu ya wema wa Bwana, kwa matendo ambayo apaswa kusifiwa, sawasawa na yote ambayo Bwana ametenda kwa ajili yetu: naam, mambo mengi mema aliyoyatenda kwa ajili ya nyumba ya Israeli, sawasawa na huruma zake na wema wake mwingi.
kindness LORD to remember praise LORD like/as upon all which to wean us LORD and many goodness to/for house: household Israel which to wean them like/as compassion his and like/as abundance kindness his
8 Alisema, “Hakika wao ni watu wangu, wana ambao hawatanidanganya”; hivyo akawa Mwokozi wao.
and to say surely people my they(masc.) son: child not to deal and to be to/for them to/for to save
9 Katika taabu zao zote naye alitaabika, na malaika wa uso wake akawaokoa. Katika upendo wake na rehema zake aliwakomboa, akawainua na kuwachukua siku zote zilizopita.
in/on/with all distress their (to/for him *Q(K)*) distress and messenger: angel face his to save them in/on/with love his and in/on/with compassion his he/she/it to redeem: redeem them and to lift them and to lift: bear them all day forever: antiquity
10 Lakini waliasi, na kumhuzunisha Roho Mtakatifu wake. Hivyo aligeuka na kuwa adui yao, na yeye mwenyewe akapigana dhidi yao.
and they(masc.) to rebel and to hurt [obj] spirit holiness his and to overturn to/for them to/for enemy he/she/it to fight in/on/with them
11 Ndipo watu wake wakazikumbuka siku zilizopita, siku za Mose na watu wake: yuko wapi yeye aliyewaleta kupitia katikati ya bahari, pamoja na wachungaji wa kundi lake? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mtakatifu katikati yao,
and to remember day forever: antiquity Moses people his where? [the] to ascend: rise them from sea with to pasture flock his where? [the] to set: put in/on/with entrails: among his [obj] spirit holiness his
12 aliyetuma mkono wake uliotukuka wenye nguvu kuwa katika mkono wa kuume wa Mose, aliyegawa maji ya bahari mbele yao, ili kujipatia jina milele,
to go: went to/for right Moses arm beauty his to break up/open water from face: before their to/for to make to/for him name forever: enduring
13 aliyewaongoza kupitia kwenye vilindi? Kama farasi katika nchi iliyo wazi, wao hawakujikwaa,
to go: take them in/on/with abyss like/as horse in/on/with wilderness not to stumble
14 kama ngʼombe washukao bondeni kwenye malisho, walipewa pumziko na Roho wa Bwana. Hivi ndivyo ulivyowaongoza watu wako ili kujipatia mwenyewe jina tukufu.
like/as animal in/on/with valley to go down spirit LORD to rest him so to lead people your to/for to make to/for you name beauty
15 Tazama chini kutoka mbinguni ukaone kutoka kiti chako cha enzi kilichoinuliwa juu, kitakatifu na kitukufu. Uko wapi wivu wako na uweza wako? Umetuzuilia wema wako na huruma zako.
to look from heaven and to see: see from elevation holiness your and beauty your where? jealousy your and might your crowd belly your and compassion your to(wards) me to refrain
16 Lakini wewe ni Baba yetu, ingawa Abrahamu hatufahamu sisi wala Israeli hatutambui; wewe, Ee Bwana, ndiwe Baba yetu, Mkombozi wetu tangu zamani za kale ndilo jina lako.
for you(m. s.) father our for Abraham not to know us and Israel not to recognize us you(m. s.) LORD father our to redeem: redeem our from forever: antiquity name your
17 Ee Bwana, kwa nini unatuacha twende mbali na njia zako, na kuifanya mioyo yetu migumu hata hatukukuheshimu? Rudi kwa ajili ya watumishi wako, yale makabila ambayo ni urithi wako.
to/for what? to go astray us LORD from way: conduct your to harden heart our from fear your to return: return because servant/slave your tribe inheritance your
18 Kwa maana kwa muda mfupi watu wako walimiliki mahali pako patakatifu, lakini sasa adui zetu wamepakanyaga mahali patakatifu pako.
to/for little to possess: possess people holiness your enemy our to trample sanctuary your
19 Sisi tumekuwa kama wale ambao hujawatawala kamwe, kama wale ambao hawajaitwa kwa jina lako.
to be from forever: antiquity not to rule in/on/with them not to call: call by name your upon them