< Isaya 63 >

1 Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu? Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari, anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake? “Mimi ndimi, nisemaye katika haki, mwenye nguvu wa kuokoa.”
Who? this - [is] coming from Edom red of garments from Bozrah this one [is] adorned in clothing his [is] stooping in [the] greatness of strength his I [am] speaking in righteousness great to save.
2 Kwa nini mavazi yako ni mekundu, kama ya yule akanyagaye shinikizo la zabibu?
Why? [does] redness [belong] to clothing your and [are] garments? your like [one who] treads in a winepress.
3 “Nimekanyaga shinikizo la zabibu peke yangu; kutoka mataifa hakuna mtu aliyekuwa pamoja nami. Nimewaponda kwa miguu katika hasira yangu na kuwakanyaga chini katika ghadhabu yangu; damu yao ilitia matone kwenye mavazi yangu, na kutia madoa nguo zangu zote.
[the] winepress - I have trodden to alone me and from peoples not anyone [was] with me and I trod them in anger my and I trampled them in rage my and it spattered blood their on garments my and all clothes my I have defiled.
4 Kwa kuwa siku ya kisasi ilikuwa moyoni mwangu, mwaka wa ukombozi wangu umefika.
For a day of vengeance [was] in heart my and [the] year of redemption my it had come.
5 Nilitazama, lakini hakuwepo yeyote wa kunisaidia, nilishangaa kwa kuwa hakuwepo yeyote aliyetoa msaada; hivyo mkono wangu wenyewe ndio ulionifanyia wokovu, na ghadhabu yangu mwenyewe ndiyo iliyonitegemeza.
And I may look and there not [was] a helper and I may be appalled and there not [was] a sustainer and it gave victory to me arm my and rage my it it sustained me.
6 Nilikanyaga mataifa kwa miguu katika hasira yangu, katika ghadhabu yangu niliwalewesha, na kumwaga damu yao juu ya ardhi.”
And I may tread down peoples in anger my and I made drunk them in rage my so I may bring down to the ground blood their.
7 Nitasimulia juu ya wema wa Bwana, kwa matendo ambayo apaswa kusifiwa, sawasawa na yote ambayo Bwana ametenda kwa ajili yetu: naam, mambo mengi mema aliyoyatenda kwa ajili ya nyumba ya Israeli, sawasawa na huruma zake na wema wake mwingi.
[the] covenant loyalti of Yahweh - I will bring to remembrance [the] praises of Yahweh as on all that he has dealt out to us Yahweh and [the] greatness of goodness to [the] house of Israel which he has dealt out to them according to compassion his and according to [the] greatness of covenant loyalti his.
8 Alisema, “Hakika wao ni watu wangu, wana ambao hawatanidanganya”; hivyo akawa Mwokozi wao.
And he said surely [are] people my they children [who] not they will deal falsely and he became of them a deliverer.
9 Katika taabu zao zote naye alitaabika, na malaika wa uso wake akawaokoa. Katika upendo wake na rehema zake aliwakomboa, akawainua na kuwachukua siku zote zilizopita.
In all distress their - ([belonged] to him *Q(K)*) distress and [the] angel of presence his it saved them in love his and in mercy his he he redeemed them and he lifted up them and he carried them all [the] days of antiquity.
10 Lakini waliasi, na kumhuzunisha Roho Mtakatifu wake. Hivyo aligeuka na kuwa adui yao, na yeye mwenyewe akapigana dhidi yao.
And they they rebelled and they grieved [the] spirit of holiness his and he changed himself of them into an enemy he he fought against them.
11 Ndipo watu wake wakazikumbuka siku zilizopita, siku za Mose na watu wake: yuko wapi yeye aliyewaleta kupitia katikati ya bahari, pamoja na wachungaji wa kundi lake? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mtakatifu katikati yao,
And it remembered [the] days of antiquity Moses people his where? - [is] who brought up them from [the] sea with [the] shepherds of flock his where? [is] the [one who] put in midst its [the] spirit of holiness his.
12 aliyetuma mkono wake uliotukuka wenye nguvu kuwa katika mkono wa kuume wa Mose, aliyegawa maji ya bahari mbele yao, ili kujipatia jina milele,
[who] caused to go To [the] right [hand] of Moses [the] arm of splendor his [who] split open [the] waters from before them to make for himself a name of perpetuity.
13 aliyewaongoza kupitia kwenye vilindi? Kama farasi katika nchi iliyo wazi, wao hawakujikwaa,
[who] caused to walk Them in the deeps like horse in the wilderness not they stumbled.
14 kama ngʼombe washukao bondeni kwenye malisho, walipewa pumziko na Roho wa Bwana. Hivi ndivyo ulivyowaongoza watu wako ili kujipatia mwenyewe jina tukufu.
Like livestock [which] in the valley it goes down [the] spirit of Yahweh it gave rest it so you led people your to make for yourself a name of splendor.
15 Tazama chini kutoka mbinguni ukaone kutoka kiti chako cha enzi kilichoinuliwa juu, kitakatifu na kitukufu. Uko wapi wivu wako na uweza wako? Umetuzuilia wema wako na huruma zako.
Look from heaven and see from [the] lofty abode of holiness your and splendor your where? [are] zeal your and mighty deeds your [the] tumult of inward parts your and compassion your to me they have restrained themselves.
16 Lakini wewe ni Baba yetu, ingawa Abrahamu hatufahamu sisi wala Israeli hatutambui; wewe, Ee Bwana, ndiwe Baba yetu, Mkombozi wetu tangu zamani za kale ndilo jina lako.
For you [are] father our for Abraham not he knows us and Israel not he acknowledges us you O Yahweh [are] father our [is] redeemer our from long ago name your.
17 Ee Bwana, kwa nini unatuacha twende mbali na njia zako, na kuifanya mioyo yetu migumu hata hatukukuheshimu? Rudi kwa ajili ya watumishi wako, yale makabila ambayo ni urithi wako.
Why? do you make wander us O Yahweh from ways your do you harden? heart our from fear of you return for [the] sake of servants your [the] tribes of inheritance your.
18 Kwa maana kwa muda mfupi watu wako walimiliki mahali pako patakatifu, lakini sasa adui zetu wamepakanyaga mahali patakatifu pako.
For little while they possessed [the] people of holiness your opponents our they have trodden down sanctuary your.
19 Sisi tumekuwa kama wale ambao hujawatawala kamwe, kama wale ambao hawajaitwa kwa jina lako.
We have been from long ago not you ruled over them not it was called name your on them

< Isaya 63 >