< Isaya 63 >

1 Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu? Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari, anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake? “Mimi ndimi, nisemaye katika haki, mwenye nguvu wa kuokoa.”
Who [is] this coming from Edom? With dyed garments from Bozrah? This that is honorable in His clothing, Traveling in the abundance of His power? “I, speaking in righteousness, mighty to save.”
2 Kwa nini mavazi yako ni mekundu, kama ya yule akanyagaye shinikizo la zabibu?
Why [is] Your clothing red? And Your garments as treading in a winepress?
3 “Nimekanyaga shinikizo la zabibu peke yangu; kutoka mataifa hakuna mtu aliyekuwa pamoja nami. Nimewaponda kwa miguu katika hasira yangu na kuwakanyaga chini katika ghadhabu yangu; damu yao ilitia matone kwenye mavazi yangu, na kutia madoa nguo zangu zote.
“I have trodden a wine vat by Myself, And of the peoples there is no one with Me, And I tread them in My anger, And I trample them in My fury, Their strength is sprinkled on My garments, And I have defiled all My clothing.
4 Kwa kuwa siku ya kisasi ilikuwa moyoni mwangu, mwaka wa ukombozi wangu umefika.
For the day of vengeance [is] in My heart, And the year of My redeemed has come.
5 Nilitazama, lakini hakuwepo yeyote wa kunisaidia, nilishangaa kwa kuwa hakuwepo yeyote aliyetoa msaada; hivyo mkono wangu wenyewe ndio ulionifanyia wokovu, na ghadhabu yangu mwenyewe ndiyo iliyonitegemeza.
And I look attentively, and there is none helping, And I am astonished that there is none supporting, And My own arm gives salvation to Me. And My wrath—it has supported Me.
6 Nilikanyaga mataifa kwa miguu katika hasira yangu, katika ghadhabu yangu niliwalewesha, na kumwaga damu yao juu ya ardhi.”
And I tread down peoples in My anger, And I make them drunk in My fury, And I bring down their strength to earth.”
7 Nitasimulia juu ya wema wa Bwana, kwa matendo ambayo apaswa kusifiwa, sawasawa na yote ambayo Bwana ametenda kwa ajili yetu: naam, mambo mengi mema aliyoyatenda kwa ajili ya nyumba ya Israeli, sawasawa na huruma zake na wema wake mwingi.
I make mention of the kind acts of YHWH, The praises of YHWH, According to all that YHWH has done for us, And the abundance of the goodness to the house of Israel, That He has done for them, According to His mercies, And according to the abundance of His kind acts.
8 Alisema, “Hakika wao ni watu wangu, wana ambao hawatanidanganya”; hivyo akawa Mwokozi wao.
And He says, “Surely they [are] My people, Sons—they do not lie,” and He is to them for a Savior.
9 Katika taabu zao zote naye alitaabika, na malaika wa uso wake akawaokoa. Katika upendo wake na rehema zake aliwakomboa, akawainua na kuwachukua siku zote zilizopita.
In all their distress [He is] no adversary, And the Messenger of His Presence saved them, In His love and in His pity He redeemed them, And He lifts them up, And carries them all the days of old.
10 Lakini waliasi, na kumhuzunisha Roho Mtakatifu wake. Hivyo aligeuka na kuwa adui yao, na yeye mwenyewe akapigana dhidi yao.
And they have been rebellious and have grieved His Holy Spirit, And He turns to them for an enemy, He Himself has fought against them.
11 Ndipo watu wake wakazikumbuka siku zilizopita, siku za Mose na watu wake: yuko wapi yeye aliyewaleta kupitia katikati ya bahari, pamoja na wachungaji wa kundi lake? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mtakatifu katikati yao,
And He remembers the days of old, Moses—his people. Where [is] He who is bringing them up from the sea, The shepherd of His flock? Where [is] He who is putting in its midst His Holy Spirit?
12 aliyetuma mkono wake uliotukuka wenye nguvu kuwa katika mkono wa kuume wa Mose, aliyegawa maji ya bahari mbele yao, ili kujipatia jina milele,
Leading by the right hand of Moses, the arm of His glory, Cleaving waters from before them, To make to Himself a continuous Name.
13 aliyewaongoza kupitia kwenye vilindi? Kama farasi katika nchi iliyo wazi, wao hawakujikwaa,
Leading them through the depths, They do not stumble as a horse in a plain.
14 kama ngʼombe washukao bondeni kwenye malisho, walipewa pumziko na Roho wa Bwana. Hivi ndivyo ulivyowaongoza watu wako ili kujipatia mwenyewe jina tukufu.
As a beast goes down into a valley, The Spirit of YHWH causes him to rest, So You have led Your people, To make to Yourself a glorious Name.
15 Tazama chini kutoka mbinguni ukaone kutoka kiti chako cha enzi kilichoinuliwa juu, kitakatifu na kitukufu. Uko wapi wivu wako na uweza wako? Umetuzuilia wema wako na huruma zako.
Look attentively from the heavens, And see from Your holy and beautiful habitation, Where [is] Your zeal and Your might? The multitude of Your bowels and Your mercies—Are they restrained?
16 Lakini wewe ni Baba yetu, ingawa Abrahamu hatufahamu sisi wala Israeli hatutambui; wewe, Ee Bwana, ndiwe Baba yetu, Mkombozi wetu tangu zamani za kale ndilo jina lako.
For You [are] our Father, For Abraham has not known us, And Israel does not acknowledge us, You, O YHWH, [are] our Father, Our Redeemer from the Age, [is] Your Name.
17 Ee Bwana, kwa nini unatuacha twende mbali na njia zako, na kuifanya mioyo yetu migumu hata hatukukuheshimu? Rudi kwa ajili ya watumishi wako, yale makabila ambayo ni urithi wako.
Why cause us to wander, O YHWH, from Your ways? You harden our heart from Your fear, Turn back for Your servants’ sake, The tribes of Your inheritance.
18 Kwa maana kwa muda mfupi watu wako walimiliki mahali pako patakatifu, lakini sasa adui zetu wamepakanyaga mahali patakatifu pako.
For a little while Your holy people possessed, Our adversaries have trodden down Your sanctuary.
19 Sisi tumekuwa kama wale ambao hujawatawala kamwe, kama wale ambao hawajaitwa kwa jina lako.
We have been from of old, You have not ruled over them, Your Name is not called on them!

< Isaya 63 >