< Isaya 61 >

1 Roho wa Bwana Mwenyezi yu juu yangu, kwa sababu Bwana amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao;
The spirit of the Lord Jehovah is upon me, For Jehovah hath anointed me; He hath sent me to publish good tidings to the distressed, To bind up the broken-hearted, To proclaim liberty to the captives, And the opening of the prison to them that are bound;
2 kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi ya Mungu wetu, kuwafariji wote waombolezao,
To proclaim the year of mercy from Jehovah, And the day of vengeance from our God; To comfort all that mourn;
3 na kuwapa mahitaji wale wanaohuzunika katika Sayuni, ili kuwapa taji ya uzuri badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho ya kukata tamaa. Nao wataitwa mialoni ya haki, pando la Bwana, ili kuonyesha utukufu wake.
To give gladness to the mourners in Zion; To give them a beautiful crown instead of ashes, The oil of joy for mourning, The garment of praise for the spirit of heaviness, So that they shall be called blessed terebinth-trees, The plantation of Jehovah for his glory.
4 Watajenga upya magofu ya zamani na kupatengeneza mahali palipoachwa ukiwa zamani; watafanya upya miji iliyoharibiwa, iliyoachwa ukiwa kwa vizazi vingi.
They shall build up the old ruins; They shall raise up the ancient desolations; They shall repair the cities laid waste, The desolations of many generations.
5 Wageni watayachunga makundi yenu, wageni watafanya kazi katika mashamba yenu, na kutunza mashamba yenu ya mizabibu.
Strangers shall stand up and feed your flocks, And the sons of the alien shall be your ploughmen and vine-dressers;
6 Nanyi mtaitwa makuhani wa Bwana, mtaitwa watumishi wa Mungu wetu. Mtakula utajiri wa mataifa, nanyi katika utajiri wao mtajisifu.
But ye shall be named the priests of Jehovah, Men shall call you the ministers of our God. Ye shall eat the riches of the nations, And in their glory shall ye make your boast.
7 Badala ya aibu yao watu wangu watapokea sehemu maradufu, na badala ya fedheha watafurahia katika urithi wao; hivyo watarithi sehemu maradufu katika nchi yao, nayo furaha ya milele itakuwa yao.
For your shame shall ye have a double reward; And for ignominy ye shall rejoice in your portion; Therefore in your land ye shall possess double; Everlasting joy shall be your portion.
8 “Kwa maana Mimi, Bwana, napenda haki, na ninachukia unyangʼanyi na uovu. Katika uaminifu wangu nitawapa malipo yao na kufanya agano la milele nao.
For I, Jehovah, love justice, I hate rapine and iniquity, I will give them their reward with faithfulness, And an everlasting covenant will I make with them.
9 Wazao wao watajulikana miongoni mwa mataifa, na uzao wao miongoni mwa kabila za watu. Wale wote watakaowaona watatambua kuwa ni taifa ambalo Bwana amelibariki.”
Their race shall be illustrious among the nations, And their offspring among the people; All that see them shall acknowledge That they are a race which Jehovah hath blessed.
10 Ninafurahia sana katika Bwana, nafsi yangu inashangilia katika Mungu wangu. Kwa maana amenivika mavazi ya wokovu, na kunipamba kwa joho la haki, kama vile bwana arusi apambavyo kichwa chake kama kuhani, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vito vyake vya thamani.
“I will greatly rejoice in Jehovah; My soul shall exult in my God; For he hath clothed me with the garments of salvation; He hath covered me with the mantle of deliverance. As the bridegroom decketh himself with his turban, And as the bride adorneth herself with her jewels.”
11 Kwa maana kama vile ardhi ifanyavyo chipukizi kuota, na bustani isababishavyo mbegu kuota, ndivyo Bwana Mwenyezi atafanya haki na sifa zichipuke mbele ya mataifa yote.
For as the earth putteth forth her shoots, And as a garden causeth its plants to spring forth, So shall the Lord Jehovah cause salvation to spring forth; And praise before all the nations.

< Isaya 61 >