< Isaya 61 >

1 Roho wa Bwana Mwenyezi yu juu yangu, kwa sababu Bwana amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao;
“[The] Spirit of Lord YHWH [is] on Me, Because YHWH anointed Me To proclaim tidings to the humble, He sent Me to bind the broken of heart, To proclaim liberty to the captives, And an opening of bands to [those] bound.
2 kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi ya Mungu wetu, kuwafariji wote waombolezao,
To proclaim the year of the favor of YHWH, And the day of vengeance of our God, To comfort all mourners.
3 na kuwapa mahitaji wale wanaohuzunika katika Sayuni, ili kuwapa taji ya uzuri badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho ya kukata tamaa. Nao wataitwa mialoni ya haki, pando la Bwana, ili kuonyesha utukufu wake.
To appoint to mourners in Zion, To give to them beauty instead of ashes, The oil of joy instead of mourning, A covering of praise for a faded spirit, And He is calling to them, Trees of righteousness, The planting of YHWH—to be beautified.”
4 Watajenga upya magofu ya zamani na kupatengeneza mahali palipoachwa ukiwa zamani; watafanya upya miji iliyoharibiwa, iliyoachwa ukiwa kwa vizazi vingi.
And they have built the ancient ruins, They raise up the desolations of the ancients, And they have renewed ruined cities, The desolations of generation and generation.
5 Wageni watayachunga makundi yenu, wageni watafanya kazi katika mashamba yenu, na kutunza mashamba yenu ya mizabibu.
And strangers have stood and fed your flock, And the sons of a foreigner [Are] your farmers and your vinedressers.
6 Nanyi mtaitwa makuhani wa Bwana, mtaitwa watumishi wa Mungu wetu. Mtakula utajiri wa mataifa, nanyi katika utajiri wao mtajisifu.
And you are called priests of YHWH, It is said of you [that you are] ministers of our God, You consume the strength of nations, And you boast yourselves in their glory.
7 Badala ya aibu yao watu wangu watapokea sehemu maradufu, na badala ya fedheha watafurahia katika urithi wao; hivyo watarithi sehemu maradufu katika nchi yao, nayo furaha ya milele itakuwa yao.
Instead of your shame—double [honor], And [instead of] confusion, They rejoice in their portion, Therefore they take possession in their land a second time, Continuous joy [is] for them.
8 “Kwa maana Mimi, Bwana, napenda haki, na ninachukia unyangʼanyi na uovu. Katika uaminifu wangu nitawapa malipo yao na kufanya agano la milele nao.
“For I [am] YHWH, loving judgment, Hating plunder for a burnt-offering, And I have given their wage in truth, And I make a perpetual covenant for them.
9 Wazao wao watajulikana miongoni mwa mataifa, na uzao wao miongoni mwa kabila za watu. Wale wote watakaowaona watatambua kuwa ni taifa ambalo Bwana amelibariki.”
And their seed has been known among the nations, And their offspring in the midst of the peoples, All their beholders acknowledge them, For they [are] a seed YHWH has blessed.”
10 Ninafurahia sana katika Bwana, nafsi yangu inashangilia katika Mungu wangu. Kwa maana amenivika mavazi ya wokovu, na kunipamba kwa joho la haki, kama vile bwana arusi apambavyo kichwa chake kama kuhani, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vito vyake vya thamani.
I greatly rejoice in YHWH, My soul rejoices in my God, For He clothed me with garments of salvation, [And] covered me with a robe of righteousness, As a bridegroom prepares ornaments, And as a bride puts on her jewels.
11 Kwa maana kama vile ardhi ifanyavyo chipukizi kuota, na bustani isababishavyo mbegu kuota, ndivyo Bwana Mwenyezi atafanya haki na sifa zichipuke mbele ya mataifa yote.
For as the earth brings forth her shoots, And as a garden causes its sown things to shoot up, So Lord YHWH causes righteousness and praise To shoot up before all the nations!

< Isaya 61 >