< Isaya 61 >

1 Roho wa Bwana Mwenyezi yu juu yangu, kwa sababu Bwana amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao;
The spirit of the Lord GOD is upon me; because the LORD hath anointed me to bring good tidings unto the humble; He hath sent me to bind up the broken-hearted, to proclaim liberty to the captives, and the opening of the eyes to them that are bound;
2 kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi ya Mungu wetu, kuwafariji wote waombolezao,
To proclaim the year of the LORD'S good pleasure, and the day of vengeance of our God; to comfort all that mourn;
3 na kuwapa mahitaji wale wanaohuzunika katika Sayuni, ili kuwapa taji ya uzuri badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho ya kukata tamaa. Nao wataitwa mialoni ya haki, pando la Bwana, ili kuonyesha utukufu wake.
To appoint unto them that mourn in Zion, to give unto them a garland for ashes, the oil of joy for mourning, the mantle of praise for the spirit of heaviness; that they might be called terebinths of righteousness, the planting of the LORD, wherein He might glory.
4 Watajenga upya magofu ya zamani na kupatengeneza mahali palipoachwa ukiwa zamani; watafanya upya miji iliyoharibiwa, iliyoachwa ukiwa kwa vizazi vingi.
And they shall build the old wastes, they shall raise up the former desolations, and they shall renew the waste cities, the desolations of many generations.
5 Wageni watayachunga makundi yenu, wageni watafanya kazi katika mashamba yenu, na kutunza mashamba yenu ya mizabibu.
And strangers shall stand and feed your flocks, and aliens shall be your plowmen and your vinedressers.
6 Nanyi mtaitwa makuhani wa Bwana, mtaitwa watumishi wa Mungu wetu. Mtakula utajiri wa mataifa, nanyi katika utajiri wao mtajisifu.
But ye shall be named the priests of the LORD, men shall call you the ministers of our God; ye shall eat the wealth of the nations, and in their splendour shall ye revel.
7 Badala ya aibu yao watu wangu watapokea sehemu maradufu, na badala ya fedheha watafurahia katika urithi wao; hivyo watarithi sehemu maradufu katika nchi yao, nayo furaha ya milele itakuwa yao.
For your shame which was double, and for that they rejoiced: 'Confusion is their portion'; therefore in their land they shall possess double, everlasting joy shall be unto them.
8 “Kwa maana Mimi, Bwana, napenda haki, na ninachukia unyangʼanyi na uovu. Katika uaminifu wangu nitawapa malipo yao na kufanya agano la milele nao.
For I the LORD love justice, I hate robbery with iniquity; and I will give them their recompense in truth, and I will make an everlasting covenant with them.
9 Wazao wao watajulikana miongoni mwa mataifa, na uzao wao miongoni mwa kabila za watu. Wale wote watakaowaona watatambua kuwa ni taifa ambalo Bwana amelibariki.”
And their seed shall be known among the nations, and their offspring among the peoples; all that see them shall acknowledge them, that they are the seed which the LORD hath blessed.
10 Ninafurahia sana katika Bwana, nafsi yangu inashangilia katika Mungu wangu. Kwa maana amenivika mavazi ya wokovu, na kunipamba kwa joho la haki, kama vile bwana arusi apambavyo kichwa chake kama kuhani, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vito vyake vya thamani.
I will greatly rejoice in the LORD, my soul shall be joyful in my God; for He hath clothed me with the garments of salvation, He hath covered me with the robe of victory, as a bridegroom putteth on a priestly diadem, and as a bride adorneth herself with her jewels.
11 Kwa maana kama vile ardhi ifanyavyo chipukizi kuota, na bustani isababishavyo mbegu kuota, ndivyo Bwana Mwenyezi atafanya haki na sifa zichipuke mbele ya mataifa yote.
For as the earth bringeth forth her growth, and as the garden causeth the things that are sown in it to spring forth; so the Lord GOD will cause victory and glory to spring forth before all the nations.

< Isaya 61 >