< Isaya 6 >

1 Katika mwaka ule Mfalme Uzia alikufa, nilimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu na kilichotukuzwa sana, nalo pindo la joho lake likajaza Hekalu.
Godine koje umrije car Ozija vidjeh Gospoda gdje sjedi na prijestolu visoku i izdignutu, i skut mu ispunjavaše crkvu.
2 Juu yake walikuwepo maserafi, kila mmoja alikuwa na mabawa sita: Kwa mabawa mawili walifunika nyuso zao, kwa mengine mawili walifunika miguu yao, na kwa mawili walikuwa wakiruka.
Serafimi stajahu više njega, svaki ih imaše šest krila: dvjema zaklanjaše lice svoje i dvjema zaklanjaše noge svoje, a dvjema leæaše.
3 Nao walikuwa wakiitana kila mmoja na mwenzake: “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu ni Bwana Mwenye Nguvu Zote; dunia yote imejaa utukufu wake.”
I vikahu jedan drugome govoreæi: svet, svet, svet je Gospod nad vojskama; puna je sva zemlja slave njegove.
4 Kwa sauti zao, miimo ya milango na vizingiti vilitikisika, nalo Hekalu likajaa moshi.
I zadrmaše se pragovi na vratima od glasa kojim vikahu, i dom se napuni dima.
5 Ndipo nikalia, “Ole wangu! Nimeangamia! Kwa kuwa mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninaishi katikati ya watu wenye midomo michafu, nayo macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
I rekoh: jaoh meni! pogiboh, jer sam èovjek neèistijeh usana, i živim usred naroda neèistijeh usana, jer cara Gospoda nad vojskama vidjeh svojim oèima.
6 Ndipo mmoja wa wale maserafi akaruka kunijia akiwa na kaa la moto linalowaka mkononi mwake, ambalo alikuwa amelichukua kwa koleo kutoka madhabahuni.
A jedan od serafima doletje k meni držeæi u ruci živ ugljen, koji uze s oltara kliještima,
7 Akanigusa nalo kinywa changu na kusema, “Tazama, hili limegusa midomo yako, uovu wako umeondolewa, nayo dhambi yako imesamehewa.”
I dotaèe se usta mojih i reèe: evo, ovo se dotaèe usta tvojih, i bezakonje tvoje uze se, i grijeh tvoj oèisti se.
8 Kisha nikasikia sauti ya Bwana ikisema, “Nimtume nani? Ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?” Nami nikasema, “Mimi hapa. Nitume mimi!”
Potom èuh glas Gospodnji gdje reèe: koga æu poslati? i ko æe nam iæi? A ja rekoh: evo mene, pošlji mene.
9 Akasema, “Nenda ukawaambie watu hawa: “‘Mtaendelea daima kusikiliza, lakini kamwe hamtaelewa; mtaendelea daima kutazama, lakini kamwe hamtatambua.’
A on reèe: idi, i reci tome narodu: slušajte ali neæete razumjeti, gledajte ali neæete poznati.
10 Fanya mioyo ya watu hawa kuwa migumu, fanya masikio yao yasisikie, na upofushe macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, nao wakageuka, nikawaponywa.”
Uèini da odeblja srce tome narodu i uši da im otežaju, i oèi im zatvori, da ne vide oèima svojim i ušima svojim da ne èuju i srcem svojim da ne razumiju i ne obrate se i ne iscijele.
11 Ndipo nikasema, “Hadi lini, Ee Bwana?” Naye akanijibu: “Hadi miji iwe imeachwa magofu na bila wakazi, hadi nyumba zitakapobaki bila watu, na mashamba yatakapoharibiwa na kuangamizwa,
A ja rekoh: dokle Gospode? A on reèe: dokle ne opuste gradovi da budu bez stanovnika i kuæe da budu bez ljudi, i zemlja dokle sasvijem ne opusti,
12 hadi Bwana atakapokuwa amekwisha kumpeleka kila mmoja mbali sana, na nchi itakapokuwa imeachwa kabisa.
I dokle Gospod opravi daleko ljude i bude sama pustoš u zemlji.
13 Hata kama sehemu ya kumi ya watu watabaki katika nchi, itaharibiwa tena. Lakini kama vile mvinje na mwaloni ibakizavyo visiki inapokatwa, ndivyo mbegu takatifu itakavyokuwa kisiki katika nchi.”
Ali æe još biti u njoj desetina, pa æe se i ona zatrti; ali kao hrast ili brijest kojima i kad zbace lišæe ostaje stablo, tako æe sveto sjeme biti njezino stablo.

< Isaya 6 >