< Isaya 6 >

1 Katika mwaka ule Mfalme Uzia alikufa, nilimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu na kilichotukuzwa sana, nalo pindo la joho lake likajaza Hekalu.
During the year that King Uzziah died, [Yahweh showed me a vision. In the vision], I saw Yahweh sitting on a throne, high above everyone. He [was wearing a very long] robe that covered [the floor of] the temple.
2 Juu yake walikuwepo maserafi, kila mmoja alikuwa na mabawa sita: Kwa mabawa mawili walifunika nyuso zao, kwa mengine mawili walifunika miguu yao, na kwa mawili walikuwa wakiruka.
Above him were standing [several] winged creatures. Each of them had six wings. They covered their faces with two of their wings, they covered their feet with two of their wings, and they flew using two of their wings.
3 Nao walikuwa wakiitana kila mmoja na mwenzake: “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu ni Bwana Mwenye Nguvu Zote; dunia yote imejaa utukufu wake.”
They were calling to each other, saying, “The Commander of the armies of angels is holy; he is completely holy! The entire earth is filled with his glory.”
4 Kwa sauti zao, miimo ya milango na vizingiti vilitikisika, nalo Hekalu likajaa moshi.
When they spoke, it caused the doorposts of the temple to shake, and the temple was filled with smoke.
5 Ndipo nikalia, “Ole wangu! Nimeangamia! Kwa kuwa mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninaishi katikati ya watu wenye midomo michafu, nayo macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
Then I said, “Terrible things will happen to me, because everything that I say [MTY] is sinful, and I live among people who constantly say [MTY] sinful things. I will be destroyed because I have seen the Commander of the armies of angels!”
6 Ndipo mmoja wa wale maserafi akaruka kunijia akiwa na kaa la moto linalowaka mkononi mwake, ambalo alikuwa amelichukua kwa koleo kutoka madhabahuni.
Then one of the winged creatures took a hot coal from the altar, using a pair of tongs. He flew to me
7 Akanigusa nalo kinywa changu na kusema, “Tazama, hili limegusa midomo yako, uovu wako umeondolewa, nayo dhambi yako imesamehewa.”
and touched my lips with the coal. Then he said, “Look [at what I have done]. I have touched your lips [with this coal]. [Now] your guilt is ended, and your sins are forgiven [DOU].”
8 Kisha nikasikia sauti ya Bwana ikisema, “Nimtume nani? Ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?” Nami nikasema, “Mimi hapa. Nitume mimi!”
Then I heard Yahweh asking, “Whom shall I send [to be a messenger to my people]? Who will go [and speak] for us?” I replied, “I will. Send me!”
9 Akasema, “Nenda ukawaambie watu hawa: “‘Mtaendelea daima kusikiliza, lakini kamwe hamtaelewa; mtaendelea daima kutazama, lakini kamwe hamtatambua.’
Then he said, “[Okay], go, and say to the [Israeli] people, ‘You will listen carefully [to what I say], but you will not understand it. You will look very carefully [at the things that I am doing], but you will not understand them.’
10 Fanya mioyo ya watu hawa kuwa migumu, fanya masikio yao yasisikie, na upofushe macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, nao wakageuka, nikawaponywa.”
[What you(sg) say will] cause these people to become stubborn [IDM]; [it will cause them] to not be able to hear [what I say] and see [what I do]. [As a result, they will not] see [what I want them to see] or hear [what I want them to hear], and they will not understand it, and they will not turn to me and be saved [from being punished].”
11 Ndipo nikasema, “Hadi lini, Ee Bwana?” Naye akanijibu: “Hadi miji iwe imeachwa magofu na bila wakazi, hadi nyumba zitakapobaki bila watu, na mashamba yatakapoharibiwa na kuangamizwa,
Then I said, “How long [do you want me to continue to do that]?” He replied, “[Do it] until their cities are ruined [by their enemies], [until] no one is living in their houses, [do it until] all the crops are stolen from their fields and the fields are ruined.
12 hadi Bwana atakapokuwa amekwisha kumpeleka kila mmoja mbali sana, na nchi itakapokuwa imeachwa kabisa.
[Do it] until I have (exiled everyone/forced everyone to go to their enemies’ lands) far away, and the whole land [of Israel] is deserted.
13 Hata kama sehemu ya kumi ya watu watabaki katika nchi, itaharibiwa tena. Lakini kama vile mvinje na mwaloni ibakizavyo visiki inapokatwa, ndivyo mbegu takatifu itakavyokuwa kisiki katika nchi.”
If [even] one tenth [of the people survive and] stay there, [their enemies] will [invade the land again and] burn everything. [But, just] like [MET] when an oak [tree] is cut down, a stump is left [from which new shoots will grow], the people who remain [in this land will be a group that will become large again] and be (set apart for/dedicated to) me.”

< Isaya 6 >