< Isaya 6 >

1 Katika mwaka ule Mfalme Uzia alikufa, nilimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu na kilichotukuzwa sana, nalo pindo la joho lake likajaza Hekalu.
I Kong Uzzijas Dødsaar saa jeg Herren sidde paa en saare høj Trone, og hans Slæb fyldte Helligdommen.
2 Juu yake walikuwepo maserafi, kila mmoja alikuwa na mabawa sita: Kwa mabawa mawili walifunika nyuso zao, kwa mengine mawili walifunika miguu yao, na kwa mawili walikuwa wakiruka.
Serafer stod hos ham, hver med seks Vinger; med de to skjulte de Ansigtet, med de to Fødderne, og med de to fløj de;
3 Nao walikuwa wakiitana kila mmoja na mwenzake: “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu ni Bwana Mwenye Nguvu Zote; dunia yote imejaa utukufu wake.”
og de raabte til hverandre: »Hellig, hellig, hellig er Hærskarers HERRE, al Jorden er fuld af hans Herlighed!«
4 Kwa sauti zao, miimo ya milango na vizingiti vilitikisika, nalo Hekalu likajaa moshi.
Og Dørstolpernes Hængsler rystede ved Raabet, medens Templet fyldtes af Røg.
5 Ndipo nikalia, “Ole wangu! Nimeangamia! Kwa kuwa mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninaishi katikati ya watu wenye midomo michafu, nayo macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
Da sagde jeg: »Ve mig, det er ude med mig, thi jeg er en Mand med urene Læber, og jeg bor i et Folk med urene Læber, og nu har mine Øjne set Kongen, Hærskarers HERRE!«
6 Ndipo mmoja wa wale maserafi akaruka kunijia akiwa na kaa la moto linalowaka mkononi mwake, ambalo alikuwa amelichukua kwa koleo kutoka madhabahuni.
Men en af Seraferne fløj hen til mig; og han havde i Haanden et glødende Kul, som han med en Tang havde taget fra Alteret;
7 Akanigusa nalo kinywa changu na kusema, “Tazama, hili limegusa midomo yako, uovu wako umeondolewa, nayo dhambi yako imesamehewa.”
det lod han røre min Mund og sagde: »Se, det har rørt dine Læber; din Skyld er borte, din Synd er sonet!«
8 Kisha nikasikia sauti ya Bwana ikisema, “Nimtume nani? Ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?” Nami nikasema, “Mimi hapa. Nitume mimi!”
Saa hørte jeg Herren sige: »Hvem skal jeg sende, hvem vil gaa Bud for os?« Og jeg sagde: »Her er jeg, send mig!«
9 Akasema, “Nenda ukawaambie watu hawa: “‘Mtaendelea daima kusikiliza, lakini kamwe hamtaelewa; mtaendelea daima kutazama, lakini kamwe hamtatambua.’
Da sagde han: »Gaa hen og sig til dette Folk: Hør kun, dog skal I intet fatte, se kun, dog skal I intet indse!
10 Fanya mioyo ya watu hawa kuwa migumu, fanya masikio yao yasisikie, na upofushe macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, nao wakageuka, nikawaponywa.”
Gør Hjertet sløvt paa dette Folk, gør dets Ører tunge, dets Øjne blinde, saa det ikke kan se med Øjnene, ej heller høre med Ørene, ej heller fatte med Hjertet og omvende sig og læges.«
11 Ndipo nikasema, “Hadi lini, Ee Bwana?” Naye akanijibu: “Hadi miji iwe imeachwa magofu na bila wakazi, hadi nyumba zitakapobaki bila watu, na mashamba yatakapoharibiwa na kuangamizwa,
Jeg spurgte: »Hvor længe, Herre?« Og han svarede: »Til Byerne er øde, uden Beboere, og Husene uden et Menneske, og Agerjorden ligger som Ørk!«
12 hadi Bwana atakapokuwa amekwisha kumpeleka kila mmoja mbali sana, na nchi itakapokuwa imeachwa kabisa.
Og HERREN vil fjerne Menneskene, og Tomhed skal brede sig i Landet;
13 Hata kama sehemu ya kumi ya watu watabaki katika nchi, itaharibiwa tena. Lakini kama vile mvinje na mwaloni ibakizavyo visiki inapokatwa, ndivyo mbegu takatifu itakavyokuwa kisiki katika nchi.”
og er der endnu en Tiendedel deri, skal ogsaa den udryddes som en Terebinte eller Eg, af hvilken en Stub bliver tilbage, naar den fældes. Dens Stub er hellig Sæd.

< Isaya 6 >