< Isaya 58 >
1 “Piga kelele, usizuie. Paza sauti yako kama tarumbeta. Watangazieni watu wangu uasi wao, na kwa nyumba ya Yakobo dhambi zao.
Crie à plein gosier, ne te retiens pas; élève ta voix comme une trompette; déclare à mon peuple leur iniquité, à la maison de Jacob ses péchés!
2 Kwa maana kila siku hunitafuta, wanaonekana kutaka kujua njia zangu, kana kwamba walikuwa taifa linalotenda lililo sawa, na ambalo halijaziacha amri za Mungu wake. Hutaka kwangu maamuzi ya haki, nao hutamani Mungu awakaribie.
Car, jour après jour, ils me cherchent et ils veulent connaître mes voies, comme une nation qui aurait pratiqué la justice et n'aurait pas abandonné la loi de son Dieu; ils me demandent des jugements justes, ils veulent s'approcher de Dieu:
3 Wao husema, ‘Mbona tumefunga, nawe hujaona? Mbona tumejinyenyekeza, nawe huangalii?’ “Lakini katika siku ya kufunga kwenu, mnafanya mnavyotaka na kuwadhulumu wafanyakazi wenu wote.
Pourquoi avons-nous jeûné, sans que tu y prisses garde, et affligé nos âmes, sans que tu le connusses? Voici, dans votre jour de jeûne, vous faites votre volonté et vous traitez durement tous vos mercenaires.
4 Kufunga kwenu huishia kwenye magomvi na mapigano, na kupigana ninyi kwa ninyi kwa ngumi za uovu. Hamwezi kufunga kama mnavyofanya leo na kutazamia sauti zenu kusikiwa huko juu.
Voici, vous jeûnez pour quereller et disputer, et pour frapper du poing méchamment; vous ne jeûnez pas comme le veut ce jour, pour que votre voix soit entendue en haut.
5 Je, hii ndiyo aina ya mfungo niliouchagua, siku moja tu ya mtu kujinyenyekeza? Je, ni kwa kuinamisha kichwa chini kama tete, na kwa kujilaza juu ya nguo ya gunia na majivu? Je, huo ndio mnaouita mfungo, siku iliyokubalika kwa Bwana?
Est-ce là le jeûne auquel je prends plaisir, un jour où l'homme afflige son âme? Est-ce de courber sa tête comme un jonc, de se coucher sur le sac et la cendre? Appelleras-tu cela un jeûne, un jour agréable à l'Éternel?
6 “Je, hii si ndiyo aina ya mfungo niliyoichagua: kufungua minyororo ya udhalimu, na kufungua kamba za nira, kuwaweka huru walioonewa, na kuvunja kila nira?
N'est-ce pas plutôt ici le jeûne auquel je prends plaisir, qu'on dénoue les liens de la méchanceté, qu'on délie les courroies du joug, qu'on renvoie libres les opprimés, et que tout joug soit brisé?
7 Je, sio kushirikiana chakula chako na wenye njaa na kuwapatia maskini wasiokuwa na makao hifadhi, unapomwona aliye uchi, umvike, wala si kumkimbia mtu wa nyama na damu yako mwenyewe?
N'est-ce pas que tu partages ton pain avec l'affamé; que tu fasses entrer dans ta maison les malheureux errants; que tu revêtes ceux que tu vois nus, et ne te détournes pas de ton semblable?
8 Ndipo nuru yako itajitokeza kama mapambazuko na uponyaji wako utatokea upesi; ndipo haki yako itakapokutangulia mbele yako, na utukufu wa Bwana utakuwa mlinzi nyuma yako.
Alors ta lumière poindra comme l'aurore, et ta guérison se montrera promptement; ta justice ira devant toi, et la gloire de l'Éternel sera ton arrière-garde.
9 Ndipo utaita, naye Bwana atajibu, utalia kuomba msaada, naye atasema: Mimi hapa. “Kama ukiiondoa nira ya udhalimu, na kunyoosha kidole na kuzungumza maovu,
Alors tu appelleras, et l'Éternel répondra; tu crieras, et il dira: Me voici! Si tu ôtes du milieu de toi l'oppression, le doigt levé insolemment, et les paroles criminelles;
10 nanyi kama mkimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi zenu na kutosheleza mahitaji ya walioonewa, ndipo nuru yenu itakapongʼaa gizani, nao usiku wenu utakuwa kama adhuhuri.
Si tu fais part de ta subsistance à l'affamé, et que tu rassasies l'âme affligée, ta lumière se lèvera dans l'obscurité, et tes ténèbres seront comme le midi.
11 Bwana atakuongoza siku zote, atayatosheleza mahitaji yako katika nchi kame, naye ataitia nguvu mifupa yako. Utakuwa kama bustani iliyonyweshwa vizuri, kama chemchemi ambayo maji yake hayakauki kamwe.
L'Éternel te conduira continuellement; il te rassasiera dans les lieux arides; il donnera la vigueur à tes os, et tu seras comme un jardin arrosé, comme une source dont les eaux ne trompent jamais.
12 Watu wako watajenga tena magofu ya zamani na kuinua misingi ya kale; utaitwa Mwenye Kukarabati Kuta Zilizobomoka, Mwenye Kurejeza Barabara za Makao.
Les tiens rebâtiront les antiques ruines, tu relèveras les fondations des anciens âges; on t'appellera le réparateur des brèches, le restaurateur des chemins, qui rend le pays habitable.
13 “Kama ukitunza miguu yako isivunje Sabato, na kutokufanya kama vile upendavyo katika siku yangu takatifu, kama ukiita Sabato siku ya furaha na siku takatifu ya Bwana ya kuheshimiwa, kama utaiheshimu kwa kutoenenda katika njia zako mwenyewe, na kutokufanya yakupendezayo au kusema maneno ya upuzi,
Si tu retiens ton pied au jour du sabbat, pour ne pas faire ta volonté dans mon saint jour; si tu appelles le sabbat tes délices, et honorable ce qui est consacré à l'Éternel; si tu l'honores plutôt que de suivre tes voies, de faire ta volonté et de dire des paroles vaines:
14 ndipo utakapojipatia furaha yako katika Bwana, nami nitakufanya upande juu ya miinuko ya nchi na kusherehekea urithi wa Yakobo baba yako.” Kinywa cha Bwana kimenena haya.
Alors tu trouveras des délices en l'Éternel; je te ferai passer par-dessus les hauteurs du pays, et je te nourrirai de l'héritage de Jacob, ton père; car la bouche de l'Éternel a parlé.