< Isaya 58 >
1 “Piga kelele, usizuie. Paza sauti yako kama tarumbeta. Watangazieni watu wangu uasi wao, na kwa nyumba ya Yakobo dhambi zao.
Call out with a throat may not you refrain like trumpet raise voice your and declare to people my transgression their and to [the] house of Jacob sins their.
2 Kwa maana kila siku hunitafuta, wanaonekana kutaka kujua njia zangu, kana kwamba walikuwa taifa linalotenda lililo sawa, na ambalo halijaziacha amri za Mungu wake. Hutaka kwangu maamuzi ya haki, nao hutamani Mungu awakaribie.
And me day day they seek! and [the] knowledge of ways my they desire! like a nation which righteousness it has done and [the] judgment of God its not it has forsaken they ask me judgments of righteousness [the] approach of God they desire!
3 Wao husema, ‘Mbona tumefunga, nawe hujaona? Mbona tumejinyenyekeza, nawe huangalii?’ “Lakini katika siku ya kufunga kwenu, mnafanya mnavyotaka na kuwadhulumu wafanyakazi wenu wote.
Why? have we fasted and not you have seen have we humbled? self our and not you know there! on [the] day of fasting your you find pleasure and all laborers your you drive hard.
4 Kufunga kwenu huishia kwenye magomvi na mapigano, na kupigana ninyi kwa ninyi kwa ngumi za uovu. Hamwezi kufunga kama mnavyofanya leo na kutazamia sauti zenu kusikiwa huko juu.
There! for strife and contention you fast and to strike with a fist of wickedness not you fast like this day to make heard in the height[s] voice your.
5 Je, hii ndiyo aina ya mfungo niliouchagua, siku moja tu ya mtu kujinyenyekeza? Je, ni kwa kuinamisha kichwa chini kama tete, na kwa kujilaza juu ya nguo ya gunia na majivu? Je, huo ndio mnaouita mfungo, siku iliyokubalika kwa Bwana?
¿ Like this is it [the] fast [which] I choose it a day to humble anyone self his ¿ to bend down like a bulrush head his and sackcloth and ash[es] he spreads as a bed ¿ this do you call a fast and a day of acceptance to Yahweh.
6 “Je, hii si ndiyo aina ya mfungo niliyoichagua: kufungua minyororo ya udhalimu, na kufungua kamba za nira, kuwaweka huru walioonewa, na kuvunja kila nira?
¿ Not [is] this [the] fast [which] I choose it to loosen [the] bonds of wickedness to unfasten [the] bindings of [the] yoke-bar and to let go crushed [people] free [people] and every yoke-bar you will tear apart.
7 Je, sio kushirikiana chakula chako na wenye njaa na kuwapatia maskini wasiokuwa na makao hifadhi, unapomwona aliye uchi, umvike, wala si kumkimbia mtu wa nyama na damu yako mwenyewe?
¿ Not [is it] to break for the hungry [person] bread your and poor [people] homeless people you will bring a house if you will see [the] naked and you will cover him and from own flesh your not you will hide yourself.
8 Ndipo nuru yako itajitokeza kama mapambazuko na uponyaji wako utatokea upesi; ndipo haki yako itakapokutangulia mbele yako, na utukufu wa Bwana utakuwa mlinzi nyuma yako.
Then it will break forth like the dawn light your and healing your quickly it will spring up and it will go before you righteousness your [the] glory of Yahweh it will be rearguard your.
9 Ndipo utaita, naye Bwana atajibu, utalia kuomba msaada, naye atasema: Mimi hapa. “Kama ukiiondoa nira ya udhalimu, na kunyoosha kidole na kuzungumza maovu,
Then you will call and Yahweh he will answer you will cry for help and he may say here [am] I if you will remove from among you [the] yoke-bar [the] stretching out of a finger and [the] speaking of wickedness.
10 nanyi kama mkimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi zenu na kutosheleza mahitaji ya walioonewa, ndipo nuru yenu itakapongʼaa gizani, nao usiku wenu utakuwa kama adhuhuri.
And you will offer to the hungry [person] self your and [the] appetite of [the] afflicted you will satisfy and it will rise in the darkness light your and gloom your [will be] like the noon.
11 Bwana atakuongoza siku zote, atayatosheleza mahitaji yako katika nchi kame, naye ataitia nguvu mifupa yako. Utakuwa kama bustani iliyonyweshwa vizuri, kama chemchemi ambayo maji yake hayakauki kamwe.
And he will lead you Yahweh continually and he will satisfy in arid regions appetite your and bones your he will strengthen and you will be like a garden watered and like a spring of waters which not they will fail waters its.
12 Watu wako watajenga tena magofu ya zamani na kuinua misingi ya kale; utaitwa Mwenye Kukarabati Kuta Zilizobomoka, Mwenye Kurejeza Barabara za Makao.
And they will rebuild some of you [the] ruins of antiquity [the] foundations of a generation and a generation you will raise up and it will be called to you [one who] walls up a breach [one who] restores paths to dwell in.
13 “Kama ukitunza miguu yako isivunje Sabato, na kutokufanya kama vile upendavyo katika siku yangu takatifu, kama ukiita Sabato siku ya furaha na siku takatifu ya Bwana ya kuheshimiwa, kama utaiheshimu kwa kutoenenda katika njia zako mwenyewe, na kutokufanya yakupendezayo au kusema maneno ya upuzi,
If you will turn back from [the] sabbath foot your to do pleasures your on [the] day of holiness my and you will call the sabbath a delight [the] holy [day] of Yahweh honorable and you will honor it from doing own ways your from finding pleasure your and to speak a word.
14 ndipo utakapojipatia furaha yako katika Bwana, nami nitakufanya upande juu ya miinuko ya nchi na kusherehekea urithi wa Yakobo baba yako.” Kinywa cha Bwana kimenena haya.
Then you will take delight on Yahweh and I will make ride you on ([the] high places of *Q(k)*) [the] land and I will feed you [the] inheritance of Jacob ancestor your for [the] mouth of Yahweh it has spoken.